Kilichomuua Ally Sonso hiki hapa, wachezaji, klabu zamlilia

Kilichomuua Ally Sonso hiki hapa, wachezaji, klabu zamlilia

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amezungumzia kifo cha mchezaji wao, beki Ally Mtoni 'Sonso' aliyefariki jana akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.

Imeelezwa kuwa kabla ya kukutwa na umauti huo, Sonso nyota wa zamani wa Lipuli,Yanga, Kagera Sugar na Ruvu Shooting alikuwa akiuguza majeraha ya mguu tangu Oktoba, mwaka jana.

Bwire amesema Sonso beki huyo alipata majeraha mara baada ya mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Simba, uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

"Mke wake ndiye alianza kunipigia akitoa kilio, baadaye Baba yake aliniambia hivyo na muda huu naelekea nyumbani kwao kwa taratibu za mazishi hapo kesho Jumamosi sambamba na timu nzima kwa ujumla, hakika tutamkumbuka," amesema Bwire.

Tangu kutangazwa taarifa za msiba huo kumekuwa na idadi kubwa ya wachezaji na klabu mbalimbali zimetumia mitandao yao ya kijamii kuelezea kusikitishwa na msiba huo.



Source: Mwananchi

sonso-pic.jpg
 
Jamaa anadai kabla ya game ya ruvu vs Simba huko ccm kilumba alihisi maumivu wa mguu akaongea na daktari wao akampa dawa ya kutuliza maumivu ..

Kesho yake pia akaona maumivu yanazidi basi kwenye hiyo game hakupangwa.. lakini akaanza kuona mguu unavimba kama tende akaongea na daktari wao wakampeleka muhimbili kwa matibabu zaidi

Basi baada ya matibabu hapo muhimbili akaomba akatabiwe kwao.. maana taarifa alizo zipata ni kwamba katupiwa jini

Basi mguu ukaendelea kuoza na kuharibika kabisa.. huko kwa mtalaam

R I p sonso
 
Inna lillahi wainna illayhi rrajiuun!

RiP Ally Mtoni mchezaji wetu wa zamani wa Yanga SC ,amen 🙏
 
Jamaa anadai kabla ya game ya ruvu vs Simba huko ccm kilumba alihisi maumivu wa mguu akaongea na daktari wao akampa dawa ya kutuliza maumivu ..

Kesho yake pia akaona maumivu yanazidi basi kwenye hiyo game hakupangwa.. lakini akaanza kuona mguu unavimba kama tende akaongea na daktari wao wakampeleka muhimbili kwa matibabu zaidi

Basi baada ya matibabu hapo muhimbili akaomba akatabiwe kwao.. maana taarifa alizo zipata ni kwamba katupiwa jini

Basi mguu ukaendelea kuoza na kuharibika kabisa.. huko kwa mtalaam

R I p sonso
Angeenda kawe kwa mwamposa pengine yasingetokea haya
R.I.P
 
Jamaa anadai kabla ya game ya ruvu vs Simba huko ccm kilumba alihisi maumivu wa mguu akaongea na daktari wao akampa dawa ya kutuliza maumivu ..

Kesho yake pia akaona maumivu yanazidi basi kwenye hiyo game hakupangwa.. lakini akaanza kuona mguu unavimba kama tende akaongea na daktari wao wakampeleka muhimbili kwa matibabu zaidi

Basi baada ya matibabu hapo muhimbili akaomba akatabiwe kwao.. maana taarifa alizo zipata ni kwamba katupiwa jini

Basi mguu ukaendelea kuoza na kuharibika kabisa.. huko kwa mtalaam

R I p sonso
Huko tiba asili siyo salama sana haswa kipengele cha mguu
 
Mikia msimu huu mnalo kweli kweli, kila baya la kimichezo ndani ya nchi hii chanzo ni nyie, mlimpiga msumari nyie………………….!

"Bwire amesema Sonso beki huyo alipata majeraha mara baada ya mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Simba, uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza"
 
Mikia msimu huu mnalo kweli kweli, kila baya la kimichezo ndani ya nchi hii chanzo ni nyie, mlimpiga msumari nyie………………….!

"Bwire amesema Sonso beki huyo alipata majeraha mara baada ya mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Simba, uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza"
alaaalaaa kumbe hatukusikia vizuri eeheee , siyo kwamba alipangwa akamuambia mkwasa hajisikiii poa mchan akatolewa kwenye list? umewek kabisa na quotation marks ukamlisha masau biwre maneno ya uongo. shame on you
 
Halafu ndo kuna wapuuzi huwa wanasema hakuna uchawi kwenye soka.
Hakuna uchawi hapo. Ni kukosa maarifa au kujaa hofu kwa wachezaji wetu. Hilo ni tatizo ambalo linatibika vyema kabisa hospitali.
Inaonekana alishakuwa kwenye ‘Complication stage’ ndo akaenda Muhimbili.

Pia nina shaka na ‘Medical team’ ya Ruvu Shooting. It’s either hawajui ama wanafanya ‘Mazoea’ kwenye afya za wachezaji wao.
 
Back
Top Bottom