Kilimo si adhabu. Ukiweka mazingira mazuri ya kilimo hata watoto watafurahia kwenda shambani

Kilimo si adhabu. Ukiweka mazingira mazuri ya kilimo hata watoto watafurahia kwenda shambani

Inawezekana kulimia trekta ni mipango tu. kama wenye mamlaka watawala wakiweka utaratibu mzuri wa kupata mikopo ya matrekta.
Acha kudanganya kwa kuota ndoto za alinacha. Kilimo cha jembe la mkono hakiwezi kumfikisha mtu pahala popote.
 
Uko sahihi sana,nakumbuka nikiwa mdogo wazazi walikuwa wanatuchukuwa tunakwenda shamba,kunapikwa chakula kule,kunachemshwa mahindi ,tunachoma mihogo n.k,ni nyakati ambazo zilikuwa zinatuvutia sana,na tukiskia kuna kwenda shamba lazima tuhakikishe na sisi hatukosi,ila nimechelewa kidogo kulipenda shamba mpaka umri huu mkubwa ndio nimekuwa na kiu ya ajabu ya kupenda kuwa mkulima...
Wazazi walikuwa ndiyo wakulima au walisimamia kilimo!
 
Hili ni jambo zuri kama watawala wangemjali mkulima.

Kuna bosi wangu alilima ekari 30 za mahindi, akavuna bei ikawa kama 200 kwa kilo, gunia la kilo 90 unauza 18000! Kisa wamefunga mipaka nk. Alikata tamaa kabisa. Hata taasisi ya fedha haiwezi kopesha kwenye mazingira tatanishi hivyo. Na nchi haitakoma upungufu wa chakula sababu watu wa kulima ekari 30+ hawakubali kuzika pesa.

Jambo la kumkomboa mkulima na kufanya tufurahie kulima ni kuacha soko huru. Mi nikauze mahindi Congo gunia 70K , hapo ndiyo kilimo kitakuwa na mkulima atakomboka. Hata nikienda benki nikiwapa mchanganuo wanaelewa.

Ni kweli ardhini kuna utajiri na kilimo ni noble professional lakini watawala wetu ndiyo wanatukwamisha.
Ukilima mahindi kibiashara na useme kilimo ni njia ya kuishi unatakiwa kuwa na eka zisizopungua 200, sasa una acre 30 unawaza kupeleka congo. Seriously [emoji15]
 
Ukilima mahindi kibiashara na useme kilimo ni njia ya kuishi unatakiwa kuwa na eka zisizopungua 200, sasa una acre 30 unawaza kupeleka congo. Seriously [emoji15]
Ukiwa na heka 200 ni lazima uwe na wafanyakazi kama 50, kati ya hao 20 wawe na ajira za kudumu na 30 vibarua.

Utahitaji dereva, mtunza store, mlinzi nk
 
Ukilima mahindi kibiashara na useme kilimo ni njia ya kuishi unatakiwa kuwa na eka zisizopungua 200, sasa una acre 30 unawaza kupeleka congo. Seriously [emoji15]
Kama kuna soko zuri, ekari 30 zinaweza kukupa pato kwa mwaka kama tu pato la afisa wa ngazi ya kati serikalini. Halafu hiyo kupeleka Congo ni mfano, haihusiani na ekari 30.
 
Kwahyo wanaolima nn ndo hawana matatizo kichwani mkuu?hongera kuishi shambani...shambani ishi ukiwa financially well...sio hata solar ushindww kuwa nayo
Miaka nenda rudi bei ya gunia la mpunga ni 35-40 huku kila kitu kimepanda, mahindi huwezi jua msimu utakuwaje ni pasua kichwani, ufuta umeliza watu mwaka jana, maharage ya njano nadhani yamesimama kwa miaka kadhaa saaa..
Mazao ya muda mfupi ni pasua kichwa sana labda upate mkataba .. kuna mzungu alitoa mbegu za maharage watu walime halafu ananunua kilo 4500 madaba.
Upande wa hass na macadamia unagombaniwa no stress
 
Kupeleka Congo kunahitajka uwe na Tani ngapi?
Heka 30 unatoa Tani ngapi?
Semi kawaida linaabeba tani 22 sawa na gunia 220.
Wakulima local wanapata gunia 4 mpaka 7 kwa ekari. Order nyingi za nje wanaanzia semi 10 na kuendelea
 
Kama kuna soko zuri, ekari 30 zinaweza kukupa pato kwa mwaka kama tu pato la afisa wa ngazi ya kati serikalini. Halafu hiyo kupeleka Congo ni mfano, haihusiani na ekari 30.
Tunapoizungumzia commercial farming tunamaana uweze kumudu na kuendesha maisha yako 100% kwa kutegemea kilimo hicho tu. Aina ya maisha haya ni kuwa na nyumba nzuri, kula vizuri kuku kuku nini kawaida, familia ivae vizuri, usafiri binafsi mzuri wewe na familia, watoto wasome shule nzuri za private, uwe na saving ya kutosha bank yaani milioni kadhaa kila mwaka hata ukifa account inasoma mamia ya milioni
 
Semi kawaida linaabeba tani 22 sawa na gunia 220.
Wakulima local wanapata gunia 4 mpaka 7 kwa ekari. Order nyingi za nje wanaanzia semi 10 na kuendelea
aisee umenipa changamoto nzuri kuhusu kilimo
 
Semi kawaida linaabeba tani 22 sawa na gunia 220.
Wakulima local wanapata gunia 4 mpaka 7 kwa ekari. Order nyingi za nje wanaanzia semi 10 na kuendelea
Mm ni mkulima wa mahindi wa kawaida Sana nalima Kati ya hekari 10-15 kila mwaka kwa zaidi ya miaka 7 Sasa.Kila hekari natoa roba 15 zenye wastani wa kilo 120 sijawahi kupata chini ya hapo

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Hili ni jambo zuri kama watawala wangemjali mkulima.

Kuna bosi wangu alilima ekari 30 za mahindi, akavuna bei ikawa kama 200 kwa kilo, gunia la kilo 90 unauza 18000! Kisa wamefunga mipaka nk. Alikata tamaa kabisa. Hata taasisi ya fedha haiwezi kopesha kwenye mazingira tatanishi hivyo. Na nchi haitakoma upungufu wa chakula sababu watu wa kulima ekari 30+ hawakubali kuzika pesa.

Jambo la kumkomboa mkulima na kufanya tufurahie kulima ni kuacha soko huru. Mi nikauze mahindi Congo gunia 70K , hapo ndiyo kilimo kitakuwa na mkulima atakomboka. Hata nikienda benki nikiwapa mchanganuo wanaelewa.

Ni kweli ardhini kuna utajiri na kilimo ni noble professional lakini watawala wetu ndiyo wanatukwamisha.
Umeweka Fact zote hii nchi inashangaza sana
 
Kilimo kwa wenzetu wanafanya matajiri maana ndio wanaweza.
Kwa wenzetu ukisikia mtu kwao au yy ni mkulima ni unamuogopa.
Huku ukisema unalima unaonekana fukara.
 
Uko sahihi kabisa, sasa hizi kauli za viongozi kusema vijana wajiajiri na ardhi tunayo. Bila maandalizi ni kutukejeli.
Tena kubwa sanaa.kilimo kina hitaji maandalizi makubwa, mtaji,wataalamu na miundo mbinu sahiii.

Nimeingia kwenye hili game nimejionea kwa macho yangu
 
Tunapoizungumzia commercial farming tunamaana uweze kumudu na kuendesha maisha yako 100% kwa kutegemea kilimo hicho tu. Aina ya maisha haya ni kuwa na nyumba nzuri, kula vizuri kuku kuku nini kawaida, familia ivae vizuri, usafiri binafsi mzuri wewe na familia, watoto wasome shule nzuri za private, uwe na saving ya kutosha bank yaani milioni kadhaa kila mwaka hata ukifa account inasoma mamia ya milioni
Nakubaliana na wewe
 
Uko sahihi kabisa, sasa hizi kauli za viongozi kusema vijana wajiajiri na ardhi tunayo. Bila maandalizi ni kutukejeli.
Kilimo ni mkombozi kama serikali inawekeza kwenye kilimo
Tumenunua ndege instead ooops sorry walisema watalii wataongezeka kutoka Mbeya kwenda Chato Chato Moshi Arusha Songwe na Dodoma Ruvuma Ruvuma Singida utalii wa ndani hahahahh
Any huuu Kilimo kinahitaji mikopo nafuu ya pembejeo matrekta masoko ya ndani na nje
Tz imebarikiwa na ardhi yenye rutuba hali ya hewa nk tulipashwa kuwa wazalishaji Africa Mashariki na Kati badala yake tunapuyanga tumeweka akili kwenye kukuza miji (Dodoma kwa mfano khee)
 
Back
Top Bottom