Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

UPUPU wa kutaka kumchafua Lowassa na Rostam.

Hata mkifanyaje tunawajua wala hatushikiki. Good story telling though.

Kumchafua kwani alisafishwa lini baada ya Richmond? Nani kamsafisha maana mwenyewe hakuweza kujisafisha. na leo tunadaiwa 111bilioni kwa kukaa kimya kwake? Mtu wa jinsi hii asiye na ujasiri kutuokoa na malipo makubwa kiasi hiki kwa kumjali zaidi rafiki yake JK kuliko watanzania masikini ndio unataka anataka kutuomba atuongoze?Hivi kati ya watanzania masikini na Jk anampenda nani?
 
CHADEMA wanajidanganya. Nakubali ndio watashinda kula za urais, hilo halina ubishi, ila EL ndiye atakayeapishwa kuwa rais.
Wasichojua ni kwamba, unaweza kulinda kura za udiwani na ubunge, lakini za Uraisi ni ngumu sana.
Hivi nchi hii imekosa waadilifu mpaka tumfikirie EL? EL na kundi lake pamoja na Sita na kundi lao la wapambanaji feki wa ufisadi wote wameprove kukosa ujasiri wa kusimama upande wa waTZ masikini.
 
Wizi mtupu... Wabongo kwa kuunganisha dot hamjambo.

Kuna mambo umesema kweli, kama la Karume kuwa makamu wa rais wa Lowassa, hii ni project yao wawili wala haina baraka za Mkapa, huo ni uongo!

Kuhusu Karume kumhenyesha Jakaya huko Butiama ni uongo, kama ulikuwepo kule unadhani Karume kwanini alilia machozi kule? Na kama alimhenyesha ilikuwaje katiba ya Zanzibar haikubadilika kumruhusu agombee tena urais wa Zanzibar kama alivyopenda yeye na genge lake?

Shein kwenda kuwa rais Zanzibar ni uoga wa Lowassa na genge lake kumhofia Shein kwamba akijengewa hoja kumrithi Jakaya itakuwa rahisi kuwashinda kwa kuwa angekuwa tayari na uzoefu kama vice president kwa term 3 na pia ni mzanzibari na kama unavyojua ni muda sasa wazanzibari hawajakikalia hicho kiti alichokalia Jakaya muda huu... wakamleta mchovu Bilal ambaye ni unfit kiafya wakijua after 5 years atakua amaechakaa zaidi na kusubiri huruma ya kupewa ugombea mwenza tena..

Nina mengi pia ngoja niyabane, nakusubiri urudi...
 
swali hapa ni hilik
ama huyo kingmaker ana nguvu saana
why alijiuzulu na kukubali kuitwa fisadi????????

mwanangu we sikiliza tu hizo porojo za hao jamaa....wanapoteza muda,rostam is a dead person politically,lakini kuna watu bado wanapenda kuishi na kivuli chake,hatuna jinsi ya kuwasaidia....
 
Kwa nyongeza tu, hata uteuzi wa EL kuwa PM, Mkapa hakukubaliana nao. Chaguo la Mkapa ilikuwa ni John Pombe Magufuli.
uongozo please - chaguo la Mkapa lilikuwa Pinda awe PM wa Jakaya sio Magufuli...
 
Hutaki Unaacha na Wana JF,

Wala sitaki kuamini kilichoandikwa na kama ni cha kweli tumeliwa Watanzania

Sitaki kupata picha Mkuu wetu wa kaya alivyozungukwa, ndio maana napata picha kiburi cha Rashid Hamad juu ya Maalim Seif.

Niliamini Hamad hawezi kuwa na jeuri na Maalim amenywea hivyo, anajua siri za Maalim.

Pili uchaguzi wa Igunga unanipa picha kamili ya hadithi hii, Kampeni zimeongozwa na Mzee Mzima BMW.

Kwa picha ilivyo, ni Watanzania tu wanaweza kutengua kitendawili hiki.
So far am speechless

Nawakilisha
 
Nami pia natoa thanks kwa mtoa mada, ila natoa tahadhari humu jf tuwe waangalifu sana hasa na watu wote wanaotuambia we are too late hakuna tunaloweza kufanya. Hawa ni ma agents wa mafisadi na wanafanya hivyo kutukatisha tamaa, jamani wameweza wa Libya na hata warusi leo hii wanamkataa Putin, sisi pia tunaweza hawa watu si chochote si lolote, huyo king maker ni ku mu eliminate tu sema makomandoo wetu ndio kituko kuliko hata hao ma recruit, hivi wanajiita kweli makomandoo ama ndio wale wa maonyesho ya uwanja wa taifa?

Kama wewe umekata tamaa, sisi tulio na watoto tumekataa kuwaruhusu monkeys watule sisi na watoto wetu, tutapigana mpaka tone la mwisho hata ikibidi kuingia mitini tuko tayari
 
Hivi nchi hii imekosa waadilifu mpaka tumfikirie EL? EL na kundi lake pamoja na Sita na kundi lao la wapambanaji feki wa ufisadi wote wameprove kukosa ujasiri wa kusimama upande wa waTZ masikini.

Inaonekana kwamba watz tulikuwa tunamwogopa sana Nyerere. Baada ya kuondoka kwa Nyerere, mambo mengi sana ya hivyo hovyo yametokea.

Wana JF: Hebu jikumbusheni kuhusu huyo kipenzi chenu EDWARD LOWASA:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/11092-salaam-kwa-mh-edward-lowassa-na-wenzake.html
 
Mkuu FP hapa si JF where we dare to talk openly!? Sasa kama una sababu zako muhimu za kumkubali Lowassa kwanini usiziweke hadharani ili kujaribu kuwashawishi wengine kwamba Lowassa anafaa kuchukua nchi 2015!? Mie sioni sababu ya kwenda PM zimwage sababu hizo hadharani.

Mkuu Hutaki Unaacha tunakusubiri kwa hamu kuu uendelee na part 2 ya habari hii. Usikawie sana kurudi tena jamvini.
Mkuu BAK, FP is right kutumia PM kwa mambo mengine, safari ya kuelekea 2015 ni safari ya kweli na timu za ukweli zipo, na mbinu safi na chafu za ukweli zipo!.

Sasa kama mimi nimetokea kunusa mahali, watu wanakuotea vibaya wewe BAK, kama mtu makini, sitakuibukia open, nita ku PM.

Kwenye hili la Lowassa, kuna mahali FP anaposimamia, hata Mzee Mwanakijiji avyopafahamu, nae sasa anasimama na Lowassa!.

Msome Mkuu Mkandara post no 132 hapo juu, amesema nanukuu Lowassa "It's a blessing! - bring it on!". Sasa kwa wale wazito kabisa kuelewa, ni wa kueleweshwa kwa pm, adui akijua route yako, anaweza kukuzungukia na kukumaliza kwa ambush!
 
Aaaah mwenzako vya kunyonga siviwezi...
On the otherhand though, I think CCM wakimsimamisha Lowassa ..It's a blessing! - bring it on!
Mkuu Mkandara, there you are, now we sail the same boat!, now join the team, tumsafishe Lowassa, tumpake mafuta angare na kumeremeta, na tumpulizia manukato ya manemane anukie vizuri kila apitapo harufu ya kunukia inatangulia, hivyo kuwavuta wote wapendao vingaavyo na vinukiavyo!.

Now join the timu, sio lazima ki waziwasi kama sisi, hata kwa kunyamaza tuu na kutombomoa zaidi Lowassa, hiyo inatutosha!

Welcome on board!
 
Duh! kuja kufikia 2015 tutayasikia mengi juu ya viongozi wetu wa Nchi.
 
bring it on! We need that part 2, ili tuweze kuunganisha dots.
 
hapa kuna mtu anapigiwa kampain ya urais, soma vizuri huo waraka utauelewa, hii ni vita ya urais, before 2015 tutaona mengi, na uzuri mengi ya uvunguni yatafunuliwa.
 
Watanzania,

Hivi kweli mnapenda story za udaku namna hii?
Why unatusemea kwanza tumekuuliza? Tuache sisi wenyewe tuamue kama ni story ya uongo au ya ukweli na sio wewe ndio useme wewe vipi? Kama una watetea hao mafisadi kakojoe ulale... Apoteze mda kuja kuwakandia watu ili iweje sasa?
 
Mkuu Mkandara, there you are, now we sail the same boat!, now join the team, tumsafishe Lowassa, tumpake mafuta angare na kumeremeta, na tumpulizia manukato ya manemane anukie vizuri kila apitapo harufu ya kunukia inatangulia, hivyo kuwavuta wote wapendao vingaavyo na vinukiavyo!.

Now join the timu, sio lazima ki waziwasi kama sisi, hata kwa kunyamaza tuu na kutombomoa zaidi Lowassa, hiyo inatutosha!

Welcome on board!

mkuu km lowasa anastahili kubomolewa kwanini asibomolewe?
mkuu wewe kila siku unaomba ushahidi wa ufisadi wa lowasa, km ushahidi upo usitolewe kwakuwa lowasa anahitajika sana nchi hii kuwa rais kuliko mtu mwingine yeyote?
 
Wewe una njaa wewe halafu inaonekana ulikuwapo kwny mtandao ukapigwa chini sasa unaleta chuki zako hapa. Waganga njaa wa aina yako tunao wengi Sana. Huu ni ujanja wa kutaka kufitinisha watu tu, huna lolote
 
Mr President,

Ningekuwa na muda ningekueleza mengi sana. Muda wangu ni kidogo sana ndiyo maana nashindwa hata kupost mambo mengi kuhusu taifa hili hapa JF. Ninatuma post hii si kwa lengo la kukutisha. Lengo ni kukukumbusha uwe makini ili usijefanya uamuzi wa hovyo na kuliingiza taifa katika machafuko na kuharibu timetable za watanzania. Machafuko ndiyo tunayoyakwepa lakini si wewe (I have to tell you the truth because you are not my breadwinner at all).
Hapa huyu Hutaki Unaacha, amejitambulisha vizuri, kuwa ameandika haya, sio ili kumtisha jk, bali kumpa warning na pia kujitanabaisha, yeye hamtegemei jk kuishi, hivyo huyu ni mtu wa TISS! aliyekereka na mambo yalivyokwenda na yanavyo kwenda! nawashauri japo tusimwaminie 100% kwa 100%, but sio wa kupuuzwa hata kidogo!. Mimi naendelea kuisoma makala yake mara mbili mbili na kila nikisoma, napata vitu vipya!

Ninachozungumzia hapa ni kundi kubwa na hatari linaloaminika kuongozwa na Edward, Rostam, Othman, Apson, Karume na Shein na Mkapa. Ninakufahamu vizuri sana na ungekuwa uwezo wako, hawa wote ungeweza kufanya uwezalo ili kumweka madarakani mtu unayemtaka kwa maana ya Asha au Nahodha. Huu ni mtandao unaofanya kazi kwa umakini wa hali ya juu sana. Ukitaka kuamini, jiulize swali la kipuuzi sana kuwa kwanini kila plans unazofanya (zisizo na faida) kwa kundi hili zote zimefail?
Kumbe JK anamtaka Nahodha na Asha?. Hapa jamaa amechapia!, JK anamtaka Shein, Asha ndie makamo wake! Naodha anarudi Zanzibar kuwa rais, Makamo wake ni Dr. Mwinyi!. Kitu ambacho CCM hawajui ni kuwa 2015 Zanzibar ni zamu ya CUF! na wakikashinda watavunja muafaka ..mtaniambia!

1. Shein ni nani?
Nataka nikukumbushe ''issue'' ya Omar Juma. Huyu alikuwa threat kubwa kwa kundi lenu kwa ajili ya 2005. Mtandao wake ukibebwa na Mkapa ulikuwa ni hatari sana. The only way ilikuwa ni ''kumwondoa'' na hilo liliwezekana. Siku nikiwa na muda nitaeleza mchezo wote ulivyofanyika. Wakati jina limeletwa tukiwa hotel moja maarufu hapa Dar, nakumbuka hukuweza kumfahamu Shein wala kulitamka jina lake vizuri. Ulikosea mara tatu kulitamka. Tukacheka wote. Hatimaye Shein akawa makamu wa rais.
Kumbe Dr. Omar, aliondolewa!, japo binafsi siamini!, nikiamini kifo chake ilikuwa ni kazi ya Mwenyeenzi Mungu, ila hii hoja jina lilitetwa wakiwa hoteli moja na eti jina la Shein lilikosewa mara tatu mpaka watu wakacheka!, hili jina la Shein lina ugumu gani mpaka likosewe mara tatu?. Hii ni fix!

Baada ya wenzako kukuweka madarakani (mgombea ndani ya CCM), kosa ambalo Shein hataweza kukusamehe katika maisha yake (Mimi sio Mungu, kwani anaweza kukusamehe vilevile) ni pale ulipo-attempt kumfanya Zakhia kuwa makamu wa rais. Asingekuwa Edward, Rostam, Mkapa na Karume, leo hii Shein angekuwa mwenyekiti wa TPDC au TANAPA!. Kitendo cha Shein kuletwa na kundi hili, kutetewa na kundi hili achilia mbali kushawishiwa na kundi hili agombee urais wa Zanzibar ili kummaliza nguvu Nahodha chaguo lako kinamfanya awe mtiifu kwao kuliko hata kwa Mwanamwema!. Unafahamu vizuri Shein alivyoshinda urais Zanzibar, rafiki zako walikuchezea akili wakikuambia kuwa wamemleta Shein ili kupunguza kura za Bilal na ulipomkubali Shein wao wakaenda kumpigia Bilal kampeni wakijua kazi ya kumweka Shein imekamilika. Baada ya hapo uliendelea kumng'ang'ania Zakhia kuwa makamu. Mkapa akishirikiana na Rostam (ambaye alikuwa akim-install Bilal kuwa makamu huku yeye akiwa South Africa kuangalia World Cup) walimweka Bilal hapo alipo.
Kumbe JK alimtaka Mama Mkwe Zakia?. Kumbe Shein aliibukia Zanzibar kummaliza Nahodha?, kumbe king maker anaweza kufanya kazi kwa remote?, kumbe JK alimng'ang'ania Zakia akashindwa na wenye nguvu zaidi yake?. Kumbe hao rafiki zake, walimchezea akili? hapa wajameni hata mimi niko gizani!.

Shein hakushinda uchaguzi Zanzibar. Kilichofanyika ni Mkapa, Rostam, Karume kumhonga pesa za kutosha sana Maalim kupitia kwa kijana wao hatari sana Jussa (kumbuka huyu aliletwa na Rosatm ili umteue awe mbunge). Today, umeshindwa kumweka mtu wako Zanzibar na makamu wa rais Muungano. Walichoweza kufanikisha ni kuiteka Zanzibar yote (Bilal na Shein). Nakukumbusha ya kwamba, ili uwe mgombea kupitia CCM, unahitaji Zanzibar na 'Lake Zone'. Kule 'Lake Zone' wamekushinda. Hilo unalifahamu vizuri. Hii ndiyo maana Wanzanzibar wamekutesa sana ndani ya CC iliyopita. Ili kukuonyesha kwamba hufai, Shein kampa udaktari wa heshima ''Baba yake'' mdogo Karume. Ninafahamu jinsi unavyojikosha kwa Anne kwa kumpa nishani ili kusiwe na vote of no confidence mwakani hasa kwa sakata la Richmond na Twiga. Napenda kumhakikishia Anne ya kwamba that's a strategy anayoitumia Mugabe ya kuwamaliza watu. JK ameiiga huko. Naomba Anne uwe makini sana. Waweza kufa kwa ''presha'' usipoangalia.
Kumbe CCM haikushinda Zanzibar?!. Kumbe Maalim Seif kahongwa kukubali matokeo?!. Kumbe ule ubunge wa Jussa kipindi cha lala salama ndiko ulikotokea?!,Kumbe ile nishani ya Anne ni kuzuia impeachment ?!- Hapa kuna kama vijiukweli ndani yake!

2. Karume ni nani?
Huyu alipigiwa kampeni kubwa sana na Edward na Rostam mwaka 2000 licha ya CCM Zanzibar kumkata jina lake. Kwa hili Karume hawezi kuwasahau hawa jamaa mpaka anakufa. Karume alikupinga Butiama. Yeye, Edward na Rostam wakaenda ku-design ''mwafaka'' wao wanaoujua ambao leo hii unafanya kazi Zanzibar. Nataka nikukumbushe mara ya pili kuwa Jussa aliletwa kwako na Rostam ili umpe ubunge. Think twice! Karume ndiye rais aliyeleta maendeleo makubwa Zanzibar. Shein will do more than what Karume did. Usishangae ukisikia Karume kuwa makamu wa Lowassa 2015!. Karume ana msimamo. Hayumbi na bahati mbaya sana hakuogopi.


NITAENDELA SIKU NYINGINE WAPENDWA WANA JF
Kumbe hata muafaka ulidesginiwa na RA na EL?!, then kama ni kweli, ni RA na El ndio waliomuweka JK madarakani, na wao ndio wakamleta Bilal, ninauhakika wa asilimia 100% chini ya 100% ndio waliomuweka Anne Makinda pale alipo!, na usikute ni wao waliomuweke Othman Chande pale alipo!, then wao ndio the most powerful persons in Tanzania!, usikute hata ni hao hao ndio waliyemuweka Rashid Othman pale alipo!, usikute ndie waliyemuweka Said Mwema pake alipo!, usikute ndio waliyemuweka Davis Mwamunyange pale alipo!, usikute ndo waliomuweka Hosea pale alipo!, and the list goes on...then if that is true, hii inamaanisha 100% sure 2015 ni Lowassa!. Hii inamaanisha JK na serikali yake yote si chochote, si lolote kwa watu hawa!

This is not a joke!.
 
Naona watu wanajenga falme zao ili maslahi yao yalindwe milele!
 
Back
Top Bottom