Kina Mangi njooni tubadilishane uzoefu. Tushirikiane.

Kina Mangi njooni tubadilishane uzoefu. Tushirikiane.

Wakati huo huo kuna mtu hiyo elf 70 anaipata kwa mteja mmoja tu. Location muhimu sana
Umeongea point Mimi eneo nilipo hapa mauzo ya juu kabisa kwa siku ni 70 na chini kabisa 30 kwahyo hii biashara inategemeana na location ulipo
 
Habari wadau,
Wale wenye maduka ya bidhaa za rejareja (mangi) tukutane hapa tubadilishane mawazo kidogo, tujadili ili kila mmoja aiweke biashara yake kwenyw kipimo kwa kulinganisha na wengine ili tuweze kuboresha zaidi.

Binafsi sina duka ila nna kijiduka au kibanda nilichokianza baada ya kupoteza kazi yangu niliyokuwa nayo mwanzo,

Wakuu mi nitagusia mambo yafuatayo;

1. Mauzo.
Hapa tujue mauzo ya kawaida kwa siku.
Mimi binafsi siku hazilingani, siku za j3 na j4 mauzo hushuka sana na kufikia angalau 120K kwa siku. Siku zingine hupanda kidogo mpaka kwenye 170, 150,... Siku za jmos na jpili mauzo hufika laki mbili au zaidi kidogo kwa siku.

2. Ushindani.
Hapa wakuu tushee picha halisi ya mazingira tunayofanyia biashara, na unakabiriana vipi na changamoto ya ushindani.
Binafsi mi nilipo nilikuta maduka mawili, mimi nikawa wa tatu. Mmoja wetu ana duka na genge, hivyo wateja wengi hupenda kwenda pale kwa sababu wanapata huduma zote kwa pamoja. Mi niliona nifanye tofaut, nikamix bidhaa za kawaida na nyingne kama baadhi ya vifaa vya umeme (taa, holder,..) Makufuli, etc.. maana niliona huduma hizi hakuna hapa mtaani, imenisaidia kufanya nizoeleke maana wateja wengine huja kufata vitu hivyo baada ya kuvikosa kwa hawa wenyeji.

3. Imani.
Wengi uhuhusisha hizi biashara na imani za kishirikina, na huenda sana kwa waganga kutafuta kitu kinachoitwa mvuto au king'amuzi.
Binafsi naamini hayo mambo yapo na watu wanachangamsha sana biashara zao kupitia mambo haya. Lakini mimi sijawahi kujihusisha na sina mpango sababu mambo haya huchukua hela nyingi na ukishayaanza ni ngumu kuacha. Vile vile mwisho wake mara nyingi sio mzuri.
Je nyie wadau mnalichukuliaje suala hili? Je wewe huwa unaenda?

4. Faida. Je hii biashara ina faida? Na ni kiasi gani? Unaijuaje au unaiona kwa namna gani hiyo faida?

Binafsi huwa sicomplicate, kila siku nachukua elf 20 naweka akiba. Haijalishi nimeuza kiasi gani.
Chakula cha kupika kinatoka dukani pamoja na mahitaji mengine, (hiyo yote ni faida). Lakini ninatoa kwa umakini sana. Na biashara yangu haijawahi kurudi nyuma, zaidi naongeza bidhaa mpya na kupanua kidogo kidogo.

Nawakaribisha wote wenye biashara ya namna hii tujadili, tubadilishane uzoefu, tufundishane, tufunguane, tunaeza pia kugusia na mengine zaidi kama namna ya kununua bidhaa, sehemu za kununua na mengine mengi.

Karibuni.
Hilo la Imani na mambo ya kishirikina litakuangusha usipokuwa makini. Nasema hivi kwa sababu kwenye biashara HAKUNA ushirikina. Huduma yako nzuri kwa wateja ndiyo ushirikina. Kwa uchunguzi wangu ni kuwa maduka mengi Bongo customer care zao ni majanga. Hili la ubovu wa customer care ni jambo common kiasi cha ku weza kuliandikia kitabu kikubwa kama biblia. Baadhi ya tabia mambo mabovu:
1. Dukani kwa nje kukaa watu (hasa vijana) wasio na kazi na kuangalia/kusikiliza kwa udadisi kila anayekuja dukani
2. Wenye maduka kuhudumia wateja huku wanafanya shughuli nyingine kama kuzungumza na simu etc
3. Kauli chafu za wauzaji
4. Kutokuandaa chenji za kutosha hivyo kulazimika kurudisha baadhi ya wateja au kuwachelesha.
5. Kuhudumia kwa dharau wateja wanaonunua mali za bei ndogo
6. Kuuza vitu vyenye hitilafu kwa ujanja ujanja au kurudisha chenji za noti mbovu bila kujali kuwa mteja asiporidhika leo kesho harudi tena
7. Wenye duka wanaume kutongoza wasichana wanaokwenda dukani eg ma-house girls
8. Kutoa majibu ya mkato na kukasirika wanapokutana na mteja msumbufu
9.
10.
11. Kuna mengi sana unatakiwa uzingatia.
 
Hilo la Imani na mambo ya kishirikina litakuangusha usipokuwa makini. Nasema hivi kwa sababu kwenye biashara HAKUNA ushirikina. Huduma yako nzuri kwa wateja ndiyo ushirikina. Kwa uchunguzi wangu ni kuwa maduka mengi Bongo customer care zao ni majanga. Hili la ubovu wa customer care ni jambo common kiasi cha ku weza kuliandikia kitabu kikubwa kama biblia. Baadhi ya tabia mambo mabovu:
1. Dukani kwa nje kukaa watu (hasa vijana) wasio na kazi na kuangalia/kusikiliza kwa udadisi kila anayekuja dukani
2. Wenye maduka kuhudumia wateja huku wanafanya shughuli nyingine kama kuzungumza na simu etc
3. Kauli chafu za wauzaji
4. Kutokuandaa chenji za kutosha hivyo kulazimika kurudisha baadhi ya wateja au kuwachelesha.
5. Kuhudumia kwa dharau wateja wanaonunua mali za bei ndogo
6. Kuuza vitu vyenye hitilafu kwa ujanja ujanja au kurudisha chenji za noti mbovu bila kujali kuwa mteja asiporidhika leo kesho harudi tena
7. Wenye duka wanaume kutongoza wasichana wanaokwenda dukani eg ma-house girls
8. Kutoa majibu ya mkato na kukasirika wanapokutana na mteja msumbufu
9.
10.
11. Kuna mengi sana unatakiwa uzingatia.
Tunazidi kupata somo mkuu, natumaini na wengine wataongeza mengine
 
Ni kiduka kidogo. Na sio frem bali kibanda cha chuma. Majirani zangu nafikiri wanalaza zaidi ya 500K kutokana na kuwa na wateja wengi sana sababu wamekaa miaka mingi sana hapa.
Issue ya kuuza high or low inategemea na ile actual population unayoitegemea kwa atleast kila siku pamoja na location
 
Umeongea point Mimi eneo nilipo hapa mauzo ya juu kabisa kwa siku ni 70 na chini kabisa 30 kwahyo hii biashara inategemeana na location ulipo
Hatutofautiani sana mimi frame niliopo zipo tatu ya kwanza duka la dawa ya pili duka la mabitaji ya nyumbani na latatu lakwangu mahitaji ya nyumbani bado eneo hili hili lina frame zakutosha yani mzunguko ni mdogo hapa inahitajika ubunifu wa hali ya juu nategemea kupitia huu uzi kuna vitu na ubunifu naeza pata, aksante.
 
usidanganyike na uwing wa mauzo mkuu..viduka vya mtaani nadra sana mtu kununua sukari 5kgs ..ni nusu na robo..!inahitaji wito sana hii biashara
Duka ukiweka mtaani itachukua miaka mingi sana kuwa na maendeleo au litabaki vilevile miaka yote. Ndo maana ishu ya location ni muhimu, biashara ya namna hii inatakiwa sehemu ambayo iko busy kidogo
 
Duka ukiweka mtaani itachukua miaka mingi sana kuwa na maendeleo au litabaki vilevile miaka yote. Ndo maana ishu ya location ni muhimu, biashara ya namna hii inatakiwa sehemu ambayo iko busy kidogo


Hyo 500k naamini ninsokoni mzee baba sio kitaa..au ni mjini..ila sio maduka ya kina mangi aisee ya mtaani
 
Hii biashara inalipa, japo wengi huiponda. Ni kuwa mbahiri tu. Mfano, maharage ya njano quality unanunua 1800 na kuuza 2400 kilo na hayakai, mchele unanunua 1700 au 1600, unauza 2, 000 kama upo location nzuri ni angalau sku 10 umemaliza kilo 100. Sukari unanunua 108,000 unauza 2500 na kupata 125,000. Kufuli ya kuuza 3500 unainunua 2000 au kasoro bei ya jumla. Taa ya kuuza 2500 unainunua 1700,.. n. K. Japo zipo bidhaa ambazo faida haifiki hata sh. 50.

Kama nilivyosema awali mi huwa sicomplicate kupiga mahesabu eti nimeuza labda 150K then faida ni kiasi gani. Nimejiwekea tu nipate elf 20 kila siku.
Ila mkuu unatakiwa uwe nadaftari la mauzo ambalo unaregister vitu ulivyonunua idadi, bei ya kununulia na faida atleast siku unaeza kaa ukafanya tathmini,
Kwamfano ulinunua catton ya sabuni faida 15k ukiona catton imeisha kama kuna uadilifu unauza duka peke yako jua kwenye mzunguko pameongezeka 15k likewise kwa bidhaa nyingine, so hii itakusaidia kufanya tathmini ambayo itakuzuia usitumie kuliko una hoingiza
 
Mimi nlifunguliwa mwaka jana nikala mtaji likafa, sasa hivi nina biashara ingine kabisa rafiki yangu alinshauri nifungue supermarket nikamjibu hapana nahitaji biashara itakayonipa kwa siku faida ya zaidi ya 35% per day, hata ikiwa seasonal business ila ya dizaini hiyo hapana maana mimi mwenyewe mtumiaji mzuri sana wa pesa nkijiskia hamu ya kula kuku choma napita bodaboda anafata sasa biashara kama hizo ukitoa 20,000 au 30,000 kwa matumizi binafsi unakula mtaji, ndo nililojifunza hapo.


hii mm hata bure siirudii..eti uweke kwa sk 20 haipo hyo..jua.utafeli tu kuleta mzigo...yaan ukikaza sana uweke 10 per day..! mie naijua ndan nje..! ht nipewe 10m siifanyi ng'o..jiashue unaumwa uchukue 30 UMEKWISHAA😂😂😂
 
Hyo 500k naamini ninsokoni mzee baba sio kitaa..au ni mjini..ila sio maduka ya kina mangi aisee ya mtaani
Ndo maana kuna sehemu hapo juu nilitaja mfano wa sehemu ambazo zipo vituoni kama Mbezi, Kimara Korogwe, etc.
 
Ila mkuu unatakiwa uwe nadaftari la mauzo ambalo unaregister vitu ulivyonunua idadi, bei ya kununulia na faida atleast siku unaeza kaa ukafanya tathmini,
Kwamfano ulinunua catton ya sabuni faida 15k ukiona catton imeisha kama kuna uadilifu unauza duka peke yako jua kwenye mzunguko pameongezeka 15k likewise kwa bidhaa nyingine, so hii itakusaidia kufanya tathmini ambayo itakuzuia usitumie kuliko una hoingiza
Ni kweli mkuu. Tathimini muhimu sana, nilijaribu kuandika badae nikashindwa.... Uvivu. Ila nitaanza tena.
Nilichofanya niliandika kila nilichokuwa nauza kila siku kwa sku 3 then nikaculculate faida nlopata kwa kila nlichouza, mwisho wa sku nikapata total faida, nikajua faida ya kila sku kwa makadilio. Ndo nikaja na maamuzi ya kuwa nasev hicho kiasi.
 
Mimi nlifunguliwa mwaka jana nikala mtaji likafa, sasa hivi nina biashara ingine kabisa rafiki yangu alinshauri nifungue supermarket nikamjibu hapana nahitaji biashara itakayonipa kwa siku faida ya zaidi ya 35% per day, hata ikiwa seasonal business ila ya dizaini hiyo hapana maana mimi mwenyewe mtumiaji mzuri sana wa pesa nkijiskia hamu ya kula kuku choma napita bodaboda anafata sasa biashara kama hizo ukitoa 20,000 au 30,000 kwa matumizi binafsi unakula mtaji, ndo nililojifunza hapo.
Hiyo biashara ukiipata unitag
 
Ni kweli mkuu. Tathimini muhimu sana, nilijaribu kuandika badae nikashindwa.... Uvivu. Ila nitaanza tena.
Nilichofanya niliandika kila nilichokuwa nauza kila siku kwa sku 3 then nikaculculate faida nlopata kwa kila nlichouza, mwisho wa sku nikapata total faida, nikajua faida ya kila sku kwa makadilio. Ndo nikaja na maamuzi ya kuwa nasev hicho kiasi.
Nipe namba yako ya watsap dm nikuoneshe namna ninavyo track mauzo japo biashara yangu ndogo na location haijakaa poa
 
Back
Top Bottom