Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

ulifikia wapi mkuu na tafiti yako?
 
wakuu hv soko la kitunguu swaumu na kitunguu maji.kipi kinasoko
 
Pole kwa yaliyokukuta. Bado unaendelea na kilimo cha vitunguu?
 
Natamani sana nianze kilimo cha vitunguu maji,nahitaji msaada wa watu wanaolima vitunguu maji maeneo ya Mto RUVU ( nimesikia kuna watu wanalima Ruvu) au kama kuna watu wanaolima kitunguu maeneo ya Kilwa Masoko sehemu iitwayo Makangaga.

Kama kuna mtu analima katika haya maeneo naomba tuwasiliane pia ningependa nifahamu kuhusu Masoko
 
Hivi wadau kuna mbegu ya red Bombay huuzwa kwa lita 20, 200000? Me nilipata dukani gram 250,30000 ila kuna mshikaji wangu akaniambia Singida huwa zinapatikana 200000 kwa lita 20, mwenye kujua anijulishe tafadhali
Mkuu zile mbegu huwa mavuno yake siyo mazuri sana.....chukua hiyo ya dukan uwezekano wa kuota ni 90%
 
Ahsante mkuu kwa mrejesho. mimi ndio nataka kuanza. nilishangaa sana eti mbegu lita 20 kwa ekari. kwanza mbegu kipimo ni kilo sio lita mbegu za vitunguu sio maji
 

Kwa mwangaza zaidi jaribu kutembelea
 
Mkuu Malila naomba na mini nisiwe mchoyo wa kutoa shukrani zangu!

Kwa kweli nimekuwa nafurahia sana mchango wako.....na umekuwa muwazi sana.....na hivi ndo wajasiriamali wa Tanzania tunatakiwa tuwe! big up saaaanaaaaa!!!
 
Kaka naomba uni pm unipe gharama kwa kila hekari kwa maeneo husika
 
Kilimo cha kitunguu

- Andaa shamba lako tayari Kwa upandaji

- Ikiwezekana Pima udongo wako kujua pH yake

- Kitunguu hustawi vizuri kwenye hali yenye ubaridi na Kisha baadae huhitaji jua Kwa ajili ya kukauka. Hii ni kukupa muongozo ni kipindi gani uanze kupanda kutokana na mkoa na pindi za mvua

- panda mbegu yako kwenye kitalu wiki 10 hadi 12 kabla hujahamishia shamani
- Andaa matuta yako Kwa ajili ya kuhamishia miche shambani

- Kawaida wakulima wengi hupanda miche 75,0000 hadi 120,000 ya kitunguu kwenye tuta moja ndani ya eka 1 ikiachiana nafasi ya inchi 2 na inchi 24 kati ya tuta na tuta kulingana na aina ya kitunguu

- Tumia mbolea kama NPK

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa kutumia namba zetu za simu au barua pepe info@kilimojoint.co.tz usisahau pia kutufuatilia kwenye Instagram au facebook page yetu KilimoJoint
 
Kwangu ni habari njema hii napenda sana kilimo ila msimamizi ameniangusha sana najipanga najua wapi nilikosea
 
Hivi hivi vitunguu vinaweza kustawi maeneo ya bagamoyo?
 
Kilimo cha Kitunguu
Kilimo cha mhindi/hindi
Uuzaji wa yai
Kilimo cha harage
 
Asante kwa taaruma sasa, nahitaji kifaa cha kupimia udongo je, nitakipata wapi na ni shilingi ngapi?
 

VIJANA wasomi wanaounda Taasisi ya Maendeleo ya Vijana Tanzania (TAYODA) wameeleza mafanikio wanayopata baada ya kuamua kujikita katika kilimo cha vitunguu tangu mwaka 2013, muda mfupi baada ya kumaliza elimu yao ya vyuo vikuu.

Vijana hao wanaomiliki shamba lenye ukubwa wa heka 300 katika kijiji cha Idodoma wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma, wamewataka vijana wanaolalamika kukosa ajira, kuunga mkono kauli ya hivikaribuni ya Rais Dk John Magufuli inayowataka wafanye kazi badala ya kucheza pool toka asubuhi.

Akizungumza na wanahabari waliotembelea shamba lao hilo hivikaribuni, Mkurugenzi wa TAYODA, Jackson Kangoye alisema; “taasisi imefanikiwa kukuza mitaji ya vijana walioko mitaani kwa kupitia sekta hii ya kilimo.”

Alisema mwaka 2013 walipoanza na vijana 25 walifanikiwa kulima zao hilo katika shamba lenye ukubwa wa heka 30, wakaendelea kupata mafanikio yaliyowazesha kupata shamba lenye ukubwa wa heka 300 huku idadi ya vijana wanaojishughulisha na kilimo hicho ikiongezeka hadi 230 mwaka huu.

“Lengo letu katika kipindi cha miaka mitatu ni kuwaingiza katika shughuli hii vijana 2500 walioko mitaani bila kujali viwango vya elimu,” alisema.

Kangoye alisema wakiwa shambani vijana hao ugawanywa katika makundi ya watu watano ambapo kila kundi hupewa heka tano kwa msimu mmoja na kuzitumia kupata mitaji.

“Tangu tuanze kilimo hiki uzoefu wetu unaonesha kwa kila heka moja, tunazalisha kati ya gunia 80 na 120 za zao hilo ambalo uuzwa kwa kati ya Sh 120,000 na Sh 170,000 ambazo ni sawa na wastani wa Sh Milioni 10 na Sh Milioni 20 kwa heka,” alisema.

Alisema kiasi kinachobaki baada ya kutoa asilimia 25 ya pato lote linalokwenda katika taasisi hiyo kwa ajili ya kusaidia vijana wengine na gharama zote za matumizi, hutolewa kwa vijana hao kama mtaji wanaoweza kuutumia kujiendeleza katika kilimo hicho katika mashamba yao wenyewe.

Kangoye alisema zaidi ya vijana 120 wamekwishanufaika kiuchumi kupitia mpango huo kwa kuanzisha miradi yao ya kilimo cha vitunguu, pilipili, tikiti na nyanya.

Source: Kijana msomi, J. Kayonge aeleza wanavyofanikiwa katika kilimo cha vitunguu - wavuti
 
Mmoja wa vijana aliyenufaika na mpango huo, Kassara Mageni alisema; “baada ya kumaliza Chuo Kikuu cha Dodoma mwaka 2012, sikutaka kubweteka kusubiri kuajiriwa. Nimehamia shamba, nalima na ninawasimamia vijana wenzangu kupitia taasisi hii ya TAYODA kujiletea maendeleo.”

Mbali na kujipatia mapato makubwa kutoka katika mashamba anayolima, alisema mpango wake ni kuhamishia maisha yake moja kwa moja katika kijiji hicho.

“Wasomi wengi tuna ndoto ya kupata mafanikio ya haraka tena kupitia kazi za kuajiriwa, bahati mbaya wengi wetu tunachelewa kufikia ndoto hiyo, niwajulishe wasomi wenzangu maisha yako huku, sekta ya kilimo ina fursa kubwa inayoweza kubadili maisha yetu vijijini na mijini,” alisema.

Kwa upande wake kijana mwingine, Gapi Yohana alisema kwa miaka miwili ambayo amefanya kazi na taasisi hiyo ameweza kuongeza ukubwa wa shamba lake kutoka heka moja hadi tano pamoja na kujiimarisha kiuchumi ikiwa ni pamoja na kununua pikipiki pamoja na kiwanja anachotarajia kukitumia kujenga nyumba yake ya kisasa.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…