Kilimo cha Tangawizi - Masoko, Mbinu na Ushauri Toka kwa Wadau

Kilimo cha Tangawizi - Masoko, Mbinu na Ushauri Toka kwa Wadau

Kamefika kwenye kutoa mchanganuo wa mapato kakalala mbele! Naona article kaliyokuwa kame-copy na kupaste haina mchanganuo huo!

Na angemalizia faida na bei zake ingekuwa poa sana.
 
nataka kujua mauzo ya heka moja faida inakuwa ni sh ngapi
Hilo ni swali ambalo wengi wetu tunahitaji majibu. Mtoa mada hajaweza kuainisha mavuno yanakuwaje kwa hekari hapo ndipo tungeweza kukokotoa makadirio ya faida.
 
Hilo ni swali ambalo wengi wetu tunahitaji majibu,,,mtoa mada hajaweza kuainisha mavuno yanakuwaje kwa hekari hapo ndipo tungeweza kukokotoa makadirio ya faida
Maana wengine tuna taka tutoke kwa kilimo sasa bila kukaa chini na kuchambua vizuri inatupa wakati mgumu
 
Kwa uzoefu wangu kwa eka moja unahitaji si chini ya kg1,000 ya mbegu, afadhali kg 1,300. Na kama umelima vizuri na ardhi yako inakuwa nzuri na umepalilia ipasavyo unaweza kupata kati ka kg 6,000 mpaka 9,000 kawaida.

Ukiacha tena kwa ajili ya mbegu kg 1,300 utauza kg4,700 mpaka kg7,700 ya tangawizi mbichi sokoni. Ila mwaka wa kwanza ni majaribio unaweza kupata chini ya hayo sababu ya kukosa uzoefu wakati wa kupanda au kupalilia au mengineyo. Bei ya Kg moja ya mbegu inategemea lini unapojaribu kuinunua.

Kwa mfano mwaka jana tumenunua kwa Tsh800 kg moja, mwaka huu inawezekana bei ya kg ni tsh1,000 hapo Madaba. Faida ipo sana, lakini unahitaji muda wa kujifunza na pia kutafuta soko. Miaka mengine wanunuzi watakuja mpaka shamba lako mengine inabidi uwatafute sana.

Kwa ufupi mtaji wa kuanzia ni kubwa kidogo lakini faidha ni kubwa sana ukijitahidi kulima vizuri na kuitunza (shamba lako likiwa mbali na bila ulinzi wezi wanaweza kuja na kuiba tangawizi lako). Wengine wamelima eka nyingi na saizi wanakuwa na pesa ya kutosha.

Mimi binafsi silimi, analima mke wangu, lakini baada ya Miaka miwili tangu alipoanza anaweza kujenga nyumba nzuri kijijini na analeta pesa ya kutosha kwa familia Dar es Salaam.
 
Sidhani kama kuna uhalisia wa bei ya Tshs milioni mbili kwa ekari moja,mwaka mmoja uliopita. Nilijaribu kulima robo eka Mkoani Kilimanjaro, nilitumia debe mbili za mbegu ambazo hazikzidi hata laki moja. Labda utofauti wa maeneo huenda ukasababisha bei iwe tofauti lakini si kwa kiasi kikubwa hivyo.
 
Kwa uzoefu wangu kwa eka moja unahitaji si chini ya kg1,000 ya mbegu, afadhali kg 1,300. Na kama umelima vizuri na ardhi yako inakuwa nzuri na umepalilia ipasavyo unaweza kupata kati ka kg 6,000 mpaka 9,000 kawaida.

Ukiacha tena kwa ajili ya mbegu kg 1,300 utauza kg4,700 mpaka kg7,700 ya tangawizi mbichi sokoni. Ila mwaka wa kwanza ni majaribio unaweza kupata chini ya hayo sababu ya kukosa uzoefu wakati wa kupanda au kupalilia au mengineyo. Bei ya Kg moja ya mbegu inategemea lini unapojaribu kuinunua.

Kwa mfano mwaka jana tumenunua kwa Tsh800 kg moja, mwaka huu inawezekana bei ya kg ni tsh1,000 hapo Madaba. Faidha ipo sana, lakini unahitaji muda wa kujifunza na pia kutafuta soko. Miaka mengine wanunuzi watakuja mpaka shamba lako mengine inabidi uwatafute sana.

Kwa ufupi mtaji wa kuanzia ni kubwa kidogo lakini faidha ni kubwa sana ukijitahidi kulima vizuri na kuitunza (shamba lako likiwa mbali na bila ulinzi wezi wanaweza kuja na kuiba tangawizi lako). Wengine wamelima eka nyingi na saizi wanakuwa na pesa ya kutosha.

Mimi binafsi silimi, analima mke wangu, lakini baada ya Miaka miwili tangu alipoanza anaweza kujenga nyumba nzuri kijijini na analeta pesa ya kutosha kwa familia Dar es salaam.


Asante mkuu kwa ufafanuzi mzuri. Swali ni hivi je changamoto kubwa ya kilimo cha tangawizi ni nini hasa na katika kuuza na wewe una uza kwa kilo au debe au gunia.
 
Sidhani kama kuna uhalisia wa bei ya tshs milioni mbili kwa ekari moja,mwaka mmoja uliopita,nilijaribu kulima robo eka Mkoani Kilimanjaro,nilitumia debe mbili za mbegu ambazo hazikzidi hata laki moja. Labda utofauti wa maeneo huenda ukasababisha bei iwe tofauti lakini si kwa kiasi kikubwa hivyo......
Kama ni kilo 1000 na bei huwa ina range kwenye 800,1000, hadi 1300 sidhani kama inafika naona jamaa alipigia bei ya kawaida buku mbili.
 
Kwa uzoefu wangu kwa eka moja unahitaji si chini ya kg1,000 ya mbegu, afadhali kg 1,300. Na kama umelima vizuri na ardhi yako inakuwa nzuri na umepalilia ipasavyo unaweza kupata kati ka kg 6,000 mpaka 9,000 kawaida. Ukiacha tena kwa ajili ya mbegu kg 1,300 utauza kg4,700 mpaka kg7,700 ya tangawizi mbichi sokoni. Ila mwaka wa kwanza ni majaribio unaweza kupata chini ya hayo sababu ya kukosa uzoefu wakati wa kupanda au kupalilia au mengineyo. Bei ya Kg moja ya mbegu inategemea lini unapojaribu kuinunua. Kwa mfano mwaka jana tumenunua kwa Tsh800 kg moja, mwaka huu inawezekana bei ya kg ni tsh1,000 hapo Madaba. Faidha ipo sana, lakini unahitaji muda wa kujifunza na pia kutafuta soko. Miaka mengine wanunuzi watakuja mpaka shamba lako mengine inabidi uwatafute sana.

Kwa ufupi mtaji wa kuanzia ni kubwa kidogo lakini faidha ni kubwa sana ukijitahidi kulima vizuri na kuitunza (shamba lako likiwa mbali na bila ulinzi wezi wanaweza kuja na kuiba tangawizi lako). Wengine wamelima eka nyingi na saizi wanakuwa na pesa ya kutosha.

Mimi binafsi silimi, analima mke wangu, lakini baada ya Miaka miwili tangu alipoanza anaweza kujenga nyumba nzuri kijijini na analeta pesa ya kutosha kwa familia Dar es salaam.
Na kilimo cha tangawizi kina chukua mda gani hadi kutoka shambani?
 
Madaba (sijui sehemu nyingine) unaanza kuandaa shamba Oktoba na unapanda Novemba. Unaweza kuvuna June au unaweza kuiacha mpaka Oktoba Novemba mwaka ujao, inategemea bei unaoikuta June, kama ni bei ya chini sana kama mwaka jana afadhali uiache ardhini kwanza. Lakini hata kwa bei ya chini bado ungepata faida ukifanya hesabu. Ukiuza unauza kwa kilo. Wakati tangawizi lipo shambani inabidi upambane na kupalilia mara kadhaa walau mara mbili na afadhali mara tatu. Pia tangawizi haipendi Maji ya mvua ikae ardhini sana na majani yake mwanzoni hayapendi jua kali. Ni nzuri daima kushirikiana na bwana shamba wa eneo husika ili apime Ph ya ardhi na akuelekeze wapi ni pazuri kupanda na wapi usipande.
 
Kumbe kina chukua mda mi nikajua ni kama miezi 5 au 8 tu usha vuna
 
Kumbe kina chukua mda mi nikajua ni kama miezi 5 au 8 tu ushavuna
 
Kilimo chenye tija ni KILIMO cha samaki tu! Karibuni tulime samaki (Sato, Kambale n.k)
Hey, please tuchambulie kidogo hii kwa kweli, inavutia niliskia sehemu juu juu, tupe hadi ghrama za kujenga bwawa.
 
Mbegu; 1000kg*5000= 5,000,000/= hizo ni mbegu tu kwa heka moja

Kukodisha Shamba lake sh...?

Kulima Heka 1 sh...?

Mbolea sh ngapi....?

Heka 1 Kupalilia sh...?

Heka 1 kuvuna sh.....?

Ni mikoa gani inasitwi

Je aina hipi ya mbegu ni nzuri...?

Mtoa mada mnisaidie hapo na ingekuwa vizuri utupie namba yako ya simu.

Call me if possible whatsup 0784584871

Salamu,
Kuna vitu vingine sio vya kuuliza,kwa maswali yako wala usijaribu kulima,
"
Kukodisha Shamba lake sh...?

Kulima Heka 1 sh...?

Mbolea sh ngapi....?

Heka 1 Kupalilia sh...?

Heka 1 kuvuna sh....?

Ni mikoa gani inasitwi",
Kwanza kabisa jua Hekta moja ni ekari kiasi gani, hakuna mkulima mtaongea kwa hekta, kila mmoja ataongelea ekari,
Shamba katufute utakapo pata uta negotiate bei ya kukodi, kulima shamba bei ni moja Tanzania nzima kwa jembe la kwanza na la pili, nenda shambani utakapo pata utajua kutokana na umbali trekta zinapopatokana, Kuvuna ni wewe kutafuta wavunaji, kila sehemu inategemea, ingia shambani fanya research mwenyewe.

Kupalilia bei ni standard Tanzania nzima, nenda shambani utajua na sio whatsapp, Mbolea bei ni moja Tanzania nzima, pata shamba utajua gharama za kufikisha shambani toka uliponunua, utapata gharama halisi.

Nakushauri usiingie, kilimo kinataka utayari na ku-focus kwenye challenge na sio mauzo.

Karibu.
 
Nataka kujua mauzo ya heka moja faida inakuwa ni sh ngapi
Elewa kilicho andikwa ndo upate cha kuuliza, sio kuuliza tuu ili mradi, mana wote maswali yenu yapo kwenye maelezo, hesabu ndogo tuu ya kuzidisha, kujumlisha na kutoa, na sio mi maswaaali na kutujazia SERVER.
 
Tafadhalini wadau naomba kupata maelezo juu ya kilimo cha tangawizi kwa vipengele vifuatavyo:-
1/ Maeneo yanakolimwa hapa Tanzania. 2/ Muda wa kulima hadi kuvunwa 3/ Soko lake likoje hapa nchini
 
Back
Top Bottom