Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Asante sana na mimi nimeipenda , ngoja nijipange nitakutafuta nimechoka kuajiriwa kwa kweli.
 
Nimeipenda, nipo mwanza natamani kufanya hivyo, mkuu maelezo tafadhali au nikupigie unipe maelekezo?
 
Kwanza kabisa napenda kuchukua nafasi hii kuomba radhi kutokana na mtu niliyemuachia maagizo ya kuweka bandiko hili hakutoa ufafanuzi mzuri.

Ufafanuzi huu ntautoa kwa kifupi hapa na ntaambatanisha na excel ambayo ina mchanganuo mzuri zaidi.
Mbegu hii imeandaliwa kisasa na inazalishwa nchini kenya, nimeitumia huu ni mwaka wa nne na sijawahi kukatishwa tamaa na mbegu hii.

Kwa kawaida hutumia lita 10 hadi 15 kwa eneo la ekari moja.

Suala la bei sokoni kwanza kabisa inatokana na ubora wa kitunguu na pia timing ya mavuno yako. Kwa mfano, mimi nalima Kidete na Bagamoyo. Kidete huwa napanda mwezi wa tatu katikati na nakuja kuvuna mwezi wa saba kwenye tarehe 10 na huwa nakutana na bei ya 110,000 hadi 95,000 na kwa bagamoyo nimepanda mwezi huu mwanzo na nategemea kuvuna mwezi wa tatu ambapo bei ya vitunguu huwa juu sana kwasababu shamban tu gunia hufikia hadi 120,000/=

Naomba nieleweke kwamba haya yote nnayoongea sio kwamba navutia biashara ya mbegu ila ni kitu halisi na mtu yoyote anaweza kufika ofisini na nikamuonyesha risiti za mauzo ya sokoni. Kwa fukara kama mimi anayetafuta kujiajiri hii ni nafasi nzuri na tutasaidiana kwa utaalamu bila malipo yoyote.

NB: Naomba muangalie excel niyoiambatanisha hapo chini nimejaribu kutoa mchanganuo wa gharama kamili ya kilimo kwa shamba la ekari moja na mchanganuo kama ukiamua wewe mwenyewe kuleta mzigo mjini na faida ya biashara nzima ndani ya miezi mitatu.

Kama kuna sehemu ntakua nimesahau kutoa maelezo basi tusameheane na ntashukuru ukinitafuta tukaongea zaidi kulikoni kutoa maneno machafu na ya kejeli mtandaoni.

Ahsanteni sana
namba yangu no 0655003510

Mkuu Bagamoyo unalimia maeneo gani? Nina shamba langu Fukayosi sijuwi kama kunafaa kulima vitunguu huko.
 
Nna ushahidi wa risiti tokea nimeanza biashara hii miaka minne iliyopita, kama nna gunia nimewahi kuuza chini ya elfu 85 nafuta tangazo hili. Cha zaidi mtu halazimishwi kuchukua opportunity, ni maamuzi binafsi kaka. Next time "Think before you act" Mr

Mkuu ulishawahi kuvuna mwezi wa 9 au wa 10 bei zake zikoje? Maana naona ndo sehemu nyingi wanalima na kuvuna muda huo.
 
Mkuu ulishawahi kuvuna mwezi wa 9 au wa 10 bei zake zikoje? Maana naona ndo sehemu nyingi wanalima na kuvuna muda huo.

Salama mkuu, huwa navuna miezi hiyo pia ila huwa ni maalumu kwa storage na sio kuuza manake bei yake huwa ndogo sana, kwa shamba huwa gunia linarange 45 - 55. Me vitunguu vya biashara huwa napanda mwezi wa tatu na kuvuna wasaba katikati.
 
Mkuu Bagamoyo unalimia maeneo gani? Nina shamba langu Fukayosi sijuwi kama kunafaa kulima vitunguu huko.

Bagamoyo nililimia pale mtoni mwaka jana nikavuna mwez wa tatu mwaka huu. Vilitoka poa sana.
 
Duka lipo wapi?

Ofisi ni kinondon studio ila biashara ya mbegu huwa nafanya kuanzia mwezi wa 11 mwishoni hadi mwezi wa 3 mwisho. Kwahiyo kwa sasa mbegu imekwisha mpaka mwezi wa kumi na moja manake kwa sasa ipo kwenye maandalizi. Ahsante na karibu.
 
Jamani hapo bagamoyo kuna mto?mnatumia nn kumwagilia?
 
Habari ndugu zangu,

Kwa jina naitwa Joseph ni mkulima na mfanyabiashara wa vitunguu. Kitunguu ni zao lenye manufaa makubwa na kipato cha hali ya juu endapo tu utafuata maelekezo ya mtaalamu.

Dhumuni langu hapa ni kuwaletea mbegu bora kabisa za vitunguu (Red Bombay) ambazo hukupa mavuno mazuri na yenye kipato kikubwa sana.

Bei ya mbegu hizi ni tsh 30,000/= kwa kopo la lita moja(1) na tsh 600,000/= kwa ndoo ya lita ishirini.

Guarantee: Ndoo ya lita 20 ambayo ni sawa na makopo 20 ya lita moja inatosha kupanda eneo la hekari 1 (m70*m70) na kiwango cha chini cha mavuno ni gunia 100 na kiwango cha juu ni gunia 110-120 ndani ya siku 90 (3 months) toka kupanda. Gunia moja sokoni kariakoo, ilala, buguruni, temeke na mabibo kwa sasa bei ni tsh 130,000/= * gunia 100 = tshs 13,000,000/= ndani ya miezi 3.

Kama utakua na swali lolote au kutaka kujua zaidi usisite kunitafuta kwa namba zangu za simu +255655003510 au e-mail address: josephkadendulah@gmail.com

Ahsanteni sana na karibuni tujenge maisha bora kwa kila mtanzani.
mkuu asante kwa kutupa habari hiyo, nikirudi tena mvumi kilosa kulima vitungu ntakutafuta tena ngoja ni hifadhi contacts zako
 
Yah upo mto Ruvu, water pump ndo inayotumika.

mkuu ninampango wakununua water pup,ila sijajua ipi ni bora na kwa garama ipi?kwa shamba la hekari 1-2.pia vipi maji yakisima chakuchimba yanaweza yakafaa..naomb unisaidie kaka.
 
Back
Top Bottom