Kile unachoandika mtandaoni kinasadifu jinsi ulivyo

Kile unachoandika mtandaoni kinasadifu jinsi ulivyo

Mbona tunazijua IDs kibao na hatufatilii maandishi yao? Kwamba kama unanifaham in person utakuwa kila ninachoandika unafatilia na nikiandika upupu unaanza kunidharau?

Hatuishi hivyo, acha jamaa aishi anonymously, ndio maana hajaweka majina yake halisi.
Ndio yeye anaishi maisha yake anonymous ila anayetaka trend na kiki ni tofauti kabisa.
 
Jana usiku wakati nimekaa na mdogo wangu wa kiume mkubwa anayenifwata kuzaliwa akaniambia "Dada kumbe baba fulani (akamtaja baba mtoto wangu) ndio hana akili hivyo? Yaani jinsi nilivyokuwa namheshimu kumbe ndio ujinga anaouandikaga mtandaoni?

Kwanza shem alivyo busy vile muda wa kuandika ujinga ule anapata wapi, huoni kama anakuaibisha hata wewe? Yaani kusema kweli baada ya kusoma threads zake leo nimemdharau sana. Kweli unaweza kuwa umesoma, una kazi nzuri na pesa ila kichwa hakina akili."

Nikamuuliza umeijuaje ID yake mbona zaidi yangu hakuna anayeijua au ulipekua simu yangu kusoma PM zangu eeh? Akajibu hapana, sehemu nyingi sana anatagiwa hata kuna uzi wake pia alijisema yeye ndio baba wa anko wangu. Kweli Shemeji anajiaibisha sana hata kama tunatumia fake IDs (Mimi na dogo tunazijua ID's zetu).

Baada ya hapo ikabidi nianze kumuelekeza kwamba huyo chizi anayejiaibisha sio baba wa anko wake kabisa, nikamuelekeza kwamba shemeji yake hana ujinga huo. Hata kama simpendi namchukia ila ukweli hawezi kuonyesha ujinga wake hadharani hivyo.

Hata kama ni malaya pia hawezi kujisifia hadharani kubadilisha wanawake kila siku. Yeye yupo busy kwenye majukwaa ya Jamii intelligence na nyuzi za sports. Hata kwa Rick boy kwenye kula kimasihara anaonyeshaga ushamba wake hadharani wa kuwashangaa wenzie wanavyokula mitaro nje nje.

Jamani wanajukwaa mitandao ya kijamii inadefine sana jinsi ulivyo. Kile unachokiandika humu kinadefine uhalisia wako kwa hiyo tujitahidi sana kuandika vitu vyenye tija na vya maana. Unaweza kuwa mtu unayeheshimika kweli ila mitandao ikakufanya ujishushie heshima yako.

Kuna watu wengine huwa najiuliza hivi bahati mbaya hata mdogo wake au mwanae akashika simu yake akijua upuuzi anaoandika humu ataendelea kumuheshimu kweli? Tuangalie maudhui tunayoyaandika jamani.
We ni mwanamke au mwanaume? Mbona kama ni member wa Upinde anayejifanya mwanamke?
 
Kwanini ukimaliza unaclear mpaka history?? Jibu litakuwa kama kichwa cha habari hapo ila watajizima data kubisha na kunitukana.
Hapana
Huu mtandao sio FB wala IG kwamba uwe publicity to my/ our people.

Kama wewe na mdogo wako mmeigeuza JF kama IG mnatajiana usernames basi ni nyie. Ila sie hatuwezi, thats why tuna clear history.
 
Mbona kama Kuna mahali umetafuna tafuna hujaeleweka. Ulivyomuuliza huyo mdogo wako mbea kajuaje kama hiyo id ni ya huyo shemeji yake mbona kajiuma uma tu mara anatagiwa mara sijui nn
Kuna uzi niliwahi kuleta humu kuomba ushauri kuhusu baba mtoto wangu baada ya siku chache kuna memba akaja kujibu ule uzi kwamba ndio baba wa mtoto. So kila uzi huwa anatagiwa na memba nikicoment ndio dogo akahisi ndie Ex shemeji yake kumbe sie.
 
Jana usiku wakati nimekaa na mdogo wangu wa kiume mkubwa anayenifwata kuzaliwa akaniambia "Dada kumbe baba fulani (akamtaja baba mtoto wangu) ndio hana akili hivyo? Yaani jinsi nilivyokuwa namheshimu kumbe ndio ujinga anaouandikaga mtandaoni?

Kwanza shem alivyo busy vile muda wa kuandika ujinga ule anapata wapi, huoni kama anakuaibisha hata wewe? Yaani kusema kweli baada ya kusoma threads zake leo nimemdharau sana. Kweli unaweza kuwa umesoma, una kazi nzuri na pesa ila kichwa hakina akili."

Nikamuuliza umeijuaje ID yake mbona zaidi yangu hakuna anayeijua au ulipekua simu yangu kusoma PM zangu eeh? Akajibu hapana, sehemu nyingi sana anatagiwa hata kuna uzi wake pia alijisema yeye ndio baba wa anko wangu. Kweli Shemeji anajiaibisha sana hata kama tunatumia fake IDs (Mimi na dogo tunazijua ID's zetu).

Baada ya hapo ikabidi nianze kumuelekeza kwamba huyo chizi anayejiaibisha sio baba wa anko wake kabisa, nikamuelekeza kwamba shemeji yake hana ujinga huo. Hata kama simpendi namchukia ila ukweli hawezi kuonyesha ujinga wake hadharani hivyo.

Hata kama ni malaya pia hawezi kujisifia hadharani kubadilisha wanawake kila siku. Yeye yupo busy kwenye majukwaa ya Jamii intelligence na nyuzi za sports. Hata kwa Rick boy kwenye kula kimasihara anaonyeshaga ushamba wake hadharani wa kuwashangaa wenzie wanavyokula mitaro nje nje.

Jamani wanajukwaa mitandao ya kijamii inadefine sana jinsi ulivyo. Kile unachokiandika humu kinadefine uhalisia wako kwa hiyo tujitahidi sana kuandika vitu vyenye tija na vya maana. Unaweza kuwa mtu unayeheshimika kweli ila mitandao ikakufanya ujishushie heshima yako.

Kuna watu wengine huwa najiuliza hivi bahati mbaya hata mdogo wake au mwanae akashika simu yake akijua upuuzi anaoandika humu ataendelea kumuheshimu kweli? Tuangalie maudhui tunayoyaandika jamani.

Hata wewe tunakuona mpuuzi



Hata Kama unatumia ID fake ila avatar yako inaonesha wewe Ni tararira
 
Mahitaji yapo ya aina 3.,Kuna vitu vya lazima,vya muhimu na vya ziada
mitandao ni vya ziada kwaiyo ni kama starehe na burudani tu kuna wakati tupo hapa kuufariji na kupoteza mawazo lakini sio ukweli kila usomacho.

Note.Uhalisia wa mtu unapatikana kwenye pesa na mali.
 
Mtaji wake ni kumfatilia ex bwashe then anakuletea sister muanze kumjadili?

Let him enjoy his anonymity mkuu, humu tunaandikaga upuuzi wakati mwingine ili kupunguza stress na kujiburudishs
Ukirudi kusoma uzi vizuri utagundua huyo anayeandika upuuzi sio Ex shemeji yake na nilimuelekeza tatizo umesoma kwa kukimbilia kucoment, anyway my Ex is very anonymous even to my young bro zaidi yangu hakuna anayejua ID yake na huwa hacoment upuuzi.
 
Back
Top Bottom