Kilimanjaro: Mwalimu ampiga Mwanafunzi hadi kifo

Kilimanjaro: Mwalimu ampiga Mwanafunzi hadi kifo

Mwanafunzi wa darasa la kwanza, shule ya msingi Samanga, Wilaya, ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, Sistus Aristid Kimario. (7) amefariki dunia kwa kile kinachodaiwa ni kuchapwa viboko na mwalimu wake kwa kosa la kupiga kelele darasani.

Inadaiwa baada ya mwalimu huyo, James Urassa kutekeleza adhabu hiyo alitoroka kusikojulikana baada ya kubaini mwanafunzi huyo amefariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema tukio hilo limetokea Julai 17, mwaka huu, baada ya mwalimu huyo kumtandika viboko mwanafunzi huyo na kusababisha umauti wake.

"Jeshi la Polisi tunaendelea kumsaka mwalimu huyu kwa sababu baada ya kubaini mwanafunzi huyo amefariki amekimbia," alisema Kamanda Maigwa.

Alipotafutwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Charles Chavunike, alikiri kutokea kwa tukio hilo Julai 17, mwaka huu saa tatu asubuhi.

Mwalimu huyo alisema akiwa darasani aliona walimu wawili wa shule hiyo wakiwa wamembeba mwanafunzi huyo akitolewa darasani na alipowauliza nini kimetokea alijibiwa mwanafunzi kaanguka darasani

"Baada ya hapo niliita watoto wawili wa darasa la kwanza nikawahoji ni kitu gani kimetokea darasani, ndiyo wakanieleza mwalimu alimchapa mwenzao kwa sababu ya kupiga kelele darasani," alisema.

Alisema baada ya tukio hilo alilazimika kufuata taratibu zote na kutoa taarifa kwa viongozi wa wa kata na vyombo vingine vya dola.

Naye babu wa mwanafunzi huyo, Patricky Kachomba alise-ma mpaka anaondoka kwenda shule alikuwa haumwi popote.
Profesa Adolf Mkenda ‘ waziri wa Elimu na Mbunge waJimbo la Rombo , sasa umebipiwa!!
 
Huko Kilimanjaro Mwalimu amempiga mwanafunzi wa darasa la kwanza mwenye umri wa miaka saba mpaka kifo kwa kosa la kupiga kelele darasan 🥲

Kwenye picha huyo ni Mama yake Mzazi wa huyo mwanafunzi ameeleza kwamba Mwalimu

Alimpiga sana mwanafunzi huyo mpaka alijikojolea baada ya hali kuwa mbaya ya mwanafunzi alifariki dunia, Mwalimu amekimbia na jeshi la polisi linaendelea kumtafuta huyo Mwalimu na kufanya uchunguzi wa shitaka hili.

#VibokoSioLazima

Credit: UTV Habari

---

Mwanafunzi wa darasa la kwanza, shule ya msingi Samanga, Wilaya, ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, Sistus Aristid Kimario. (7) amefariki dunia kwa kile kinachodaiwa ni kuchapwa viboko na mwalimu wake kwa kosa la kupiga kelele darasani.

Inadaiwa baada ya mwalimu huyo, James Urassa kutekeleza adhabu hiyo alitoroka kusikojulikana baada ya kubaini mwanafunzi huyo amefariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema tukio hilo limetokea Julai 17, mwaka huu, baada ya mwalimu huyo kumtandika viboko mwanafunzi huyo na kusababisha umauti wake.

"Jeshi la Polisi tunaendelea kumsaka mwalimu huyu kwa sababu baada ya kubaini mwanafunzi huyo amefariki amekimbia," alisema Kamanda Maigwa.

Alipotafutwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Charles Chavunike, alikiri kutokea kwa tukio hilo Julai 17, mwaka huu saa tatu asubuhi.

Mwalimu huyo alisema akiwa darasani aliona walimu wawili wa shule hiyo wakiwa wamembeba mwanafunzi huyo akitolewa darasani na alipowauliza nini kimetokea alijibiwa mwanafunzi kaanguka darasani

"Baada ya hapo niliita watoto wawili wa darasa la kwanza nikawahoji ni kitu gani kimetokea darasani, ndiyo wakanieleza mwalimu alimchapa mwenzao kwa sababu ya kupiga kelele darasani," alisema.

Alisema baada ya tukio hilo alilazimika kufuata taratibu zote na kutoa taarifa kwa viongozi wa wa kata na vyombo vingine vya dola.

Naye babu wa mwanafunzi huyo, Patricky Kachomba alise-ma mpaka anaondoka kwenda shule alikuwa haumwi popote.


Hata kusoma ni ngumu, unampigaje mtoto helpless?
 
Bora kesi nyingine ila sio ya mauaji. Hii kesi huwa inafuatiliwa mwanzo mwisho. Mwalimu atakimbia kimbia ila watamkamata na ndo itakuwa mwisho wake kuonekana uraiani. Hapo tayari mwalimu kashaharibu maisha yake yote yaliyobakia. Isitoshe ishu ishafika kwenye vyombo vya habari hivyo watetezi wa haki za watoto na wanasiasa lazima wajichukulie maujiko kupitia hii ishu. Hili ni fundisho kwa waalimu wengine kusoma alama za nyakati.
 
Hamjui tu yaliyotokea , mtt alikuwa na tatizo lake binafs ,SEMA wachaga wa useri wamechachamaa [emoji15] sisis ndo wachaga asee[emoji33]
 
Tena na hivyo mishahara haiongezwi mtegemee Mengi zaidi
 
Tukikataza kupiga watoto tunaitwa wakina mama Junia [emoji24][emoji24][emoji24]

Rest in Peace Angel, [emoji885]

Huyo bazazi atahangaika na Dunia na atakufa kifo cha kikatili sana.
Tatizo kubwa ni kwamba bado serikali inaruhusu adhabu ya viboko. Najua kuna utaratibu wameweka wa kuchapa wanafunzi lakini hakuna mwalimu au shule inayoufuata na serikali iko reluctant kukazia au kufuatilia. Dunia ya sasa iliyostaarabika viboko ni adhabu ya kikatili mno. Hebi fikiria mtoto wa miaka 7 anaanza kupata kipigo kikali namna hiyo!
 
Back
Top Bottom