Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Ndio kuna bwawa lina maji mengi tu karibu na shamba. Je una interest ya kulima na wewe?

Na mimi nina interest ya kulima vitunguu lakini napata info nusu nusu.

Hata sijajua nitalima wapi maana naogopa ikiwa mbali sana nitashindwa kufuatilia kwa karibu kwakuwa nipo nyumbani sunday tu!
 
Nasikitika umri ulikuwa mdogo sikuwa najua jf hapo nyuma!

Naomba kuuliza kwa maeneo ya songea(katikati ya njombe na songea) pana kubali hiki kilimo ukiwa na mashine yako ya umwagiliaji?

Nafurahi sana kuwa na wazee wa jf.
 
Wakuu naombeni mnipatie uzoefu wenu katika kilimo cha vitunguu ruaha mbuyuni, jmosi natarajia kwenda ruaha kutafuta shamba eli ni jaribu hichi kilimo cha vitunguu, kwa yoyote aliyenauzoefu kwenye kilimo hichi naomba mchango wake.
 
Wakuu naombeni mnipatie uzoefu wenu katika kilimo cha vitunguu ruaha mbuyuni, jmosi natarajia kwenda ruaha kutafuta shamba eli ni jaribu hichi kilimo cha vitunguu, kwa yoyote aliyenauzoefu kwenye kilimo hichi naomba mchango wake.

Kama unakwenda kukodi shamba sawa, mashamba ya kununua bei iko juu vibaya, je kuna mtu unayemfahamu pale wa kukusaidia? Kama huna sema nikupe mtu akusaidie na yy ana shamba pale.
 
Nasikitika umri ulikuwa mdogo sikuwa najua jf hapo nyuma!
Naomba kuuliza kwa maeneo ya songea(katikati ya njombe na songea) pana kubali hiki kilimo ukiwa na mashine yako ya umwagiliaji???
Nafurahi sana kuwa na wazee wa jf.

Vijiji gani pale, Je ni Lilombwi, Ifinga, Wino au Liwengi? Udongo unatofautiana sana kutoka Kifanya mpaka Lilondo.
 
Asante ndugu yangu.

Kama uko DSM niambie ili siku nikifika dar nikutafute, leo niko nje ya dar. Unaweza kushiriki vikao vyetu bila taabu. Hakuna kiingilio na hatumfichi mtu kitu tunachofanya. Tunajadili namna ya kushiriki uchumi wa nchi yetu na sio kuwa watazamaji.
ningependa kushiriki pia namba yng 0717410406 nichek pls
 
Jaman natka kushiri kikao namba yng 0717410406 mie sio mtu wa mtandao sana so nichek kwenye simu direct bip tu

Kweli ww sio mtu wa mtandao, post tano tu !!!!! Nitakubip kama ulivyosema kwa line ya airtel jioni hii.
 
Jaman nina shamba eneo la kitonga mbele kidogo ya chamanzi dar es salaam nauliza eneo hilo na hali ya hewa ya joto ya dar vitunguu swaum vinakubali? Wenye ujuzi na uzoefu naombeni msaada wenu wa mawazo.

asanteni kwa ushauri, natanguliza shukrani
 
Naona jamaa wamechunia kabisa hii thread.......kwanini usiende kilimo kuuliza,au umeshajaribu kutafuta online namna ya kukuza za hili?......it will give you a lot of info!
 
Wadau naomba kujuzwa juu ya upatikanaji wa mbegu za bora vitunguu mkoani Morogoro
 
mkuu vitunguu saumu haviwezi kulimika dar kwa sababu ya joto kali na ardhi ya kichanga.Lima matikiti,mihogo au nanasi.
Huo ni ushauri wangu tuu.
 
Thanx kwa ushauri nimewaelewa wakuu,pm zimekua nyingi wanataka kukodi na kununua as if nimesema naliuza
 
Sikiliza Dangote hebu usikatishwe tamaa sijui umesha surrender tayari, ujue wengine ndiyo tunaona thread yako hapa si unajua ndiyo bado hatujasettle humu JF macho ya ugeni bado tunashangaa shangaa!

Ni hivi Dangote, humu humu jamvini kuna watu wameshasema kuwa kule Ruvu wanastawisha sana vitunguu!! Mbona naona ni ukanda huu huu wa pwani kwenye joto hili hili la Dar?

Tatizo mimi sifahamu location ya Chamazi! Nikwambie ndugu yangu, watu tunapoongea hatuongei kitaalamu, tunasema sehemu fulani ina joto sana haifai kwa hiki au kile lakini hatusemi joto kiasi gani? Na ni majira gani? Utakubaliana nami kuwa kunamajira hata ukanda wa pwani huwa kuna baridi! Uongo?

Sasa nikuleze kuwa hata Kilosa ambako kuna joto sana majira ya joto kitunguu swaumu kinalimwa sana lakini kinalimwa majira ya baridi kuanzia mwezi wa nne hadi mwezi wa nane watu wanaanza kuvuna safi kabisa!

Kwa hiyo ninachokushauri kwa vile nchi yetu haina utafiti wa kutosha uliofanyika kila eneo kujua kuwa linafaa kwa zao gani au halifai kwa zao gani na pia kwa kuwa unashauku sana kulima kitunguu na kwa kuwa shamba ni lako lima kitunguu swaumu hapo Chamazi majira ya baridi! Ukanda wa pwani wote ninaimani joto hushuka sana kuanzia mwezi wa nne pia!

Tafuta aina mbili au tatu tofauti za vitunguu swaumu ili uweze kujua aina gani itakubaliana na mazingira hayo! Jambo moja ukae ukijua kuwa kila mahali penye zao linalostawi kuna mtu alijaribu kwanza likastawi ndiyo wengi wakafuata. Hakika nakuhakikishia utaweza kupata matokeo ya kushangaza na kukusisimua sana kwa sababu ninauhakika utafiti wa mboga mboga tanzania ni kama hakuna kabisa wamekaa wanategemea takwimu za kiujumla jumla tu kwamba Pwani kuna joto ilihali kuna majira Kisarawe huwa kunabaridi kama uko bara kabisa!

Kwa hili nakutia moyo na kama unamaswali mengine uliza tu, ila tafadhari matokeo yote utakayopata leta tumwagie hapa hapa kama wakubwa wetu Malila, El nino n.k. walivyotuonyesha njia!

Samahani kwa maelezo marefu namimi nami sinaga dogo mweeeee!!
Heshima sana kwa MALILA na EL Nino you are my Heros and the reason to be here!
 
Morogoro vitunguu bora vinapatikana kwenye maduka mengi sanaaa ya pembejeo mjini Morogoro. Hizo ni mbegu bora kwa vile ni officially certified. Mbegu hizi zinadosari kubwa mbili, kwanza huwa ghari sana kwa mtu anaetaka kulima eneo kubwa kibiashara mfano ekari moja na kwenda juu. Kwa hiyo gharama ya mbegu huwa kubwa ingawa kwa kweli huwa mara nyingi ni mbegu halisi!

Tatizo la pili ni jinsi hali ya hewa ilivyoharibika Kitaifa kwamba kila biashara sasa kuna kitu-FEKI! Unanunua mbegu kwa bei mbaya inamhuri unaosomeka kabisa kuwa mbegu hiyo imekuwa packed January na wewe unainunua April unaisia inagoma kuota kabisa! Unahofia labda nimesia vibaya, unanunua nyingine tena matokeo yale yale haioti!

Mfano iliwahi kunitokea mimi mwaka mmoja nilinunua mbegu ya Pilipili Hoho za kampuni maarufu ya Holand! Muhuri ulionyesha ni mbegu mpya kabisa ya hoho lakini haikuota!! Nimekuwa nikipata mbegu ya uhakika toka kampuni ya Mkulima Seeds hizo ndiyo zilikuwa zikiota, lakini tena tatizo likaja Mbegu za Mkulima seeds nazo ni mchanganyinko, hoho zingine zilikuwa ndefu sana na nyeupe (matunda)!

Pia kuna Nyanya aina ya Tanya naijua vema tabia yake na tunda linavyokuwa, niliwahi kununua mbegu aina hiyo ya nyanya zinazozalishwa na East Africa Seed company zilipoanza kuiva ilikuwa ni uchafu tu hata wateja walisusia kununua! Ilikuwa ni mchanganyiko wa mbegu usioeleweka! Kwa ukweli usiamini mbegu yoyote eti mradi iko kwenye Kopo au pact yenye lebo nzuri ni wizi wizi tu! Mkakati wangu kwa hili ni kuzalisha mbegu mwenyewe watu hawaaminiki!

Sehemu ya pili ya kupata mbegu Morogoro ni mbegu zinazozalishwa na wakulima. Morogoro kuna eneo maarufu kwa kilimo cha vitunguu linaitwa Lumuma, wilaya ya Kilosa huko kunawazalishaji wengi sana wa mbegu za vitunguu waliopata mafunzo rasmi ya uzalishaji bora wa mbegu za vitunguu.

Mbegu za vitunguu toka kwa wakulima huuzwa kwa kupimwa kwa ujazo wa lita. Kutegemea mwaka lita huanzia sh 15,000/- hadi 30,000/- mwaka 2010 ilifikia bei ya lita moja 50,000/-! Mbegu huvunwa mwezi wa 10 huu ni muda mzuri kununua baada ya hapo bei hupanda juu. Mkulima anaetaka kulima eneo kubwa mbegu hii ndiyo inamfaa maana ni nafuu kuliko za kwenye makopo.

Tatizo kubwa la mbegu za wakulima nalo ni ulaghai! Kwa kuitazama mbegu huwezi jua kama ni mbegu aina unayoitaka, wengi huwa wanadanganya ukijapanda baadae unabaki kulia kuwa umetapeliwa! Inabidi pia uwe unajua kuzipima kama zinaota au la, wenyeji wananjia mbalimbali wengine wanatumia maji wengine moto! Kitaalamu ni budi kuotesha sample kwanza kisha angalia uotaji wake kisha ukiridhika nunua kwa wingi kutoka kwa mkulima husika.

Tatizo lingine kwenye mbegu za wakulima za vitunguu ni hili: kwa kawaida vitunguu vinatabia msimu wa kwanza havitakiwi vitoe mabomba ya maua bali vitoe vitunguu tu, msimu wa pili unapopandikiza kitunguu-mama ndiyo hutakiwa kitoe bomba, maua na hatimae mbegu. Sasa kwa wakulima laghai inapotokea kitunguu kikatoa mbegu isivyotarajiwa ule msimu wa kwanza huzivuna hizo mbegu na kuziuza!

Ukinunua mbegu kama hizo matokeo yake ni kujikuta vitunguu asilimia kubwa shambani vimetoa mabomba ya maua! Na hii ni hasara kwani vitunguu vyako hukosa ubora sokoni yaani ni msiba kwako!

Ili kuepuka hili unatakiwa uwahi kwa mkulima mzalishaji wa mbegu ukaone vitunguu vyake vikiwa bado shambani mwezi mmoja au miwili kabla hajavuna ili ujiridhishe kwamba ni aina halisi ya vitunguu unayotaka ili akivuna ununue kitu halisi.

Vinginevyo tumia wakulima waaminifu ambao akikuambia ni red ni red kweli akisema khaki ni khaki kweli! Msimu wa mwisho nilimwamini kijana mmoja alikuwa akileta mbegu toka Singida, kumbe kule Singida alikuwa akizoa hizo mbegu nilizoeleza hapo juu, wanazoa zoa mashambani tu, matokeo yake nikaanza kuona vinajitokeza vitunguu vyeupe na vyekundu, baadae shamba zima lilichanua utadhani nimelima vitunguu vya mbegu!!

Kuwa mwangalifu utakapokuwa unatafuta mbegu!

Niwie radhi jamani maelezo yangu marefu saa zingine namimi nae mweeee!
 
Mkuu mimi nalima Kigonga maeneo hayo kupita kidogo kwa Mboma upande wa kushoto. Kimsingi vitunguu swaumu vinakubali lakini lazima kujua muda upi uweke dawa ipi na wadudu gani wanashambulia wakati gani. Mimi niliandaa water melon (matikiti maji) lakini mfanyakazi hakuya-treat vizuri yakawa yanapasuka kabla ya kukomaa! Ilinikatisha tamaa sana!
 
Sikiliza Dangote hebu usikatishwe tamaa sijui umesha surrender tayari, ujue wengine ndiyo tunaona thread yako hapa si unajua ndiyo bado hatujasettle humu JF macho ya ugeni bado tunashangaa shangaa!

Ni hivi Dangote, humu humu jamvini kuna watu wameshasema kuwa kule Ruvu wanastawisha sana vitunguu!! Mbona naona ni ukanda huu huu wa pwani kwenye joto hili hili la Dar? Tatizo mimi sifahamu location ya Chamazi! Nikwambie ndugu yangu, watu tunapoongea hatuongei kitaalamu, tunasema sehemu fulani ina joto sana haifai kwa hiki au kile lakini hatusemi joto kiasi gani? Na ni majira gani? Utakubaliana nami kuwa kunamajira hata ukanda wa pwani huwa kuna baridi! Uongo? Sasa nikuleze kuwa hata Kilosa ambako kuna joto sana majira ya joto kitunguu swaumu kinalimwa sana lakini kinalimwa majira ya baridi kuanzia mwezi wa nne hadi mwezi wa nane watu wanaanza kuvuna safi kabisa!

Kwa hiyo ninachokushauri kwa vile nchi yetu haina utafiti wa kutosha uliofanyika kila eneo kujua kuwa linafaa kwa zao gani au halifai kwa zao gani na pia kwa kuwa unashauku sana kulima kitunguu na kwa kuwa shamba ni lako lima kitunguu swaumu hapo Chamazi majira ya baridi! Ukanda wa pwani wote ninaimani joto hushuka sana kuanzia mwezi wa nne pia! Tafuta aina mbili au tatu tofauti za vitunguu swaumu ili uweze kujua aina gani itakubaliana na mazingira hayo! Jambo moja ukae ukijua kuwa kila mahali penye zao linalostawi kuna mtu alijaribu kwanza likastawi ndiyo wengi wakafuata. Hakika nakuhakikishia utaweza kupata matokeo ya kushangaza na kukusisimua sana kwa sababu ninauhakika utafiti wa mboga mboga tanzania ni kama hakuna kabisa wamekaa wanategemea takwimu za kiujumla jumla tu kwamba Pwani kuna joto ilihali kuna majira Kisarawe huwa kunabaridi kama uko bara kabisa!! Kwa hili nakutia moyo na kama unamaswali mengine uliza tu, ila tafadhari matokeo yote utakayopata leta tumwagie hapa hapa kama wakubwa wetu Malila, El nino n.k. walivyotuonyesha njia!

Samahani kwa maelezo marefu namimi nami sinaga dogo mweeeee!!
Heshima sana kwa MALILA na EL Nino you are my Heros and the reason to be here!

Kweli, ni vizuri ajaribu mwenyewe,
Nilikuwa nadhani vitunguu maji haviwezi kuota na kuzaa vizuri huku Mkuranga. Ni mpaka nilipoona kwa macho ndio nikaondoa wasiwasi, vitunguu jamii ya Red Indian vinazaa vizuri. Niliona miche ya nyanya aina ya Roma pale Shungubweni Mkuranga imezaa sana kama Ilula Iringa.

Nenda ujaribu kisha rudisha mrejesho hapa jamvini.
 
Jaman nina shamba eneo la kitonga mbele kidogo ya chamanzi dar es salaam nauliza eneo hilo na hali ya hewa ya joto ya dar vitunguu swaum vinakubali? Wenye ujuzi na uzoefu naombeni msaada wenu wa mawazo.

asanteni kwa ushauri, natanguliza shukrani

Mkuu sidhani kama unataka kulimia jembe la mkono, na obviously utakuwa umejipanga kidogo kifedha, as long as una eneo, suala la udongo ni suala dogo sana.

Chukua sample ya udongo uende nao kwa wataalam wa kilimo waupime kwanza, siku hizi kuna kilimo cha kisasa (drip irrigation, protected sunlight, artificial soil etc...)

Ukiwa na pesa kidogo na uwezekano wa kupata maji karibu unaweza kulima chochote popote hapa Dar
 
Mkuu mimi nalima Kigonga maeneo hayo kupita kidogo kwa Mboma upande wa kushoto. Kimsingi vitunguu swaumu vinakubali lakini lazima kujua muda upi uweke dawa ipi na wadudu gani wanashambulia wakati gani. Mimi niliandaa water melon (matikiti maji) lakini mfanyakazi hakuya-treat vizuri yakawa yanapasuka kabla ya kukomaa! Ilinikatisha tamaa sana!

Watermelon kupoasuka kabla ya kukomaa, nadhani umelima kipindi cha mvua au maji yalikuwa mengi sana?
 
KIbanga nashukuru. Nilimbiwa mbolea ya kuku iliwekwa nyingi (sina hakika), mara maji yalimwagiliwa mengi -ilikuwa wakati wa jua kali, lakini yalipasuka yakingali na size ndogo! mara
Watermelon kupoasuka kabla ya kukomaa, nadhani umelima kipindi cha mvua au maji yalikuwa mengi sana?
 
Back
Top Bottom