Unapoteza muda ndugu, ungetuuliza tuliozaliwa na kukulia Tabora kabla ya kuingia gharama zote hizi ikitarajia mapato hewa hewa (ya kwenye makaratasi).
Msimu wa maembe huko Tabora huwa yanagawiwa bure, yaani inafika muda Kenta zima linuzwa elfu 30. Ili unielewe vizuri uliza watu wa Iringa, msimu wa nyanya baei inakuwaje. Na kwanini kilimo cha nyanya hakiwatoi.
Pia waulize watu wa huko Mbeya na Njombe kwanini kilimo cha parachichi hakiwatoi?
Wakati wewe ukihangaika kupanda miembe, Kuna maeneo huko Tabora wamezaliwa na kukuta msitu wa miembe.