Kila limsemo likitoa we unalo. Sasa unamwambia nani habari za Maokoto?

Wakili wa shetani

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2022
Posts
1,726
Reaction score
3,391
We ni mtu mzima, huu ujinga wa kudandiadandia mambo unatoa wapi? Kila msemo unauvalia njuga. Kipindi wanasema wahenga ulikomaa kishenzi na huo msemo. Nakumbuka ukaja kukomaa na "Injinia soma hiyooooo" hadi ukawa kero kuu. Mara ukaja na Chap kwa haraka, ukaenda na mzee baba. Kuna mingine umepita nayo hapa kati. Siku hizi umekuja na Maokoto. Halipiti saa hujasema Maokoto. Punguza huu ujinga na anza kujiheshimu.
 
Umekunywa chai Kamanda?
 
Mwenye tatizo ni wewe. Unaanzaje kujisikia vibaya Kwa sababu MTU ametamka Jambo Fulani tena hata sio tusi???



Sijasoma Kiswahili saana Ila nadhani hayo maneno yanayokuja na kuondoka yanaitwa misimu. Ni Jambo la kawaida.

Wajuvi WA kiswahili watarekebisha.
 
Uwa wananikera sana ndiyo ukae na tuvijana ambao hawana hata kumi mfukoni basi kusema maneno hayo kwao ni kama fahari mara maokoto , mara nini ushamba mwingi tu.

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Ni kero kubwa sana. Tatizo ni kutokuwa na chochote cha maana kichwani. Likitokea limsemo linajaza kichwa kizima. Mtu akilala akiamka anakuwa anasikia limsemo "Injinia soma hiyooooo" au "Nawaona nawaona" likipiga kichwani.
 
CAF wenyewe wameandika "hii imeendaa" baada ya Tanzania kufuzu AFCON. Twitter
 
Ukweli mtupu, Wanakera Wapumvavu hawa na Misemo ya Kichoko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…