Kilemachocho
JF-Expert Member
- Feb 19, 2016
- 560
- 365
Mkuu itakuhitaji kuwa na mtaji kiasi gani ili uweze kulimaa heka 2Mkuu byakuzana huu ndio muda muafaka kwa kilimo cha kitunguu binafsi Niko kwenye maandalizi mbegu iko tayari kitunguu cha mwezi huu kawaida kinatoka mwakani mwezi Wa kwanza majira hayo sokoni hakuna kitunguu bei iko juu kikitoka vizuri lazima ucheke Mkuu zingatia matunzo dawa Na mbolea
Mwaka huu kitunguu kimelimwa hasa nahisi kutakua na poromoko kubwa la bei hasa ikifika masika maana limelimwa isivo kawaida,me nalimia iringa ruaha mbuyuniMwenye kuwa na majibu yanayobainisha juu ya huu mda kulima kitunguu tunaomba aje atueleze. Ila kwa mimi hofu kubwa ni kukutwa na mvua kikaharibiwa na maji ya mvua maana ukisia mbegu saiv September kutoka ni kwenye January, February.
Pia kuhusu soko. Naona kitunguu kimelimwa kila kona ya nchi, hapo sasa cjui itakuwaje, yaweza kuja kuporomoka bei. But, by the way ni kujipa moyo na kufanyia kazi changamoto ambazo unauwezo wa kuzikabiri.
Mwaha huu hata dec sidhani kma bei itakua nzuri kitunguu kimelimwa sana hasa huku iringa na bado watu wanaandaa vitalu kwa upande wa bei now n elfu 55 kwa hapa ruaha mbuyuniInategemea na soko! Hio elfu 40 ni wapi? Sema hata hivo kipindi iki vitunguu hua vingi sokoni.. Target soko la dec..ingawa si kazi rahisi
Mwaka huu sidhani kama mambo yatakua the same lets wait n see maan huku limelimwa sana tofaut na miaka yote nna uzoefu wa miak 4 na hili zao sijawahi kutana na hali hiiMkuu byakuzana huu ndio muda muafaka kwa kilimo cha kitunguu binafsi Niko kwenye maandalizi mbegu iko tayari kitunguu cha mwezi huu kawaida kinatoka mwakani mwezi Wa kwanza majira hayo sokoni hakuna kitunguu bei iko juu kikitoka vizuri lazima ucheke Mkuu zingatia matunzo dawa Na mbolea
Mambo ya muhimu(chakula basic) hakiathiriwi na mzunguko wa fedha.Hii ni necessary good sio luxury kama bia au kitimoto.Kwanza mzunguko wa fedha hauko vizuri na kiukwelibna sikia kwa sasa Kidete ni elfe 50
Tuwasiliane 0763370175Mwanza mkuu
Umenene nami mbegu ya red creole naielewa sana ipo poa na nimeweka shambanilipokuwa TZnimewah lima na kunitoa saana maeneo ya sanawali ya juuu. cha muhim cheza na soko pia tafta mbegu nzurikama RED CREOLE F1 japo ina gharama ila mbegu hii inazaa saana na pia inavumilia saana magonjwa na ukame. fanya ufanyavyo ila jitahid mwez wa tatu au wa nne uwe umepeleka kitunguu sokoni hapo utapiga hela mwana waneee balaa.
ila kinachangamoto saana aisee saana saana, ndio maana na recommend hyo mbegu kwa wale beginners. all the best.
kumbuka usi focus kweny nini utapata ila i tune akili yaako i focus kwenye changamoto za HYO KITU ni boraa kabala ya kuanza ukamtafta mtaalamu akakusaidia na akakueleza changamoto kwaanza kabla hajakueleza mafanikio.
Hapo inategemea na mbegu gani atatumia ila kwa mbegu bora ni m3 kwa ekaKitunguu heka 2million ukisimamia mwenyewe karibu kwa kujifunza zaidi 0763370175
Niko Arusha nafahamu sana kwa huku ,msimu huu huwa kinacholipa ni vitunguu,hoho zinazotoka from Decemberingefaa tumpate mtallaam wa mambo ya kilimo hapa hatusaidie kuhusu msimu wa kuanza kulima zao lolote na
atuelezee namna ya kilimo kilivyo itakuwa vyema zaidi maan wengi hata mm nataka kulima na nimeshaanza kuilima
ruvu jkt nalima bamia je kwa kipindi hiki cha mweizi huu September inini kinatakiwa kulimwa zaidi
Acre 10 sio kitu kidogo ila ukikifanya vizuri kitakulipa sana ,kwa ushauri wangu lima kitunguu this season sababu unaposhana na wa Singida wale ndio wanalima kutegemea mvua hata elf 30 gunia kwake faida ,lima msimu huu uvune by February gunia huwa hadi laki 2,ila tafuta mtaalam wa kilimo huko unakolima akusimamie na uwe na vibarua u will see the results usifanye majaribio kwa eka kumi bali fanya production ya eka kumi ,kufanikiwa usilime kimazoea vyema ukimpata horticulturist kabisa kila mkoa wapo though huwa sio wengi ila ukiangalia upande wa ngo's na makampuni ya mboga huwa wapo wengi tu na wana experience ya mazao ya mbogaWakuu, mimi nipo interest sana kwenye kujaribu hii kitu kwa mid scale, yaani acre 10 na kuendelea. Naombeni mwenye ujuzi wa juu anipe namba nizungumze nae.
Kwangu mimi masoko sioni kama tatizo. Naona tatizo ni unknown nyingi shambani.
Ukitumia neptune mbegu kg 1.5 ni tsh 555,000/=Mkuu horticulturist fafanua hiyo milioni tatu kwa kirefu kidogo...Tujue bei ya mbole na inahitajika kiasi gani kulima shamba nk
Ahsante mbegu yenye kutoa mazao yanayokubarika sokoni la ndani na la njeUkitumia neptune mbegu kg 1.5 ni tsh 555,000/=
Kukodi shamba=
Kulima trecta=
Kuandaa kitalu sqm 500=
Kuandaa matuta ya kusia=
Kunyesha ya kwanza=
Kusia=
Kutafuta na kutandika matandizo=
kunyesha kitalu mara 20(mafuta,kibarua etc)=
Kitalu mbolea can kg 1,seedling starter 1=
Dawa ya ukungu 0.5kg na ya wadudu(thrips and red spider)=
Kibarua kitaluni=
Kupiga harrow shamba au kulima na ng'ombe=
Kunyesha ya kwanza na kuandaa matuta=
Kusia shamb eka vibarua=
Mbolea dap kg90 ya eka=
Kunyesha shamba mara 2 kwa wiki kwa mwezi mmoja kisha mara moja kwa mwezi kwa miez 3=
Palizi mbili =
Mbolea shambani urea/can kg 90,yara winner kg 90=
Dawa ukungu kg 1(ivory 72/rido/ebony 72 etc,blue copper),wadudu thrips,red spider,caterpillar(evisect,dynamec,belt)=
Kibarua kupiga dawa=
Kuvuna vibarua=
Hizo general gharama jaza amount kwa uliko uone unapata kiasi gani ,hapo ya kwako au msimamizi nnje ya budget