Kilimo cha maembe ya kisasa

Kilimo cha maembe ya kisasa

Tafuta mashine ya kukamua juice baadae badala ya kuwa supplier wa Bakhressa
Au utakaa nayo mbele ya nyumba kama wanaouza matikiti?
Ubunifu muhimu ila mawazo sio mabaya
Swali kwanini ujikite kwenye maembe tu kama ardhi unayo?
Panda matunda aina hata 5
 
Unapoteza muda ndugu, ungetuuliza tuliozaliwa na kukulia Tabora kabla ya kuingia gharama zote hizi ikitarajia mapato hewa hewa (ya kwenye makaratasi).

Msimu wa maembe huko Tabora huwa yanagawiwa bure, yaani inafika muda Kenta zima linuzwa elfu 30. Ili unielewe vizuri uliza watu wa Iringa, msimu wa nyanya baei inakuwaje. Na kwanini kilimo cha nyanya hakiwatoi.

Pia waulize watu wa huko Mbeya na Njombe kwanini kilimo cha parachichi hakiwatoi?

Wakati wewe ukihangaika kupanda miembe, Kuna maeneo huko Tabora wamezaliwa na kukuta msitu wa miembe.
Mkuu parachichi zinawatoa watu. Mwaka huu kuna watu wameuza kilo sh 200 wengine sh. 1600.Inategemea factor nyingi.
Lakiini mkuu kwa nini tusianze kuwaza lama wenzetu wachina,wahindi, wazungu nk. Wao wanatoa product nyingi badala kuuza tinda la kula.
 
Kwa nini alikimbie?Tunaomba wenye uzoefu wa mkoa/mikoa mingine mfano Pwani au Tanga kuhusu soko la maembe
Kwenye hii nchi tatzo ni soko,akina kikwete ndo wanalima wanauhakika wa soko

Juzi kuna jamaa kalamba teuzi kalikimbia shamba la nyanya,kama kungekuwa na soko asingezikimbia nyanya

huku mwanza kuna jamaa alipanda hayo maembe lakin huwa naona anajiuzia mwenyew kwenye kamji ambako kana watu elfu 10 tu,hapo lazima mzigo uoze,pia mengi hutoka shamban yakiwa yameoza kwa ndani,wateja huwa wanamlalamikia sana,wengi siku hz wameshaanza kuyapotezea
 
Katika hekaheka za kujiandaa kustaafu miaka 7 baadae nimeamua nipande miche kama 500 yaani ekari 10 za maembe kisasa.

Shamba lipo Tabora kwa sasa naendelea kuchimba mashimo. Nitapanda bila mbolea ya samadi ila taweka NPK baada ya miezi 3 ikiwa imeshika.

Mpango wangu miche 450 ipone ili nipate wastani wa embe 500 kila mti mwaka wa 6 na hii itanipa embe 225,000 na kama tauza kwa Tzs 400 nipate 90m.Hapo nitaamua kustaafu kazi nikiwa na miaka 55.
Ni kilimo kizuri,ila panda embe bolibo ya asili kwa kuwa hupo hapo Tabora.Soko lako litakuwa la uhakika kwa kuwa ndiyo embe wanazotumia Bhakharesa na Jamukaya kutengeneza juice.
 
Katika hekaheka za kujiandaa kustaafu miaka 7 baadae nimeamua nipande miche kama 500 yaani ekari 10 za maembe kisasa.

Shamba lipo Tabora kwa sasa naendelea kuchimba mashimo. Nitapanda bila mbolea ya samadi ila taweka NPK baada ya miezi 3 ikiwa imeshika.

Mpango wangu miche 450 ipone ili nipate wastani wa embe 500 kila mti mwaka wa 6 na hii itanipa embe 225,000 na kama tauza kwa Tzs 400 nipate 90m.Hapo nitaamua kustaafu kazi nikiwa na miaka 55.
Maembe haya haya? Njoo huku Ipwasi Idodi yapo ya kuokota tu na bado watu hawajastaafu sababu ya maembe.
 
Kent inapatikana wapi na ina sifa zipi ?

..Kent sifa yake kubwa ni kwamba inazaa nje ya msimu ambao miembe mingine huzaa.

..kwa hiyo mkulima akimaliza kuvuna mdodo, boribo,etc, ndipo Kent nazo zinaanza kuzaa.

..unaweza kupata miche kwenye vituo vya serikali kama mabwepande, au kwa wauza miche ya matunda.

..jaribu kwa mwanachama mwenzetu wa JF Lily Tony huenda akawa nayo.
 
Good.
Ila mi nashauri upande na ya kienyeji ila uyapande kisasa. Mfano embe bolibo na embe dodo ni maembe mazuri yanayopendwa Tanzania.
Kitu kingine kwa uzoefu wangu wa kupanda miti ya matunda, ili upate idadi ya miti uliokusudia zidisha miche halafu ikishika ikikua una punguza miti na kubakiza idadi unayotaka.
heka badala ya miche 80 panda 100.
Miti mpaka ije ifungane unakuwa ushavuna mara kadhaa ndio unaipunguza.
Hiyo dodo mpaka kuja kuanza kuvuna si miaka 29 huko
 
Mpango wangu miche 450 ipone ili nipate wastani wa embe 500 kila mti mwaka wa 6 na hii itanipa embe 225,000 na kama tauza kwa Tzs 400 nipate 90m.Hapo nitaamua kustaafu kazi nikiwa na miaka 55.
Mkuu umeweka makadrio ya juu mno! Mti mmoja wa hizi embe unaita za kisasa huwezi kupata maembe 500 kwa umri huo wa miaka 6, Umezaa sana ni kati ya 200 na 300. Mimi ninao una miaka 11 leo lakini sijawahi kupata maembe zaidi ya 300 kwa msimu. Hivyo hesabu zako aifanye ziwe za chini sema maembe 200 x 450 = maembe 90,000 kwa msimu x TZS 200 = 18,000,000 kwa msimu!
 
Hiyo dodo mpaka kuja kuanza kuvuna si miaka 29 huko
Hapana mkuu huwa wanayafanyia budding au grafting. Unachukua kikonyo cha mwembe uliokomaa unakipandikiza kwenye kishina cha mwembe dodo mchanga. Baada ya kama miaka miwili hadi mitatu unaanza kutoa matunda. Hapa kuna kitu hamjakielewa, hata hiyo wanayosema ya kisasa siyo kwamba inapatikana kwa kupanda kokwa! Ukitegemea kokwa ndiyo hiyo ya kusubiri miaka 20! Kwangu nilipanda kokwa la embe dodo miaka 6 iliyopita ndiyo mwaka huu umeanza kutoa matunda.
 
..Kent sifa yake kubwa ni kwamba inazaa nje ya msimu ambao miembe mingine huzaa.

..kwa hiyo mkulima akimaliza kuvuna mdodo, boribo,etc, ndipo Kent nazo zinaanza kuzaa.

..unaweza kupata miche kwenye vituo vya serikali kama mabwepande, au kwa wauza miche ya matunda.

..jaribu kwa mwanachama mwenzetu wa JFLily Tony huenda akawa nayo.
JokaKuu asante
 
Mkuu karibu sana SUA tukuhudumie,tuna miche ya maembe aina Saba tofauti tofauti Kwa bei sh 2000 kila mche.
Tuna Aina zifuatazo
1.Dodo
2.Bolibo
3.Tommy
4.Kent
5.Alphonso
6.embe Tanga
7.red Indian
 
Katika hekaheka za kujiandaa kustaafu miaka 7 baadae nimeamua nipande miche kama 500 yaani ekari 10 za maembe kisasa.

Shamba lipo Tabora kwa sasa naendelea kuchimba mashimo. Nitapanda bila mbolea ya samadi ila taweka NPK baada ya miezi 3 ikiwa imeshika.

Mpango wangu miche 450 ipone ili nipate wastani wa embe 500 kila mti mwaka wa 6 na hii itanipa embe 225,000 na kama tauza kwa Tzs 400 nipate 90m.Hapo nitaamua kustaafu kazi nikiwa na miaka 55.
we jamaa unatembea na akili yangu kabsa mimi Niko dsm hata najipanga nipate m4 naenda sua nanunua embe Miche 500 na ndimu Miche 1000 mambo yakuwa sawa nataka na limao Miche hata 300 bahada ya hapo nakomaa na madawa na palizi hongera sana mkuu umefanya maamuzi mazuli.
 
Mkuu karibu sana SUA tukuhudumie,tuna miche ya maembe aina Saba tofauti tofauti Kwa bei sh 2000 kila mche.
Tuna Aina zifuatazo
1.Dodo
2.Bolibo
3.Tommy
4.Kent
5.Alphonso
6.embe Tanga
7.red Indian
mkuu naomba no yako nbox
 
Mkuu umeweka makadrio ya juu mno! Mti mmoja wa hizi embe unaita za kisasa huwezi kupata maembe 500 kwa umri huo wa miaka 6, Umezaa sana ni kati ya 200 na 300. Mimi ninao una miaka 11 leo lakini sijawahi kupata maembe zaidi ya 300 kwa msimu. Hivyo hesabu zako aifanye ziwe za chini sema maembe 200 x 450 = maembe 90,000 kwa msimu x TZS 200 = 18,000,000 kwa msimu!
Unauzia wapi mkuu
 
Katika hekaheka za kujiandaa kustaafu miaka 7 baadae nimeamua nipande miche kama 500 yaani ekari 10 za maembe kisasa.

Shamba lipo Tabora kwa sasa naendelea kuchimba mashimo. Nitapanda bila mbolea ya samadi ila taweka NPK baada ya miezi 3 ikiwa imeshika.

Mpango wangu miche 450 ipone ili nipate wastani wa embe 500 kila mti mwaka wa 6 na hii itanipa embe 225,000 na kama tauza kwa Tzs 400 nipate 90m.Hapo nitaamua kustaafu kazi nikiwa na miaka 55.
Wazo zuri mstaafu mtarajiwa, tafuta mbinu ya kupambana na madalali pia usisahau wataalam wa kilimo kwa miongozo.
 
Mkuu karibu sana SUA tukuhudumie,tuna miche ya maembe aina Saba tofauti tofauti Kwa bei sh 2000 kila mche.
Tuna Aina zifuatazo
1.Dodo
2.Bolibo
3.Tommy
4.Kent
5.Alphonso
6.embe Tanga
7.red Indian
Ni vyema ukaweka mawasiliano yako hapa
 
Ni vyema ukaweka mawasiliano yako hapa
0719527062
0757056472
Karibu mkuu ninapatikana 24/7
Lakini pia ipo Uzi hapa Jf ambao nimeelezea kwa kirefu kidogo kuhusu miche mbalimbali ya matunda.
Ukipata nafasi unaweza kuupitia pia Kwa maelezo zaidi
 
Back
Top Bottom