Uchaguzi 2020 Kimbunga cha Lissu chaingia Muheza Tanga

Huyu jamaa kila neno analoongea linatafakarisha na ni chakula cha ubongo!

Yaani Lissu sasa anawazindua watanzania kutoka katika usingizi mzito wa propaganda za Magufuli na chama chake!
Vipi zile story za "jogoo oyee!" au "jee nyinyi mnataka kupanuliwa?" Watanzania bado wanahamu ya kuzisikia?
Au muzee abadilishe upepo na kuanza kumwaga hizi za "I'm politishen i don't want so machi wed .."?

Your browser is not able to display this video.
 
Ngoja tuone mkuu. Wote tuwe wapole kwenye kisanduku cha kupigia kura. Mutampigia kura mgombea wenu, na sisi wananchi tutampigia kura rais wetu. Nasisitiza kwenye matokeo tuwe wapole.
Yawezekana wewe miaka 5 hii ilikuwa ya kheri kwako basi mpigie aliye nuru kwako.
Lakini wengine ambao mitano hii ilikuwa ya GIZA kwenye freedom, ajira, vyeo kutokupanda, mishahara kuwa stuck wakati bei zinapaa, kilimo cha biashara kinakufa nk nk hao hawatapigia kura GIZA tena bali NURU.
NURU ni nani? NURU kwao ni Lissu ambaye Mungu amemponya uhai wake kiajabu ili aje awatumikie watu wake.
Hivi Mungu anaweza kufanya muujiza pasipo sababu? Alimponya Lissu kimaajabu namna ile kwa sababu anampenda Lissu kwa sura yake nzuri? Au Lissu anatoa sadaka sana hivyo Mungu kamponya kwa sababu ni chanzo kizuri cha mapato?
Kwenye muujiza wowote wa Mungu binadamu tunapaswa kuutafakari na sio kumchukulia Mungu poa tuu.
 
Tanga ni kati ya mikoa yenye utajiri mkubwa sana lakini kama Kawaida imekosa Maendeleo tangu Mkoloni alipoondoka. Hakuna miundo Mbinu bora japo kuna Ardhi nzuri yenye Rutuba iliyoporwa na na Mabeberu na kupandwa mkonge. Tupo bilionea namba moja Mo aliyewekeza kwenye mkonge kwa malaki ya hekari lakini hakuna miundombinu hata madaraja ni hafifu .
Bilionea namba moja Afrika mashariki enzi za mkoloni na baada ya Uhuru aliyefukuzwa na Mwalimu baada ya kusema kuwa ameiweka Serikali mfukoni naye pia aliwekeza kwenye uchimbaji wa madini lakini mpaka sasa hali ni mbaya hakuna miundo mbinu.
Kifupi mkoa wa Tanga umeongozwa na wabunge wa CCM kama sehemu ya kujipatia umaarufu tu na sio kuongoza wananchi wake kujiletea maendeleo. Lushoto pekee ndiyo iliyobahatika kupata maendeleo kutokana na Kukaliwa na Wakoloni na kubahatika kuwa sehemu ya utalii.

Kuna miji midogo kama Mombo isiyo inayozungukwa na maji kwenye milima ya Usambara lakini Hakuna maji safi na salama. Watu wanapewa maji yenye matope na vumbi kwenye bomba. Wananchi wapiga kura wanaishi mabondeni kwenye mafuriko huku ardhi yao nzuri ikiwa inashikiliwa na mtu mmoja na kulimwa mkonge. CCM imeongoza majimbo yote Tanga kwa nusu karne sasa lakini hali ya maendeleo ni duni kama kawaida ya ngome za CCM ,vijana na wazee wengi hawana ya kutosha. Hata hivyo Tanga imefanikiwa saaana kupata Makada wengi wa CCM na kueneza chama hicho na kuwa mioyoni mwao kama ilivyo kwa maeneo ya mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Songea,Dodoma, Rukwa, Tabora n.k.

Hivyo Tundu Lisu akaze buti mana hizi ni ngome imara za CCM. Huko kwenye mikoa hiyo kuona Diwani toka CCM mwenye elimu ya darasa la pili ni kawaida sana. Na akaongoza mpaka halimashauri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…