Kilimanjaro: Lyatonga Mrema kufunga ndoa Alhamisi Machi 24, 2022 katika Parokia ya Uwomboni kijijini kwake Kiraracha

Kilimanjaro: Lyatonga Mrema kufunga ndoa Alhamisi Machi 24, 2022 katika Parokia ya Uwomboni kijijini kwake Kiraracha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Siku moja kabla ya kufunga ndoa Mwenyekiti wa TLP Taifa, Dk. Augustino Mrema amesema kuwa atajaribu kujikokota kuelekea Kanisani na kama itatokea ataishia njiani kutokana na afya yake kutokuwa sawa, anaamini Paroko atajua nini cha kufanya.

Mrema amesisitiza kuwa huduma ya Kanisa inapatikana popote, ikitokea hata ameshindwa kwenda Kanisani anaweza kufungishwa ndoa chumbani kwake au hata kitandani kwake ilimradi wahusika wameridhia.

Kuhusu kuoa akiwa mtu mzima, Mrema amesema: “Dhumuni la ndoa ni kupata watoto kama hawapatikani si basi, kwani kuna ugomvi?”

Mrema anatarajiwa kufunga ndoa Alhamisi Machi 24, 2022 katika Parokia ya Uwomboni kijijini kwake Kiraracha mkoani Kilimanjaro.

Mrema ambaye ana umri wa miaka 77 akiwa pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya PAROLE Tanzania, amekuwa akijinadi kupata mrembo mwenye umri mdogo na mweupe, anafunga ndoa baada ya kumpoteza aliyekuwa mkewe Rose Mrema aliyefariki dunia mwaka jana.

Amesisitiza kuwa kilichomsukuma kuoa ni kumpata msaidizi wa kumsaidia katika maisha yake kwani yeye ni mzee na anahitaji mtu wa karibu wa kumwangalia na kumsaidia kwa ukaribu, akisisitiza familia yake kumpa ruhusa ya ndoa hiyo.

“Kuhusu jina la mke wangu mtarajiwa mtalijua siku ya ndoa, pia kutakuwa na sherehe nyumbani kwangu pamoja na ibada ambapo Paroko pia atazindua sanamu ya mtakatifu Augustino hapohapo nyumbani kwangu,” alisema Mrema.



Pia soma...
Augustino Mrema kufunga ndoa Machi 24, 2022. Amepata kimwana mdogo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Fellas, get brains and rim jobs while still young so you don't end up trading away your lifetime bread for nothing. Let your joystick run wild when there's still room for recovery. No school will teach you.
 
Mbona nasikia mrembo karuka kwamba haolewi au wanacheza na akili za wabongo
 
Mrembo lazima aolewe,nadhani hiyo ndoa itakua na waandishi wa habari wengi sana.
 
Afadhali yake sio wa upande wa dini ile.., umri huo angelijuta kutangaza ndoa kwa matusi ya wabongo
 
Miaka 77?
Alafu kachukua mtoto mbichi.
Anataka agundue Nini?
 
Alex Ferguson na Wenger wana 70+ lakini hawaonyeshi kuisha kama Mrema.

Na hii ni kwa wabongo wengi wakifikisha umri huo tu wanakua hoi kimwili na hata akili zinaanza kupotea. Shida ni lishe au hali ya hewa?
 
Back
Top Bottom