Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Mkuu hatua uliyofikia ni kubwa sana huitaji kupunguza uzalishaji kwa kuhofia soko Bakresa anatoa bei nzuri sana kwa matikiti last time ilikuwa 800 TZS per kg ila ananunua minimum 250 tones so kama una eneo kubwa kacheki nao ustrike hiyo dili then uongeze uzalishaji
Habari,
hii habari si kweli,nlifika kiwandani kwao,wakaniambia matunda pekee wanayonunua ni machungwa na maembe tena si kila siku,kuna miezi maalum.
 
Naweza kukukodisha eka moja kwa Tsh 60,000/ unanilipa kabla, shamba lipo Pwani ya Mkuranga,maji yapo mengi sana,banda la kuishi kijana lipo. Unaweza pata eka hata 15 zilizo kando ya maji ya kudumu.

Please naomba unitumie contact zako kwenye PM
 
Zaidi ya 80% ya matajiri duniani ama wametajirika kwa ukulima ama wametajirika kwa mazao ya ukulima.

Sio kwa kulima directly lakini wengi wao walikuwa wanunuzi wa mazao ya kilimo kama middle men
 
Mie nataka kulima Mtwara je inawezekana????
Popote tu mkuu alimradi usiwe udongo wa mfinyanzi. Huo ukanda wa Pwani tikiti linastawi tu vizuri ila usilime wakati wa mvua, matikiti hayapatani na mvua, inabidi iwe wakati wa kiangazi na iwe Kwa kumwagilia.
 
Habari zenu wadau.

Wakuu mimi nataka kujaribu kulima tikiti maji kipindi hiki cha masika. Nitafanya kilimo cha kisasa. Mbegu ni Sukari F1 hybrid.

Tatizo nimekuwa nikipata ushauri tofauti kuhusu kipindi hiki ambacho masika inakaribia kuanza (Takribani mwezi mmoja baadaye) Wengine wanasema Matikiti hayapendi mvua nyingi, wengine wanasema kama nitayahudumia kwa madawa hakutakuwa na tatizo.

Wakuu naombeni mawazo yenu, je inawezekana nikafanikiwa kuvuna kipindi hiki cha masika?

Natanguliza Shukrani.
 
Waheshimiwa ina maana hakuna mwenye kujua na kunisaidia katika jambo hili? Msaada wenu tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu wadau.

Wakuu mimi nataka kujaribu kulima tikiti maji kipindi hiki cha masika. Nitafanya kilimo cha kisasa. Mbegu ni Sukari F1 hybrid.
Tatizo nimekuwa nikipata ushauri tofauti kuhusu kipindi hiki ambacho masika inakaribia kuanza (Takribani mwezi mmoja baadaye) Wengine wanasema Matikiti hayapendi mvua nyingi, wengine wanasema kama nitayahudumia kwa madawa hakutakuwa na tatizo.

Wakuu naombeni mawazo yenu, je inawezekana nikafanikiwa kuvuna kipindi hiki cha masika?

Natanguliza Shukrani.

matikiti yana tabia ya kupasuka wakati wa maska. Kama utalma yapandshie kwe bed lefu na uliweke matandazo. Nakushaur tumia mbegu ya sentinel f1 n nzur kubwa na soko lake la uhakika.
 
Asante Mkuu, but nilikuwa nataka kujua changamoto zinazoweza nipata kipindi hiki cha mwanzo cha masika katika ukulima wa tikiti

Mkuu Malila, Malafyale, Avatar na wengineo msaada wenu tafadhali

Kilimo kina changamoto nyingi sana, nikuulize swali, wewe unataka kulimia wapi? Je ni huku Pwani au mikoani? Ninachojua, tikiti la masika linasumbua ila likitoka soko lake ni kubwa balaa, kiasi kwamba unaweza dhani ulichelewa wapi, ila ukikosea step kidogo tu,kilio chake hakichukuliki.

Nijibu hayo maswali kwanza.
 
Kilimo kina changamoto nyingi sana, nikuulize swali, wewe unataka kulimia wapi? Je ni huku Pwani au mikoani? Ninachojua, tikiti la masika linasumbua ila likitoka soko lake ni kubwa balaa, kiasi kwamba unaweza dhani ulichelewa wapi, ila ukikosea step kidogo tu,kilio chake hakichukuliki.

Nijibu hayo maswali kwanza.

Nalimia mkoani mkuu Malila
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom