Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Ndio maana naipenda jf university collegge hapa unapata elimu bila cheti safi sana mm nipo znz lakini nataka kukimbia huku nihamie dar ili nilime haya matikiti maana huku znz yana soko balaa hasa kwenye mahotel ya kitalii.

Big up kwa hili darasa nimelipenda
 
wapendwa naomba kujua aina gani ya mbegu ni nzuri na pia mnijuze garama ya mbegu, na ni kiasi gani mbegu ya tikiti inahitjika kwa heka mbili. Natanguliza shukrani wakuu!!
 
mbegu nzur ni za hybrid.
1. Pata negra inazaa vizur.
2. Sentinel mbegu ya rang ya pundamilia 2nda lenye umbo la yai
3. Sukari f1nayo nikama s3ntinel
Bei 1.pata negra 1000 seeds sh. 42,000
Sentinel 1000 seeds sh 50,000
Sukari F1 25g -17.000
50g-30.000

100g -55.000
500g- 220.000
 
mbegu nzur ni za hybrid.
1. Pata negra inazaa vizur.
2. Sentinel mbegu ya rang ya pundamilia 2nda lenye umbo la yai
3. Sukari f1nayo nikama s3ntinel
Bei 1.pata negra 1000 seeds sh. 42,000
Sentinel 1000 seeds sh 50,000
Sukari F1 25g -17.000
50g-30.000

100g -55.000
500g- 220.000

mkuu nashukuru sana kwa maelezo mazuri, mimi ndio ninataka niingie kwenye hichi kilimo. Nitakushukuru sana ukinidadavulia vizuri gharama zake kwa ujumla ktk hizi heka mbili ili nijipange vzri nisije kuishia njiani!
 
mkuu nashukuru sana kwa maelezo mazuri, mimi ndio ninataka niingie kwenye hichi kilimo. Nitakushukuru sana ukinidadavulia vizuri gharama zake kwa ujumla ktk hizi heka mbili ili nijipange vzri nisije kuishia njiani!

Mkuu unataka kulimia pande za wapi??
 
maverick supplies, ni kampuni inayoshughulika na uuzaji wa mazao ya chakula hasa mayai na matikiti maji. Kwa yeyote mwenye mahitaji ya kuuziwa bidhaa izi kwa tender au kwa jumla, naomba afanye mawasiliano na mkurugenzi wa kampuni kupitia 0713079661 kwa maelewano ya kibiashara

that great
 
1) Mtaji unategemea na jinsi wewe mwenyewe unavyofanya kilimo chako, watu uliowaajiri n.k. Kwa mfano, kama unamwagilia inategemea unamwagilia na nini, pump ya mguu kama MoneyMaker au ya Petrol? Zote mwisho wa siku utapata faida tofauti. To be on the safe size, weka 1M hadi kuvuna. Ila inaweza ikazidi au ikapungua.

2) Matikiti yanachukua miezi miwili hadi kukomaa

3) Kama wewe ni mjasiriamali unapaswa kujua soko kabla ya kuamua kulima. So tafuta soko kwanza, then ndo uamue kulima.

4) Kipindi cha kipupwe ndio kizuri kwa matikiti maji. Matikiti maji hayapendi mvua nyingi. Yakipata maji mengi karibia na mavuno yanaweza kupasuka yakiwa shambani ukapata hasara.

5) Karibu Mkuranga tulime matiki. Ila maeneo mengi ya ukanda wa pwani ni mazuri kwa matikiti maji.

Hope that helps.

MKURANGA UNATUMIA UTARATIBU GANI KUMWAGILIA? Pia nielekeze mkuranga maeneo gani unakolimia? Tuwasiliane if possible 0712 661366 email jmalove23@gmail.com
 
Drip irrigation ni somo refu sana, so inabidi nijipange sana ili kuelezea kitu kinachoeleweka. Ila kwa kifupi, kuna mambo machache ya kuzingakita kama ifuatavyo:

1) Umbali kati ya mche na mche (Plant Spacing)
Umbali kati ya mche na mche kwa zao la matikiti maji hutofautiana kutokana na ulimaji. Kuna wengine huacha umbali wa 1.8 - 2.0m kati ya shimo na shimo na kila shimo wanaacha miche mitatu hadi minne. Kuna wengine wanaacha nafasi ya 1.0m na wanaweka miche miwili kila shimo.

Binafsi nilikua nataka kujaribu kuacha nafasi ya 0.5m na kuacha mche mmoja kila shimo, ingawa kuna wengine wanasema unaweza ukaacha umbali wa 0.3 - 0.4m kwa kila mche. Mimi nimeshawahi kuacha nafasi ya 1.5m kati ya shimo na shimo na kila shimo niliacha miche mitatu.

Unapochagua drip tapes (ambayo ni mipira midogo yenye matundu) unatakiwa uzingatie umbali kati ya mmea na mmea kutokana na ulimaji wako. Kuna drip tapes zenye umbali wa 10cm ~ 30cm na kuendelea. Ila ambazo zinapatikana sana ni zile za 20cm and 30cm.

Hivyo, kama unataka uache umbali wa 1.5m kati ya shimo na shimo basi utapata wakati mgumu sana kupata drip tapes zenye umbali huo.

Kama unataka kulima tikiti maji, tafuta drip tapes za 30cm spacing na unaweza ukaruka tundu (dripper) moja kila baada ya mche. Hii itafanya umbali kati ya mche na mche kuwa 60cm.

2) Ukubwa wa mabomba (Main and Sub-main Pipe Sizes)
Kwenye drip irrigation unatakiwa utumie mabomba kuendana na kiasi cha maji kinachohitajika shambani. Kadiri maji yanavyohitajika kwa wingi ndio unavyolazimika kutumia mabomba makubwa. Kwa ekari moja unaweza tumia sub-main yenye ukubwa wa 2" hadi 2.5" kutegemeana ma mwinuko wa shamba.

3) Kiasi cha maji kinachohitajika (Water consumption)
Unalazimia kukokotoa kiasi cha maji kinachohitajika shambani ili uweze kutengeneza ratiba yako ya umwagiliaji. Kwa mfano, kama shamba lako lina miche 4,000 na kila mche mmoja unatakiwa kiasi cha maji cha lita 2 kwa siku, basi shamba lako kwa siku litahitaji lita 8,000. Kama unamwagilia mara mbili, basi asubuhi lita 4,000 na jioni lita 4,000. Hii itakufanya uwe na ratiba mbili kwa siku.

Kama ratiba ya asubuhi hufanyika ndani ya saa moja, basi inabidi uwe na mabomba (main and sub-main) ambayo yanaweza kupitisha lita 4,000 za maji kwa saa. Pia lazima uwe na pump yenye uwezo wa kusukuma kiasi hiki cha maji kwa saa katika presha inayotakiwa. Drip system nyingi hutumia pressure ya 0.7 - 1.0bar. So pump yako lazima iweze kusukuma kiasi cha lita hizo kwa saa kwa msukumo wa 1.0bar.

Pia, drip tapes zako lazima ziwe na matundu yenye flow rate ya 1 litter per house (1lph) at the operating pressure. (could be 0.7 ~ 1.0bar depending on dripper construction)

Kama nilivyokwisha sema, mambo ni mengi kwenye drip irrigation. Ila kwa leo naomba niishie hapa. Kama una swali uliza tuelimishane taratibu.

KAKA UNALIMIA WAPI NIMEHAMASIKA! Tuwasiliane 0712 661366 au jmalove23@gmail.com
 
mwana jf naombeni mawazo yenu kuhusu matikiti kuwekea mbolea za kisasa yaani urea+can+npk hizi zinawekwa wakati mche una siku ngani naomba ufafanuzi wake na kipimo size gani kwa kila mche waungwana miche yangu ina wiki mbili sasa naomben msaada wenu ktk hilo jamani asanteni.

mtama unatengenezea chibuku tbl wnanunua shayiri,ni jamii ya ngano

tafuta solution mkuu kwa kufikiri nje ya box. Hakuna tatizo lisilokuwa na suluhisho unless uamue kulikumbatia peke yako na kuendelea kufikiria kitatizotatizo badala ya kufikiri kisuluhishosuluhisho. Sorry, huenda ninasound very theoretical kwako lakini huo ndio ukweli mkuu.

mkuu nashukuru sana kwa maelezo mazuri, mimi ndio ninataka niingie kwenye hichi kilimo. Nitakushukuru sana ukinidadavulia vizuri gharama zake kwa ujumla ktk hizi heka mbili ili nijipange vzri nisije kuishia njiani!

ndio maana naipenda jf university collegge hapa unapata elimu bila cheti safi sana mm nipo znz lakini nataka kukimbia huku nihamie dar ili nilime haya matikiti maana huku znz yana soko balaa hasa kwenye mahotel ya kitalii.

Big up kwa hili darasa nimelipenda

napita tu...

asante neema, je umeishawahi kufanya hivi? Edmund anaruka mita 2 kwa kila shimo ila mbegu 2 kwenye shimo moja. Mie nadhani hii inakuwezesha kupita ukipulizia dawa nk. Labda useme mita 1 ila nusu? Tupe uzoefu wako kwenye hili

duka wapo 0712 661366
 
Wadau nina mbolea nzuri hisiyo na kemikali kwa yeyote mkulima anicheck tufanye kazi ni bei nzuri na ni costless kwa matumizi yako inafaa kwa matunda likiwemo tikiti maji,mbogamboga na nafaka na miti mbalimbali.kwa masiliwano 0652198319
 
Wadau nina mbolea nzuri hisiyo na kemikali kwa yeyote mkulima anicheck tufanye kazi ni bei nzuri na ni costless kwa matumizi yako inafaa kwa matunda likiwemo tikiti maji,mbogamboga na nafaka na miti mbalimbali.kwa masiliwano 0652198319

Uko wapi mkuu?
 
Back
Top Bottom