Kimenuka: Lady jay Dee afunguka, Atoa wosia wake siku akifa

Kimenuka: Lady jay Dee afunguka, Atoa wosia wake siku akifa

Huyu ni kinega mkomavu. Hii ni Anti virus IV. Hadi msibani wasihudhurie na wala redio yao ya wafu isitangaze kifo chake??? Kusaga tokea amezaa na Zamaradi naona nuksi zinamuandama tu

Mkuu funguka sijakusoma.
 
Hii imeshaletwa na mdau KakaJambazi tayari....!

icon1.png
Kimenuka: lady jay Dee afunguka, Atoa wosia wake siku akifa


WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA




Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.
 
Last edited by a moderator:
sasa yale mambo au ahadi ya studio ya mh rais itakuwaje? Kuna ulazima wa hawa watu kusuluhishwa aisee.
 
Damn! What the flip is going on between her and them?

So far I've seen shots being fired from one side only and the other side is not returning any fire (at least not publicly).

Just wondering why is she so mad. What exactly did they do to her to make her this mad?

Lazima awe mbogo etii wanakata mirija.. Wanataka kuiua band yake, pia kuna uwezekano wa kukosa wadhamini ktk tv show yake.. Yaani Clouds kwa kutumia influence yao wanataka kummaliza Jide kama walivyowapoteza wengine
 
Hizi tuzo niliziponda toka nibahatike kuwasikia watu wa clouds wanaongea nani apewe tuzo
 
Mwisho WA hiyo radio unakaribia.hivi kumbe zamaradi kazaa na kusaga?hii kwangu ni breaking news
 
mia dada mkubwa cha msingi ongeza bidii katika kazi zako utafanikiwa ushauri usitegemee muziki tu angalia na mambo mengine kama biashara nakadhalika rughe na kusaga ni vinega

Hata huko kwingine wanawafuta Jide analalamikia fitna zinazohusiana na TV show yake ya DIARY walitaka iwe clouds TV bbada ya Jide kukataa wanalloby na wadhamini waipige chini kwenye hotel band yake inapopiga washaanza majungu... Ruge na Kusaga hawafai wanaitumia influence yao vibaya sana Sugu ana habari yao jins walivyompora project ya malaria no more
 
dada hii hatari dada jide naona ameamua kufunguka ile mbaya kweli joto hasira
tumekuelewa,tumekusikia mama mimi mwenyewe nahisi ntarusha hata jiwe moja kama ulivyosema
 
[h=3]WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA[/h]


Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.
Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.

Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.
Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.

Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.
Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.

Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.

Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame
Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.

Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai
Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.
Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.

Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.
Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.

Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..

Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.
Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.

Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.
Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.
Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??
Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??

Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.

Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.
Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??
Roho gani hiyo??

Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu

JIDE

jide ukifa kifo cha kawaida mimi sina neno lakini chenye utata mimi nitahakikisha nauwa hiyo radio pamoja na hao watu washenzi, dada kiukweli sio tu nazipenda nyimbo zako bali hata roho yako.
 
Go go goooo bint machozi, nakukubali sana single zako tutanunua kwan kipaji unacho.achana na machuma ulete hao wanaovizia kula kwenye migongo ya wasanii
 
Dah hata wauza madawa ya kulevya wangekuwa wanatajwa kama alivyofanya huyu dada kusingekuwepo na biashara hiyo.pole dada
 
Acha nao hao.......wasije kbs!watu wa dizain hiyo hawafai.Wanyonyaji wa nguvu za watu
 
tatizo hawa jamaa wanamtegemea mkubwa... ndio maana hujitahidi sana kupromoti kaz za mkubwa redioni kwao.. MKUBWA DHAIFU
 
Mwisho WA hiyo radio unakaribia.hivi kumbe zamaradi kazaa na kusaga?hii kwangu ni breaking news

Very breaking news......khaaaaa......!!
nikirudi kwenye topic.......mpaka Jide ameongea.....kweli hao majamaa ni mashetwain........mdada wa watu anajitahidi sana.......inaudhi kuona mtu anajituma kwa jasho lake.....mwingine anamrudisha nyuma.....kwa hili kwa kweli......limenigusa.......
 
Dah hata wauza madawa ya kulevya wangekuwa wanatajwa kama alivyofanya huyu dada kusingekuwepo na biashara hiyo.pole dada

hehehe kweli kabisa,
ila dada pole na shida zote, ila sie wengine tusingekujua kama sio hao hao, wema waliokutendea zamani, hautafutwa kwa ubaya wowote wanaokutendea sasa.
Ningefurahi katika yote ungeanza na kuwashukuru kwanza kwa dhati
 
wapi Jide mimi penda wewe sana yaani jotoHasira litupitie mbali
mimi mwenyewe hao ntawarushia hata jiwe moja siku wakija ka ulivyosema......

Kusaga ni ana roho ya kwanini yule,afu ni mtu mzima lakini anapenda kujidogosha mbaya kujiona kama wa 1990's
...........yule aloleta thread ya umri pleeease tunaomba utuangalizie huyu jamaa nae ni wa mwaka 40 na ngapi...?
 
Back
Top Bottom