Kila la heri timu ya Taifa, Taifa Stars

Kila la heri timu ya Taifa, Taifa Stars

Watanzania wengi wana IQ ndogo sana ! Hivyo wana michezo ,wanasiasa hawana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na kwa haraka!
Tunachoweza na ambacho hatuna mshindani duniani ni unafiki na urongo tu!
 
Naniliu alisema tutapeleka jeshi kushindana, hivyo vuta subira.
 
Mechi yetu ya kwanza AFCON 2019 dhidi ya Senegal huko Misri ndiyo tu imemalizika muda mfupi uliopita kwa timu yetu ya Tanzania (Taifa Stars) kuchezea kichapo cha goli 2 bila majibu.

Mchezo ulikuwa wa upande mmoja zaidi bila shaka kwa kila aliyeutazama kupitia TV ama ana kwa ana kwa wale waliokwenda Misri

Laiti Senegal wangekuwa makini kidogo tu, ni wazi tungeweza kuchezea kichapo kikubwa zaidi cha magoli kwa idadi isiyopungua "ngumi ya mkono mmoja" ama "kidumu Chama Cha Mapinduzi"

Kwa maoni yangu naweza kusema bila shaka yoyote kuwa, tumekwenda Misri kushiriki na siyo kushindana na tusitegemee chochote cha maana kutoka kwa vijana wetu hawa.

Historia inaonesha kuwa kabla ya ushiriki wetu wa AFCON ya mwaka huu 2019, kwa mara ya mwisho tulishiriki mashindano kama haya mwaka 1980 ambapo tuliishia katika hatua ya makundi huku tukifungwa mechi zote kasoro mechi moja tuliyoambulia droo.

Kwa tathmini yangu, na kwa picha tuliyoiona ktk mechi hii ya kwanza tu, mwaka huu tutagongwa mechi zote hata mechi dhidi ya jirani zetu Kenya kuna uwezekano wa zaidi ya 75% kupigwa goli za kutosha sana tu

Kiukweli tulichokiona katika mchezo wa leo, ndiyo halisi jinsi tulivyo kama taifa. Kwamba, tuko weak kwa karibu kila nyanja si siasa, uchumi, elimu hata michezo.

Haieleweki hasa sababu ni nini tunashindwa kusonga mbele kwenye maeneo yote huku tukiwa ni taifa kubwa lenye idadi ya watu takribani 60,000,000 na eneo la nchi la takribani kilometa za mraba zaidi ya 900,000 likiwa na kila aina ya rasrimali (natural resources) ndani yake ndani yake ikiwemo human resources

Nchi ya Senegal tuliyocheza nayo leo tunaizidi mbali sana kwa rasrimali watu na ardhi kwani population yake ni takribani watu milioni 16.7 tu (karibu mara nne ya Tanzania) na eneo la takribani kilometa za mraba 190,000 (zaidi ya mara saba ya Tanzania) huku sehemu kubwa ikiwa jangwa!

Lakini wenzetu hawa wako mbali sana karibu ktk kila nyanja hususani ktk nyanja ya sanaa na michezo ambayo ndiyo mjadala wa leo..

Karibu wachezaji wao wote wanaoshiriki AFCON mwaka huu ni professionals wanaoshiriki ligi mbalimbali za kiwango cha juu huko duniani hususani barani Ulaya tofauti kabisa na sisi ambaye sana sana tunaye mmoja tu anayejulikana ingalau aitwaye Mbwana Samatta anayechezea moja ya club kule barani Ulaya nchini Ubelgiji.

Na ndo huyo pekee tunayemtegemea afanye maajabu huko Misri. Haiwezekani hata kidogo!

Nimejiuliza sana hivi tuliwezaje hata kufuzu kwa kiwango kile tunachocheza hata kwenda kwenye mashindano haya?

Nikagundua kuwa ni kwa kutumia njia zilezile za ujanja ujanja ule ule tunaotumia ktk maeneo mengine kama vile "kushinda chaguzi za kisiasa kwa kishindo" huku tukijua kabisa mtu ameshinda kwa wizi tu wa kura na siyo kwa sababu "SMART" Sera na mipango thabiti.

Angalia tu, kuwa, Taifa Stars ilifuzu si kwa sbb tuna "sustainable plans" thabiti bali ni kutokana na mipango ya zima moto ya muda mfupi chini ya kina Albert Bashite a.k.a Christian Makonda Malyangili RC wa DSM ya kwamba njooni mshangilie timu na ikishinda watu wote watakunywa pombe (bia) kilevi bure!!

Sasa matokeo yake ndiyo nayo. Tumekwenda Misri tukiwa tumelewa pombe kwenye nafsi na akili zetu

Kupitia mchezo wa leo imeonesha wazi kuwa vijana wetu hawana energy, creativity pamoja na exposure..

Mambo haya hayaji kwa ujanja ujanja kama wa kuiba kura ktk chaguzi za kisiasa kunakofanywa na CCM kila uchaguzi ili tu waendelee kuwa madarakani huku kukiwa hakuna sera na mipango thabiti ya kuendeleza sekta ya michezo

Namalizia kwa leo kwa kusema tena tulichokiona leo huko Misri, ndiyo picha halisi ya jinsi tulivyo kama Taifa na nchi chini ya serikali inayoongozwa na CCM kwa takribani miaka 58 sasa tangu Uhuru 1961!!
Sababu ni moja kati ya mbili. Ama kocha anaihujumu timu au hajui. Maelezo mengine hayana mashiko. Kuna uvurugaji wa timu makusudi katika kupanga kikosi katika michezo yote ya kufuzu, ya maandalizi ns ya mashindano. Asiyeweza kuona hilo haelewi mpira.
 
Kocha tuta msingizia bure.

Mpira hauna shortcut ni mwenye mipango thabiti na kuifanyia kazi ndio hufanya vizuri.

Inabidi tuanze kuboresha mfumo wa mpira wetu.
Sababu ni moja kati ya mbili. Ama kocha anaihujumu timu au hajui. Maelezo mengine hayana mashiko. Kuna uvurugaji wa timu makusudi katika kupanga kikosi katika michezo yote ya kufuzu, ya maandalizi ns ya mashindano. Asiyeweza kuona hilo haelewi mpira.
 
Sababu ni moja kati ya mbili. Ama kocha anaihujumu timu au hajui. Maelezo mengine hayana mashiko. Kuna uvurugaji wa timu makusudi katika kupanga kikosi katika michezo yote ya kufuzu, ya maandalizi ns ya mashindano. Asiyeweza kuona hilo haelewi mpira.
Mkuu,wala usisumbuke sana bali elewa hii region yetu ya East and Central Africa watu wake wanazidiwa mambo mengi tu na watu wa Afrika ya Kaskazini na Afrika Magharibi soka ikiwemo.

Na hata hawa waafrika wenzetu nao wakikutana na watu wa mabara mengine mfano Ulaya,kisoka mara nyingi wanaishia tu hatua za awali kama ilivyo kwenye kombe la dunia na katika michezo mingine.

Kimsingi kuna tatizo na tatizo hili lina uhusiano mkubwa sana na Nature na Regions anakopatikana binadamu.Binfsi huwa naamini regions zime-define au zime-influence kiasili mambo mengi kuhusu viumbe hai na binadamu tukiwemo.
 
Kenya keshapigwa moja huku tayari

Kuna kupigwa goli lakini ukiwa optimistic kuwa next time unaweza kuwa tofauti....

Naitazama. Kweli wamefungwa lakini wanaonesha competitiveness kuliko Tanzania yetu

Taifa Stars ya Makonda haina tofauti na timu ya taifa ya SOMALIA mkuu!!

Ni kweli kabisa na ni haki kujiuliza hivi tulifuzuje kushiriki mashindano haya hata kuipiku Rwanda ya Kagame ambayo kwa mtazamo wangu is far better than TZ?
 
Mechi yetu ya kwanza AFCON 2019 dhidi ya Senegal huko Misri ndiyo tu imemalizika muda mfupi uliopita kwa timu yetu ya Tanzania (Taifa Stars) kuchezea kichapo cha goli 2 bila majibu.

Wote tumeona mchezo huu kupitia TV kuwa kwa zaidi ya 90% ulikuwa wa upande mmoja zaidi na bila shaka walioko huko Misri na kuuona ana kwa ana ndani ya uwanja wako very disappointed na wanaweza kushuhudia wenyewe.

Na laiti Senegal wangekuwa makini kidogo tu, ni wazi tungeweza kuchezea kichapo kikubwa zaidi cha magoli kwa idadi isiyopungua "ngumi ya mkono mmoja" ama "kidumu Chama Cha Mapinduzi"

Kwa maoni yangu naweza kusema bila shaka yoyote kuwa, tumekwenda Misri kushiriki na siyo kushindana na hivyo basi tusitegemee chochote cha maana kutoka kwa vijana wetu hawa.

Historia inaonesha kuwa kabla ya ushiriki wetu wa AFCON ya mwaka huu 2019, tumewahi tena kushiriki mashindano kama haya mwaka 1980 ambapo tuliishia katika hatua ya makundi huku tukifungwa mechi zote kasoro mechi moja tuliyoambulia droo.

Na kwa picha tuliyoiona ktk mechi hii ya kwanza tu, hata mwaka huu tutagongwa mechi zote hata ile dhidi ya jirani zetu Kenya kuna uwezekano wa zaidi ya 75% kupigwa goli za kutosha kwa sana tu

Sijaona timu ambayo iko committed kwelikweli kuchuana na timu za Algeria ya watu wanaojua wanafanya nini....

Kiukweli tulichokiona katika mchezo wa leo, ndivyo sisi sote kama taifa jinsi tulivyo.

Kwamba, tu dhaifu mno karibu katika kila nyanja iwe ni katika siasa, uchumi, elimu ama michezo ambayo ndiyo mjadala wa leo

Haieleweki hasa sababu ni nini tunashindwa kusonga mbele kwenye maeneo karibu yote huku tukiwa ni taifa kubwa lenye idadi ya watu takribani 60,000,000 na eneo la nchi la takribani kilometa za mraba zaidi ya 900,000 likiwa na kila aina ya rasrimali (natural resources) ndani yake ndani yake ikiwemo human resources

Hopefully, tatizo ni ukosefu wa UONGOZI BORA na SIASA SAFI ambazo ndizo huzaa Sera na mipango safi na endelevu kwa watu na taifa zima kwa maana ARDHI na RASRIMALI WATU kama nilivyosema wapo wa kutosha tu

Nimejaribu kuitazama na kuilinganisha nchi ya Senegal tuliyocheza nayo leo na Tanzania yetu nikagundua kuwa tunaizidi kwa mbali sana kwa rasrimali watu na ardhi

Mathalani population ya Senegal ni takribani watu milioni 16.7 tu (karibu mara nne ya Tanzania) na eneo la nchi yake ni takribani kilometa za mraba 190,000 tu (zaidi ya mara saba ya Tanzania) huku sehemu kubwa ikiwa jangwa!

Lakini wenzetu hawa wako mbali sana karibu ktk kila nyanja hususani ktk nyanja karibu zote hususani katika sanaa na michezo ambayo ndiyo mjadala wa leo..

Karibu wachezaji wao wote wanaoshiriki AFCON mwaka huu ni professionals wanaoshiriki ligi mbalimbali za kiwango cha juu huko duniani hususani barani Ulaya tofauti kabisa na sisi ambaye sana sana tunaye mmoja tu anayejulikana ingalau...

Huyu si mwingine bali ni Mbwana Samatta anayechezea moja ya club ya kulipwa kule barani Ulaya nchini Ubelgiji.

Na ndo huyo pekee tunayemtegemea afanye maajabu huko Misri. Haiwezekani hata kidogo!

Nimejiuliza sana hivi tuliwezaje hata kufuzu kwa kiwango kile tunachocheza hata kwenda kwenye mashindano haya?

Nikagundua kuwa ni kwa kutumia njia zilezile za ujanja ujanja ule ule tunaotumia ktk maeneo mengine kama vile "kushinda chaguzi za kisiasa kwa kishindo" huku tukijua kabisa mtu ameshinda kwa wizi tu wa kura na siyo kwa sababu "SMART" Sera na mipango thabiti.

Angalia tu, kuwa, Taifa Stars ilifuzu si kwa sbb tuna "sustainable plans" bali ni kutokana na mipango ya zima moto ya muda mfupi chini ya kina Albert Bashite a.k.a Christian Makonda Malyangili RC wa DSM ya kwamba njooni mshangilie timu na ikishinda watu wote mtakunywa pombe (bia) kilevi bure!!

Sasa matokeo yake ndiyo nayo. Tumekwenda Misri tukiwa tumelewa pombe kwenye nafsi na akili zetu!!

Kupitia mchezo wa leo imeonesha wazi kuwa vijana wetu hawana energy, creativity pamoja na exposure..

Jamani mambo haya tukubali tu kuwa hayaji kwa ujanja ujanja kama wa kuiba kura ktk chaguzi za kisiasa kunakofanywa na CCM kila uchaguzi ili tu waendelee kuwa madarakani huku kukiwa hakuna sera na mipango thabiti ya kuendeleza sekta ya michezo

Namalizia kwa leo kwa kusema tena ,kuwa, tulichokiona leo huko Misri, ndiyo picha halisi ya jinsi tulivyo kama Taifa na nchi chini ya serikali inayoongozwa na CCM kwa takribani miaka 58 sasa tangu Uhuru 1961!!
kama himidi mao ataendelea kucheza hakuna tunachokifanya
 
Mkuu,wala usisumbuke sana bali elewa hii region yetu ya East and Central Africa watu wake wanazidiwa na mambo mengi tu na watu wa Afrika ya Kaskazini na Afrika Magharibi soka ikiwemo.
Na hata hawa waafrika wenzetu nao wakikutana na watu wa mabara mengine mfano Ulaya,kisoka mara nyingi wanaishia tu hatua za awali kama ilivyo kwenye kombe la dunia na katika michezo mingine.
Kimsingi kuna tatizo na tatizo hili lina uhusiano mkubwa sana na Nature.
Mkuu,wala usisumbuke sana bali elewa hii region yetu ya East and Central Africa watu wake wanazidiwa mambo mengi tu na watu wa Afrika ya Kaskazini na Afrika Magharibi soka ikiwemo.

Na hata hawa waafrika wenzetu nao wakikutana na watu wa mabara mengine mfano Ulaya,kisoka mara nyingi wanaishia tu hatua za awali kama ilivyo kwenye kombe la dunia na katika michezo mingine.

Kimsingi kuna tatizo na tatizo hili lina uhusiano mkubwa sana na Nature na Regions anakopatikana binadamu.Binfsi huwa naamini regions zime-define au zime-influence mambo mengi na kiasili kuhusu viumbe hai na binadamu tukiwemo.
Maelezo yako ni sahihi. Lakini kwa muktadha wa upangaji wa timu kwenye mechi tulizocheza za kirafiki na za makundi kuna kila ishara ya makusudio ya kushindwa. Wala sioni sababu ya kumtetea kocha. Sitashangaa nikisikia kuna mfarakano kati ya wachezaji na kocha. Kuna shida kubwa sana kwenye timu yetu.
 
Back
Top Bottom