DOKEZO Kilimanjaro: Shule ya Msingi ya Serikali yaandikisha Wanafunzi watatu (3) kuanza Darasa la Kwanza

DOKEZO Kilimanjaro: Shule ya Msingi ya Serikali yaandikisha Wanafunzi watatu (3) kuanza Darasa la Kwanza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Mlembea, ni moja ya Shule ya Serikali iliyopo Wilaya ya Rombo katika Tarafa ya Mashati Mkoani Kilimanjaro ambapo kwa Mwaka huu wa 2024 imeandikisha Wanafunzi watatu tu (3) kuingia darasa la kwanza kitu ambacho sio kawaida.

Shule hiyo ya Msingi Mlembea jumla ya idadi ya wanafunzi katika shule nzima Kuanzia chekechea hadi darasa La saba inakadirwa kuwa na wanafunzi tisini (90) tu.

Sababu kuu mbili za shule hiyo kuwa na idadi ndogo ya wanafunzi kuliko shule nyingine inatajwa kuwa ni mambo ya kishirikina yaliyotokea miaka ya nyuma ambapo wanafunzi walikuwa wanadondoka wawapo shuleni hivyo kufanya wazazi kuhamisha watoto wao na kuwaandikisha katika shule nyingine. Ndani ya Tarafa hiyo.

Pia soma:
  1. Mkurugenzi Rombo: Shule iliyoandikisha Wanafunzi Watatu hakuna imani za kishirikina ni maamuzi ya wazazi tu
  2. Kilimanjaro: Baada ya Shule kuandikisha Wanafunzi Watatu tu, Serikali yaanzisha msako kutafuta Watoto waliopo mtaani
Sababu ya pili inatajwa na baadhi ya wadau ni masuala ya uzazi. Idadi ya Vijana wamekimbilia Mijini na idadi ya vijana waalibaki kuingia kwenye ulevi na hivyo kushindwa kujenga familia.

 
Sema Uchagani wamebaki wazee kiukweli. Nilienda kuhesabiwa, niliona wazee wengi sana, kila unapopita/enda wazee tu vijana wachache sana.

Ni kweli vijana wengi Uchagani wanakimbilia Mijini. Kwaiyo hata uzazi pia lazima uwe kidogo.
 
Sema Uchaga wamebaki wazee kiukweli..,nilienda kuhesabiwa, niliona wazee wengi sana, kila unapopita/enda wazee tu vijana wachache sana.

Ni kweli vijana wengi Uchagani wanakimbilia Mijini!
Kwaiyo hata uzazi pia lazima uwe kidogo.
Ni tatizo la mkoa mzima hata uko upareni kuna shule zimefungwa kwa kukosa wanafunzi
 
Sema Uchaga wamebaki wazee kiukweli..,nilienda kuhesabiwa, niliona wazee wengi sana, kila unapopita/enda wazee tu vijana wachache sana.

Ni kweli vijana wengi Uchagani wanakimbilia Mijini!
Kwaiyo hata uzazi pia lazima uwe kidogo.
... ardhi ya kule imebaki kwa ajili ya kwenda kuzika tu na kugeuza.
 
Shule ni nyingi za serekali + private!

Pili, idadi ndogo ya watu vijijini, wengi wameenda tafuta maisha mijini.

Vijijini % kubwa kumebaki wazee na makaburi, si uchagani tu hata huko upareni
 
Nakumbuka miaka ya 93 kuna shule moja ya msingi darasa la saba walikuwa 27 tu!wavulana 11 na wasichana 16
 
Mlembea, ni moja ya Shule ya Serikali iliyopo Wilaya ya Rombo katika Tarafa ya Mashati Mkoani Kilimanjaro ambapo kwa Mwaka huu wa 2024 imeandikisha Wanafunzi watatu tu (3) kuingia darasa la kwanza kitu ambacho sio kawaida.

Shule hiyo ya Msingi Mlembea jumla ya idadi ya wanafunzi katika shule nzima Kuanzia chekechea hadi darasa La saba inakadirwa kuwa na wanafunzi tisini (90) tu.

Sababu kuu mbili za shule hiyo kuwa na idadi ndogo ya wanafunzi kuliko shule nyingine inatajwa kuwa ni mambo ya kishirikina yaliyotokea miaka ya nyuma ambapo wanafunzi walikuwa wanadondoka wawapo shuleni hivyo kufanya wazazi kuhamisha watoto wao na kuwaandikisha katika shule nyingine. Ndani ya Tarafa hiyo.

Sababu ya pili inatajwa na baadhi ya wadau ni masuala ya uzazi. Idadi ya Vijana wamekimbilia Mijini na idadi ya vijana waalibaki kuingia kwenye ulevi na hivyo kushindwa kujenga familia.
double kick ni noma!!!
 
Nasikia wachagga tangu wakiwa wadogo hawapendi ishi ama fanya biashara mahali penye mambo ya kishirikina sanaaa
 
Kuna shule ya msingi naijua kule Ina wanafunzi 90 shule nzima
 
Back
Top Bottom