Kila unalotakiwa kujua kuhusu IPTV (kuangalia TV kwa kutumia internet)

Kila unalotakiwa kujua kuhusu IPTV (kuangalia TV kwa kutumia internet)

Nonsense,,,, maelezo kibao NA tutorial za kufa mtu,,, at the end nothing.Dunia ya sasa iko simple sana na clear ndo maana hata job interviews zimepungua masaa,,,;sasa umeapload movie ya 2hrs kwenye somo? Sasa mtihani si itakuwa TB au XB?

Najaribu kuelewa ulichoandika lakini bado naona sielewi na nimeisoma post yako zaidi ya mara 6....punguza stress na viroba
 
Unamaanisha LazyIPTV au Kodi?

Kama ni Kodi je umeinstall version ipi?

Kodi v 4.2 nikifungua vdubt25 channel zake inasema one or more item failed to play chek the log file
 
Kodi v 4.2

Tatizo lako la pale juu umelitatua?

nikifungua vdubt25 channel zake inasema one or more item failed to play chek the log file

Maana yake link unayoifungua ipo dead (ni mfu) hivyo haiwezi funguka...

Inabidi usubiri hadi developer wa vdubt25 atapofanya update...

Pia huenda huna connection ya internet au upo geo-restricted
 
Stage zote za Ku install Vdubt25 nimekamilisha nasikia sauti tu kwa baadhi ya Chanel kama za cartoon channel zingine inakuja msg Chen the log file nimekosea wapi? au nifungue channel ipi?iliyo wazi
 
Tumezoea katika maisha yetu tukiangalia Tv basi huduma ile tunaipata kupitia madishi, cable au antenna. siku zinavyosogea mbele na technology ndivyo inavyokuwa na ndio jinsi madish na antenna vinavyopitwa wakati. leo kwenye uzi huu tutaangalia IPTV.

Ni nini hii IPTV?
IPTV ni kifupi cha Internet Protocal TeleVision. Hii ni aina ya uangaliaji TV kupitia mtandao wa internet ambapo kituo cha TV badala ya kutumia satelite dish au cable wenyewe wanarusha matangazo kwa internet.

Unawezaje kuangalia IPTV?
Utahitaji kifaa chenye internet na uwezo wa kustream ili kuweza kuangalia kama vile smartphone, tablet, laptop, desktop hadi TV zenye internet zinaweza kustream.

Internet yenye speed gani inahitajika?
Internet yoyote hata ya edge inaweza kustream ila iwe na latency nzuri, zipo stream zinahitaji speed ya 200kbps tu (25KBps). Kama una latency ndogo hata internet iwe na speed vipi huwezi kustream live utastream tu vitu ambavyo si live. Kujua zaidi kuhusu latency nenda thread hii
https://www.jamiiforums.com/tech-ga...iwa-na-download-speed-kubwa-ndio-mzuri-2.html

Je software gani inatumika kustream hizo TV?
Kikawaida browser yenye flash au html5 inaweza kustream tv lakini ukitaka kustream vizuri zaidi software kama VLC au KODI ni muhimu. Kutokana na uhaba wa links za VLC nitazungumzia zaidi jinsi ya kutumuia KODI kuangalizia IPTV.

KODI ni nini?
KODI ni software (media centre) ambayo hutumika kuubadili muonekano wako wa simu uwe kama TV na kuweza kuenjoy TV unazotumia na inapatikana kwenye simu, tablet, computer hadi TV.
Kodi-devices-smudged.jpg


Kuidownload nenda website yao hii hapa chini, ni bure haiuzwi
Downloads | Kodi

Nikishadownload kodi nini kinafuatia?
Utahitaji ku install plugin ili uweze kuangalia TV online. Click video add on halafu chagua watchmojo, install halafu ifungue tuone kama itafanya kazi.
9vW4MHp.jpg


KODI imefanya kazi, je siwezi angalia mpira na vipindi vyengine?
Unaweza angalia mpira chanel unayotaka kuanzia za ki-Africa kama Super sport, za Ulaya kama Sky sport, za Asia kama Bein sport hadi za kimarekani kama NBC cha muhimu uwe na plugin (add ons) husika, hizi plugin za mpira na michezo mengine zinapatikana tu internet mfano mimi plugin yangu ninayotumia inaitwa Vdtube25 ina channel nyingi sana kuanzia mpira hadi movie.
zNbDtYR.jpg

PppArCw.jpg


Hio hapo juu sky sport 3

Uzuri wa hizi plugin za kodi zipo TV ni HD na nyengine ni full HD kabisa hivyo internet yako tu.

Malipo?
Kila kitu kuanzia juu hadi hapa ulipofikia ni bure hutoi pesa, ila hizi plugin za bure haziaminiki zipo za kulipia ambazo hazikati ovyo. Mimi sijawahi kulipa natumia tu bure ila kama unahitaji service nzuri zaidi unaweza kulipa ila pia kuwa makini na matapeli

Tutorial ya kuweka na mahala pa kupatia plugins
Plugin yangu ninayotumia ya vdtube25
https://seo-michael.co.uk/how-to-install-vdubt25-add-on-kodi-xbmc

Website hio hio pia utapata plugins nyingi.

Kama una swali lolote usisite kuuliza chini

Nawezaje kuistall KODI kwenye TV ?
 
Nawezaje kuistall KODI kwenye TV ?

Kama tv ina android ndio utaweza kama haina inabidi ununue box la android au nunua computer yenye hdmi au nunua computer ya kizamani halafu eka graphics card yenye hdmi then tumia hio kuangalizia kodi kwenye tv
 
Nonsense,,,, maelezo kibao NA tutorial za kufa mtu,,, at the end nothing.Dunia ya sasa iko simple sana na clear ndo maana hata job interviews zimepungua masaa,,,;sasa umeapload movie ya 2hrs kwenye somo? Sasa mtihani si itakuwa TB au XB?

Umekula maharage ya wapi wewe?
 
Nilikua Offline kwa siku kadhaa nimekuta new ideas hapa

TV Directo

SportsDevil

Nimeinstall sportsDevil ila sijaona faida yake maana Content zake naona ni sawa na zile za Phoenix,vdtube25 etc

Hiyo TV directo nime google sijaelewa
 
naulizia swala la bundle kwasababu hamjaongelea kabisa! mfano nikiwa na 1GB naweza kustrem kwa mda gani kama nacheki football?@chief
 
naulizia swala la bundle kwasababu hamjaongelea kabisa! mfano nikiwa na 1GB naweza kustrem kwa mda gani kama nacheki football?@chief

Inategemea na quality na stream pia. Ni vizuri ukafanya research mwenyewe kaka.

Tv nyingi zina quality za aina tatu
SD au 480p
HD au 720p
Full HD au 1080p

Kama wewe unabania mb zikimbie hizo chanell za hd na pendelea za sd.

Utajuaje ipi ni hd au sd? Ukishaplay tv ukistop kodi inatambua quality ya ile stream hivyo kwa mbele inakuandikia kama ni hd au sd

Kwa mahesabu ya haraka haraka mpira na mapumziko na dakika za nyongeza ni kama masaa 2 (dk 120)

Dakika 120 ni sekunde 7200
Internet yako ni mb 1000

Roughly kila sekunde unaweza tumia kilobyte 140 ambayo ni zaidi ya 1mbps.

Kama umesoma post ya juu njunwa anasema amestream hd kwa net ya 1mbps tu, mimi pia nimewahi fanya hivyo.

Hivyo jibu ni ndio kaka gb1 unaweza stream mpira wote hadi unaisha make sure huchagui tu full hd
 
Nilikua Offline kwa siku kadhaa nimekuta new ideas hapa

TV Directo

SportsDevil

Nimeinstall sportsDevil ila sijaona faida yake maana Content zake naona ni sawa na zile za Phoenix,vdtube25 etc

Hiyo TV directo nime google sijaelewa
Sportsdevil tv zake ni zile zinazopatikana site maarufu za mpira kama firstrow, livetv.ru na rojadirecta. Zenyewe zina quality ndogo sana kwa wale wenye internet isio na speed. Mfano rojadirecta ana chanell ambazo ni chini ya 200kbps. Ukiwa na network ya edge unaweza stream
 
Inategemea na quality na stream pia. Ni vizuri ukafanya research mwenyewe kaka.

Tv nyingi zina quality za aina tatu
SD au 480p
HD au 720p
Full HD au 1080p

Kama wewe unabania mb zikimbie hizo chanell za hd na pendelea za sd.

Utajuaje ipi ni hd au sd? Ukishaplay tv ukistop kodi inatambua quality ya ile stream hivyo kwa mbele inakuandikia kama ni hd au sd

Kwa mahesabu ya haraka haraka mpira na mapumziko na dakika za nyongeza ni kama masaa 2 (dk 120)

Dakika 120 ni sekunde 7200
Internet yako ni mb 1000

Roughly kila sekunde unaweza tumia kilobyte 140 ambayo ni zaidi ya 1mbps.

Kama umesoma post ya juu njunwa anasema amestream hd kwa net ya 1mbps tu, mimi pia nimewahi fanya hivyo.

Hivyo jibu ni ndio kaka gb1 unaweza stream mpira wote hadi unaisha make sure huchagui tu full hd

Basi hapo unabidi utafute unlimited internet kuangalia mda wote coz bundle ya 1GB wanatuzia mpka buku mbili kwny hii mitandao yetu ya bongo,lakin naona revolution kwny internet nw days kuna hawa simba net naona wanasambaza wire mitaani sijajua maybe watatoa mambo ya bundle
 
Tatizo lako la pale juu umelitatua?



Maana yake link unayoifungua ipo dead (ni mfu) hivyo haiwezi funguka...

Inabidi usubiri hadi developer wa vdubt25 atapofanya update...

Pia huenda huna connection ya internet au upo geo-restricted

Yap la mwanzo nilifanikiwa...... Lkn hilo la kuto play bado lipo kwa channels nying.
Hii vidubt ndo linasumbua lkn nyingne zipo poa
 
Yap la mwanzo nilifanikiwa...... Lkn hilo la kuto play bado lipo kwa channels nying.
Hii vidubt ndo linasumbua lkn nyingne zipo poa

So far una addons ngapi za kutazama mpira/michezo?

Zile links (channels) katika Vdubt25 si zote zinazoonekana maana wakati mwingine zile links zinakuwa zimekufa...

Siku ya soka mathalani baadaye wakati Man U akicheza na Spurs utaona kuna links zitaongezwa (updated) sehemu ya Live Sports...
 
Back
Top Bottom