Tetesi: Kilichomponza Diamond ni Sakata la ATCL

Tetesi: Kilichomponza Diamond ni Sakata la ATCL

_20181218_223109.JPG
 
Kwenye Show za Mtwara,Iringa,Morogoro,Sumbawanga Wimbo wa Nyegezi haukuimbwa? Kama uliimbwa imekuaje wamechelewa kuwafungia.Halafu Mie nlidhani umefunguliwa,maana Mtaani Nyegezi unapigwa kama kawa
 
Ngoja nae aonje keki ya taifa ya maumivu, maana awamu ni full kugawa maumivu kwa wananchi wake, nakumbuka ule wimbo wake wa "nakaa kimya" aliboa sana
 
Hujawahiona mwizi kaiba, kaonekana na Watu wakamtolea ushahidi, akapigwa akiadhibiwa ili akubali kosa asamehewe lakini akakataa katu katu akikanusha hadi akafa kwa kipigo cha kutosha?

Epuka kuongozwa na akili za mahaba sababu sheria no msumeno na Diamond ni Binadamu so huweza kukosea sawa na Binadamu wengine na anastahili adhabu kwa mujibu wa sheria za nchi.
Mbona amekuambia, kwamba katika watu aliofika nao wakati mmoja airport kuna waliochukuliwa, pale walipoambiwa tuna nafasi za watu wawili tu kwenye kundi lenu?

Kukiwa na overbooking mnaweza mkawa watano mmefika wakati mmoja akaondoka mmoja tu kati yenu
 
Sio kumfungia Ila according to mleta mada anadai chanzo kilichosababisha diamond kufungiwa ni issue yake ya usafiri wa ndege, so basata wakatumia huo uchochoro kumnyoosha
Kwani ile nyimbo ya nyegezi haiwezi kuwa kigezo ashikishwe adabu?

Inaleta picha gani hasa hususani kwa mila na desturi zetu Tanzania ikiwa nyimbo imejaa matusi tupu?

Nguvu za kifreemason zitawaendesha sana msipokuwa karibu na Mungu akawajaza hekima katika kuelewa dunia inaelekea wapi kwa ushetani uliojificha kupitia hizi nyimbo za kisasa.
 
Na bado atawanyosha sana ninyi vimeo, inadhani Kikwete aliposema anawaletea "CHUMA" sababu yeye ni mpole sana na hana maamuzi alikuwa akiwatania???
Ubabeshow inaendelea mbele, mwisho wake ni uchungu mzito kwa watawala.

ATCL haitafika popote zaidi ya kufa tena maana wanalazimisha tuamini uongo wao badala ya kujirekebisha kwa kosa walilomfanyia Diamond,

tatizo kubwa na chanzo cha maamuzi ya kibabe ni JIWE.
 
Kufanikiwa siyo kuwa vizuri kiuchumi, je mahusiano yako na jamii inayokuzunguka katika maisha uishiyo inaakisi au inazaa matunda mema kwa kumpendeza Mungu?

Kila mwenye pesa anaishi maisha ya furaha(ametawaliwa na amani nzuri rohoni mwake)?
Duuu kumbe diyamondi bado hajafanikiwa
 
Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limetangaza kumfungia msanii Diamond Platnumz na mwenzake Rayvanny kufanya maonesho yoyote ndani au nje ya nchi kwa muda usiofahamika. Si hivyo tu, bali pia wamelifutilia mbali Tamasha la Wasafi Festival ambalo limekuwa gumzo kubwa katika siku za hivi karibuni.

Sababu zinazotolewa na Basata, ambazo zina ushahidi wa wazi, ni kwamba msanii huyo amekiuka maelekezo aliyopewa na Basata, ya kuacha kuperform wimbo wa Nyegezi (Mwanza) uliofungiwa na Basata kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kukiuka maadili ya Kitanzania.

Tukio la Diamond kupigwa pini na Basata, limekuja muda mfupi baada ya Mbongo Fleva huyo kusababisha hali ya sintofahamu katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza baada ya video kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikimuonesha 'bwa mdogo' huyo akiwatemea mbovu wafanyakazi wa uwanja huo, kwa kile alichodai kwamba wamemchezea rafu kwa kuuza tiketi alizozifanyia booking mapema na kusababisha ashindwe kusafiri kurejea Dar baada ya kumalizika kwa shoo yake jijini Mwanza.

Madai hayo yalililazimu shirika la ndege la ATCL kutoa tamko rasmi na kukanusha madai ya Diamond ambapo taarifa ilieleza kwamba hakuna aliyeuza tiketi yake isipokuwa yeye ndiye aliyefanya makosa kwa kuchelewa kufika uwanja wa ndege hivyo kwa mujibu wa kanuni na taratibu, alipoteza sifa za kusafiri na ndege hiyo hivyo kuomba kupangiwa siku iliyofuatia.

Kabla ya ATCL kutoa ufafanuzi huo, watu wengi waliotazama video hiyo, waliamini kwamba kweli ATCL wamefanya uzembe, wamepiga dili kwa kuuza tiketi ya Diamond na kundi lake kwa watu wengine, kwa lugha nyepesi Diamond aliwaaminisha watu kwamba ATCL si waaminifu kwa wateja wake na ndiyo maana wameuza tiketi ambazo zilishafanyiwa booking kwa watu wengine.

Ikumbukwe kwamba ATCL ni shirika la serikali na serikali ya awamu ya tano imewekeza nguvu kubwa kulihuisha shirika hilo lililokuwa mahututi kwa kununua ndege mpya na kulifanya sasa angalau liwe na uhai baada ya kudoda kwa muda miaka mingi. Tayari ndege tano zimeshafika nchini na zinafanya kazi na matarajio ni kuleta mashine kubwa zaidi, Airbus mapema mwezi huu.

Wakati serikali ikihangaika kuhakikisha ATCL inapata wateja wa uhakika na kujiendesha kwa faida, anatokea 'mwehu' mmoja na kuibua tuhuma ambazo zinawafanya wateja wapoteze imani na shirika hilo na hivyo kulikosesha wateja na mapato.

Diamond ambaye kwa heshima na taadhima, alialikwa wakati moja kati ya ndege hizo ikiwasili nchini, badala ya kuwa balozi wa kuwahimiza watu wengine watumie huduma za ATCL, yeye anahujumu kwa kuibua tuhuma za uongo zenye lengo la kuikosesha ATCL wateja na mapato.

Fyekelea mbali ili siku nyingine ajifunze kuwa na adabu na uzalendo! Siku zote serikali inaweza kuwa inajua kwamba unafanya makosa lakini kwa sababu hugusi maslahi yake, ikakuacha uendelee kukosea! Ndiyo, kwani Diamond ameanza kuidharau Basata leo kwa kuimba Nyegezi? Upo ushahidi wa mpaka video akiwa Zanzibar na kwingineko, alionekana akiwaimbisha mashabiki kijanja.

Kama ishu ingekuwa ni hiyo tu, Basata wangeweza kuweka pamba masikioni au kuitana kishkaji, Mngereza alikuwepo kwenye uzinduzi kule Mtwara, kwa hiyo kwao siyo adui tena bali mlezi, wangeweza kunena kwa lugha moja wakayamaliza ili kuepusha hasara ya mamilioni ambayo sasa ataipata kwa kufungiwa.

Diamond, man up! Don't mess with the government!


Safi sana, wakajifunze muziki wa ukweli sasa. No more karaoke.
 
Ama kweli we ni Great Thinker
Nilivyoona ile video, halafu ATCL wakakanusha madai yake nilijua kuna kitu kitafata, Diamond ambacho hajui ni kwamba kazi yake anaifanya kwenye nchi ambayo anahitaji cover kubwa sana na kuinyenyekea serikali.

Sasa kufanya kile alichofanya na wao wakiamua wammalize ni rahisi, watakuja na issue za vibali, ulinzi, kodi, nk.

Anatakiwa kuujua msemo wa "ukila na kipofu usimshike mkono".
 
Safi saaaana...mawatu yanachangia tu mada kwa mihemko yao ya kishabiki hata kama Diamond kakosea basi asiadhibiwe kama vile Malaika?

Hala!
Tatizo kubwa ni kwamba wengi mnaochangia hapa kama wewe mnachangia kama wasafiri wa labda mabasi au wasafiri wa humu humu nchini.
Jiulize; Hivi wajua kuwa safari za ndege huhusiana kote ulimwenguni?? Kwa vipi? Kama nina safari kutoka Mza kwenda Jberg, naweza fanya booking yangu nikasafiri bila kulala Dar na nikaenda kulala home Jberg siku hiyo hiyo??
Sasa ndio maana unaambiwa, Fika even 2 hrs before departure time. Hii inakusaidia na pia inawasaidia wasafirishaji wanaokusafirisha kurekebisha mambo kama kweli walizidiwa na abiria.
Kivipi; Wakiona kuna msongamano au wamezidiwa wanafanya mpango kukodi ndege nyingine iliyopo jirani ili kukuwahisha dar chini ya nusu saa 7a muda uliokuwa umepangiwa kuingia. Unafika unaendelea na safari yako in time.
Mnaposema Mondi kaonewa, hakufanyiwa haki, Je, kuchelewa kwake ati nusu saa kabla ya departure time ndio kuiharibie sifa ATCL kwa sababu ya "Ujuha wake?"
Next time, akodi bus au ndege yake binafsi
 
Back
Top Bottom