Kina Mangi njooni tubadilishane uzoefu. Tushirikiane.

Aisee umegusa penyewe, kwenye biashara yoyote ile ni kinachowaangusha watu ni detail ndogo ndogo sana ambazo wanazipuuza, Wahindi na Waarabu wamefanikiwa sana sababu ya attention to details, discipline
Waafrika wote tungeukuwa makini hivi tungekua mbali sana
 
Biashara yako ukichomoa laki 1 ikayumba ujue haijakomaa hiyo, bado inahitaji kulelewa.
 
Hiyo ya kwanza inakwaza sana. unakuta umefata kitu cha aibu kununua kama kondomu au pedi hlf mijamaa imejazana hapo shop inapiga stori na muuza. nageuza zangu tu chap nasepa.
 
Natumaini neno "Mangi" ni wafanya biashara na siyo swala la ukabila?!
Tumeipenda thread yako tatizo ni hilo la "Umangi"...
 
Mkuu hujajibu ni kwa namna gani unapambana na mikopo/wakopaji?
Mkuu mi sikopeshi. Sina maana kuwa sikopeshi kabisa. Nina mama ntilie watatu tu ndo wanachukua vitu asubuhi na mchana then wanalipa jioni. Nina watu kama wanne nawakopesha ila huwa hawalazi hela yangu zaidi ya siku mbili.
Mtu akija kukopa hata kama ni mteja wangu huwa nampa maelezo mazuri ya uongo, ninamwambia nina mzigo wa tajiri na leo anatakiwa kuchukua hela yake lakin bado haijatimia.
Au namwambia biashara nafanya kwa mkopo hivyo narejesha kila sku.
Au namueleza kwa sasa hali ni ngumu sana na nina watu wengi sana naowadai kwahiyo kwa sasa nimesitisha kidogo kukopesha ili nisijekurudi nyuma.

Yaani mtu unampa maneno ambayo yatamuonesha hujamnyima. Ajue ulikuwa na nia ya kumpa lakini bahat mbaya mambo yako sio mazuri. Ili aendelee kununua kwako.

Kuna mtu mwingine anakuwa sio mteja wako kabisa, ila akitaka kukopa ndo anakuja kwako, huyo unamchana live kuwa huwa sikopeshi.

Na kwakweli hapa nilipo sijafikisha hata miaka miwili, hivyo watu wengi hawajanizoea kivile kiasi cha kunikopa hovyo hovyo.

Ukishaona madhara ya mikopo huwezi kuiendekeza. Maana tabia ya wengi ni kuwa mtu akishakukopa hata kama ni 1000 anahama duka, humuoni tena hata njia anabadilisha.

Kama upo kwenye location nzuri ukaepuka mikopo, matumizi mabaya ya pesa, na kuzingatia manunuzi yaani kununua bidhaa zako penye unafuu mbona biashara inalipa. Mfanyabiashara hupaswi kukalili duka moja la kununulia bidhaa, utashangaa unauziwa mafuta elf 52 kumbe yalishafika 49. Unatakiwa kuwa mtafiti wa bei. Nenda Manzese, nenda K. Koo nenda River side, nenda Kimara, nenda Tandale.

Mi mzee wangu ana maduka mawili ya reja reja, hana kazi nyingine lakini kanunua assets za kutosha kupitia biashara, ana maviwanja, majumba, magari. Katusomesha pia. Na mifano ya watu wa namna hiyo wapo wengi tu.
Na mimi najiona huko miaka ijayo Mungu akipenda.

Wanaoponda biashara hii jua waliifanya kwa kujaribu tu hawakuwa serious au ni watu wenye tamaa ya mafanikio ya haraka. Jamani hii biashara usifanye ukajua utafanikiwa ndani ya mwaka mmoja.
Mimi hapa nilipo nimefungua mara ya tatu. Nilifungua sehemu ya kwanza mauzo yakawa chini nikashindwa kulipa kodi nikafunga, nikaenda sehemu nyingine zikatokea changamoto kubwa sana nikafunga, nikaenda sehemu nyingine hapa nilipo kwakweli Alhamdulillah. Kama umeamua kufanya usifel mara moja ukaacha, jaribu jaribu jaribu na tena.

Pia kumbuka biashara nzuri ni ile unayoianza na mtaji kiduchu ukaikuza taratibu. Biashara ya kuanza na mtaji mkubwa au biashara ya kufunguliwa na mtu ni mara chache sana hudumu.
Wewe binafsi epuka kufanya biashara yako kwa mikopo. Tumia hela yako \ mtaji wako binafsi hata kama ni mdogo.

Angalizo; Ukimuajiri mtu dukani usitarajie maendeleo.
 
Natumaini neno "Mangi" ni wafanya biashara na siyo swala la ukabila?!
Tumeipenda thread yako tatizo ni hilo la "Umangi"...
Mkuu hili umekuja na jipya ambalo halikuwa kichwani kwangu. Au una lengo la kubadili mwelekeo wa thred
 
Hapo kwenye imani umeongea ukweli, mtaani kuna jamaa mmoja alianza biashara taratibu sana kwa mtaji mdogo baadae akapanuka kidogo.... Baadae biashara iliinuka ghafla mpaka duka likawa dogo ikashindikana kuhudumia wateja mwenyewe

Wakawa watatu tena hapo ni baada ya kumuhamisha jirani yake na kuunganisha zikawa frem mbili.... Biashara iliendelea kuumuka mpaka akaifikia frem ya 3 na yenyewe akamuamisha mtu

Biashara ilichanganyia mpaka gari la TBL likiwa likija linamalizia mzigo hapo.... Gari ya sigara ilikua inakuja na security na bunduki... Hawa Coca-Cola na Pepsi walikuwa wanamgombania..

Alikua anavamiwa mpaka na majambazi wenye bastola wanaiba pesa kwenye maboksi lakini bado jamaa yupo tu kwenye chat.... Dah jamaa alikua anauza jumla tu sababu rejareja ilikuwa kama ni kujidharaulisha au kupoteza muda

Ila alivyoanza kuporomoka mpaka utamuonea huruma, me sipendi kabisa kumuona mtu anaanguka lakini nikimuona yule jamaa huwa hata machozi yananilengalenga sababu ni mtu ninaomfahamu toka nikiwa kinda kabisa tunatumwa mahitaji dukani kwake

Ni kwamba yule jamaa saivi ni dereva kirikuu anapaki tu mahali anasubiri wateja nikimuona huwa nakuwa mdogo sana kama piriton na ninajua mtu kushuka ni time yoyote, mtu ambae alikua anafunga hesabu za mamilioni kwa siku saivi anazikimbiza elfu 10 10

Yanaongelewa mengi kuhusu jamaa ila kubwa ni hilo la imani za...
 
Asante kwa mfano hai. Ndumba mwisho wake sio mzuri mara nyingi.
 
Mnaonaje tuanzishe group la wasap tuwe tunashea mawzo ya kibiashara..hasa wa maduka ya reja reja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…