Kila dalili zinaonesha Bwawa la Nyerere kuhujumiwa na wapigaji ili kupata kile wangekosa chini ya Hayati Magufuli

Kila dalili zinaonesha Bwawa la Nyerere kuhujumiwa na wapigaji ili kupata kile wangekosa chini ya Hayati Magufuli

Kwani kufunguliwa kesi ndio kushindwa au kuzama? Sasa unataka nchi tuwe watiifu kwa dhuluma kwa kua tutashitakiwa tukichukua hatua kujinasua? Kushitakiwa ni jambo linaweza kutokea kufuatana na hao dhulumati wakiona uwezekano wa kushinda. Nchi ikiwa na wanasheria wa ovyo au wapenda rushwa utashindwa hata kama una haki.

..haya mambo hayaendeshwi kwa emotions, yanahitaji maamuzi yanayopima faida na hasara. Sasa katika hili Magufuli alidanganywa na Kabudi na Kilangi matokeo yake nchi imeingia hasara kubwa zaidi.
 
Usiongee kama Kasuku,be specific with evidence Kabudi alimdanganya Magufuli kwenye issue ipi.
Usisahau pia Katiba yetu inasema Rais halazimiki kufuata ushauri utakaotolewa na mtu yoyote,kama alimshauri hakusilizwa Je!

..kama Kabudi alishauri na hakusililizwa basi alipaswa kujiuzulu.

..kwa msingi huo Magufuli, Kabudi, na Kilangi, ndio waliosababisha Tanzania iburuzwe ICSD na kuhukumiwa kulipa mabilioni ya fedha.
 
Sijui hata kama unatuelewa. Januari alipue mabomba ya gesi kwa umeme ya kazi gani? Kwani yeye hataki huo uwaziri wa nishati? Mtu ni mpigaji atapigaje akibomoa?🤣. Simumesikia wakipanga ununuzi kufuru. Mita za papo kwa papo, kurepea mtandao wa usambazaji bilioni 11 etc etc tenda kibao... Huku umeme hakuna na bei na maharage wake wamesema hawashushi kukidhi wasia wa magufuli.🏃🏃
Huyo niliyem quote anasema Bwawa linahujumiwa na January ndio nikauliza why asihujumu gesi inayofua 70% ya umeme wa Tanzania aje kuhangaika na umeme wa Maji?

Yaani mtu aibe maharage wakati Kuna nyama? Nlichogundua wengi mnapinga hata hamjui mnapinga nini. TANESCO is incompetent kama ilivyo taasisi zote za umma Sasa why muingiza hujuma sijui mabeberu.

Mnashangaza sana
 
Huku umeme hakuna na bei na maharage wake wamesema hawashushi kukidhi wasia wa magufuli
JPM mwanasiasa tu Ile uwekezaji wa trillion 6 hauwezi ukashusha tu bei wakati operating costs ni kubwa na mikopo lazima ilipwe. Hata SGR nauli ni bei kubwa, bei hushuka baada ya mtaji kurudi hakuna shortcut hizo alizowadanganya JPM.

Mbona aliwadanganya kitambulisho cha machinga kinadhaminika kuchukua mkopo benki!! JPM was a fraud
 
Kwa nini iwezekane vitambulisho vya mpiga kura inawezekana kuchapwa na kupewa wote umri miaka 18 waliyojiandikisha kwa muda mfupi ila watu hao hao ishindikane kuwapa vitambulisho vya taifa miaka mingi tu imepita sasa. Ukweli kuna watu wananufaika na kutokua na vitambulisho watu
Ndio maana nikauliza nyie mbona hamsemi NIDA inahujumiwa na waziri wa mambo ya ndani au mabeberu? Incompetence Iko ofisi zote za serikali kuanzia TTCL mpaka Bandari hadi mnataka mkodishe sekta binafsi.

Nashindwa kupata logic yenu kabisa. Mnamshambulia mtu alafu makosa hayo hayo yapo wizara zote mpo kimya.
 
Hakuna alichomponza. Mikataba illiingiwa na Kikwete,mikataba ya hovyo sana. Ni bora kuikata kuliko kuendelea nayo.

Tungeendelea nayo tungelipa zaidi ya hizo pesa.

Wewe ungekuwa kiongozi wa serikali, mzalendo ungeendelea na hii mikataba, Nikupe mfano gesi kusini, bandari, misitu, mikataba 30 unajua vigezo vyake?

Ukiingia serikalini kwanini usivunje mikataba mibovu?
Kuna njia nyingi za kudhibiti mikataba mibovu kwa kutumia akili.
Wote wanaofanya shughuli zao nchini mwako unaweza kuwadhibiti kwa njia rahisi mpaka wafunge virago, changamoto ni siasa na mbaya zaidi wengi wa wanasiasa wana madaraka ambayo huwalevya na hivyo kujitangaza kwamba wana nguvu kuliko yeyote.
Serikali ikiamua kuwanyima ushirikiano awekezaji watashindwa kuendeleza mikataba. Ingefanya waone mazingira siyo rafiki.
 
Hivi kipi ambacho serikali ya CCM inakiweza? Kwanini Kila mkifeli lawama ni kwa mabeberu au "washauri wa Rais" yaani hakunaga failure yoyote mnakubali ni udhaifu wenu.

Mbona TTCL imekufa ni mabeberu? Mbona ATCL ni hasara Kila siku ni mabeberu? Mbona mwendokasi imefeli kuwa na ufanisi nao ni mabeberu? Why uzembe mfanye wenyewe alafu msingizie mabeberu?

Nachosema hapa kama wazungu au huyo January angetaka kuhujumu umeme basi mabomba ya gesi yangelipuliwa maana umeme wa Gesi ndio unazalisha 70% ya umeme wa Tanzania. Sasa why mtu ahujumu umeme wa Maji ilihali wa gesi ambao ndio tunategemea usiguswe?

Tuache propaganda na CCM mjifunze kuwajibika kwa failures zenu.
Atcl, Ttcl zilishamili kipindi Cha magufuli .
 
Back
Top Bottom