Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

Naunga mkono kukataa misaada lkn serikali inampango gani kwenye kujifunga mkanda mana tusije pata msote wachache then viongozi wale kuku wote tuingie giza ili kufanya pesa iende kwenye maendeleo tupige mnada magar ya kifaahari ya serikal ili kujijengea uwezo zaidi wakandarasi wa ndani makampuni ya ujenzi ya bongo yapewe tenda kizalendo na kufanya kaz kuwe na wazir wa kuajiliwa kufanya kaz ipasavyo kuwe na dira ili waziri mwenyekuweka kutekeleza kwa awamu apewe mkataba akishindwa kufungwa na kufilisiwa na sekta muhimu zipewe uwezo na umakini kwa muda maalum apo wengi tutaenda shamba kulima maana umoja wa kitaifa utakuwepo kama wakipitisha katiba ile ya warioba itakua imefanikiwa zaid lakin kwa wengine wachache kupinga vitu bila hoja tutaona vioja sna hiki rais huyu anavunja na kujenga akija mwingine anavunja cha mwenzie na kuanza cha kwake
 
What happened in Zanzibar? Kilichotokea Zanzibar ni siasa za Zanzibar period. Irrelevant and inconsequential. Mtanitafuta ugomvi bure tu. Zanzibar walitaka kuiba uchaguzi kwa kulazimisha kushinda wakachomolewa kama walivyotaka kujaribu Bara wakawahiwa. Simple as that.

Usaliti ni kuwa na msimamo katika ukweli; wasaliti wa demokrasia ndio wamekuwa mashujaa wenu sasa?

Kweli huu uchizi. Wewe huyohuyo unasema "Siasa za Zanzibar" halafu kuna "wasaliti wa demokrasia". Tendea haki neno demokrasia, kabla ya kuandika tuu kwa njaa. Ukweli unajulikana Zanzibar CCM wamekuwa wakiiba matokeo, wewe hujui hilo? Jecha ni instrument tu pale ya mabwanyenye wenye mali na ardhi ambao wanahofia serikali mbadala. Sababu zingine za kipuuzi eti Zanzibar nchi ya kimapinduzi, kwani nchi ngapi duniani zilipitia mapinduzi na sasa demokrasia inatawala?

Eti irrelevant? Wapi?
 
Kuna wakati ambao inatubidi tuseme ukweli tu, kama kweli tunataka tujitegemee ni lazima tubadilike, tuje na vision na mission za kujitegemea ya kipindi cha miaka 20 lakini tukigawanye katika awamu nne ya miaka mitano mitano. Maana yake kipindi chote cha utawala wa Magufuli kama mungu atamsaidia akafikisha pengine miaka 10 aweke misingi hiyo ya kujitegemea, kama tuko serious na neno kujitegemea basi hatuna budi kuanza na Mapinduzi ya Kilimo, Viwanda na Utoaji wa Huduma kwa Jamii. Tutenge mikoa kazaa kwa ajiri ya viwanda tu, tuiite ukanda wa viwanda Tanzania, Pili tuanzishe kilimo cha kisasa, tuwahamasishwe bwana shamba wote wanaomaliza vyuo waende vijijini kusimamia kilimo, pia tutoe vifaa vya kisasa na kiwe na kilimo cha umwagiliaji ili mazao yanayopatika moja kwa moja yaende viwandani kwa ili tutengeneze bidhaa tuweze kuuza nchini na kusafirisha nchi za nje tuweze kuinua pato la Taifa hivyo serikali itaweza pata pesa nyingi za kuweza kutoa huduma za jamii kwa wananchi eg kujenga miundo mbinu, madawa mahosipitali, kujenga mashule, kujenga bandari , airports ili kuchochea maendeleo. Pia tukiwa tuna export thamani ya pesa yetu itaongezeka hivyo kuchochea wawekeza kuja TZ kuweekeza, leo hii pesa ya tanzania its unstable currency,leo imebadilika kuwa hivi kesho kuwa vile, haivutii wawekezaji, hivyo kufanya flow ya pesa nchini kuwa ndogo. Sasa Hii misaada kwa sasa tuichukue ili iweze kufanikisha kwanza azima yetu ya kilimo, ujenzi wa viwanda kimya kimya kwa muda fulani, then tunakuja tunaipiga chini tukiwa stable. Leo hii ukiniambia tunajitegemea wakati serikali haina pa kushika zaidi ya kukata PAYE za wafanyakazi na vikontena viwili bandari inakuwa ngumu, pato letu kwa mwezi tukilipa wafanyakazi , tukalipa madeni ya wakandarasi na maendeleo kidogo tayari pesa zote zinakwisha ,serikali iko broke kila mahali then unaniambia tujitegemee nakuwa sikuelewi, **** mambo mengine hayana siasa ,tunatakiwa just to comply with donors tupate misaada yao at the same time tunaendelea na plan zetu za kujitegemea, otherwise tutawaumiza watanzania bure, kwani kama tungepata hizo trion 1 zingeliajiri wtz wangapi? tungesema tuzimwage kwenye viwanda tungelijenga viwanda vingapi? tuweni wakweli.
 
Shida sio misaada, Hoja walizojenga mbona hamzungumzii???? mbona unajitoa ufahamu bure? wewe upo marekani, unaelewa maana ya kukaa na kiza mwezi mzima? acha kufurahisha genge kaka....
Tumejiandaaje kujitegemea kama sio unaongea vitu vya kufikirika? unadhani maisha ni riwaya?
Shida ni misaada...unadhani ingekuwa sio msaada kwa nini wasiseme tunasitisha uhusiano let say wa kibiashara?
 
CHALLENGE
MM
Njoo uishi Tanzania isiyopokea misaada kwa mwaka mmoja tuu
Njoo wakati tunavumilia maumivu ya kuwacha ulevi wa kutegemea misaada
Hata teja anapewa methadone ili awache uraibu taratibu
Oh..by the way pitia Sumbawanga/Tunduma,Tanga/Horohoro,Namtumbo/Mbinga uwambie tulifanya makosa kupokea msaada wa MCC kuwajengea barabara hizo
Ina maana bila MCC hiyo njia isingajengwa?
Unaujua mfuko wa barabara?
Unajua ni kiasi gani cha fedha za kitanzania zilitumika hapo?
 
Shida sio misaada, Hoja walizojenga mbona hamzungumzii???? mbona unajitoa ufahamu bure? wewe upo marekani, unaelewa maana ya kukaa na kiza mwezi mzima? acha kufurahisha genge kaka....
Tumejiandaaje kujitegemea kama sio unaongea vitu vya kufikirika? unadhani maisha ni riwaya?
Mbona hiyo misaada ilikuwa inatolewa miaka ya nyuma kwanini mna kaa giza mpaka leo ??
 
Mbona hiyo misaada ilikuwa inatolewa miaka ya nyuma kwanini mna kaa giza mpaka leo ??

Kwani MCC ilianzishwa mwaka gani?
Hata hivyo CCM ipo kwenye position nzuri sana kujibu hilo swali lako la msingi.... kwamba kwa miaka 55 tumeshindwa kujitegemea, leo kwa kunyimwa misaada kwa ulafi wa madaraka mnakuja na drama za uzalendo na blabla...kujitegemea bila viwanda, umeme wa uhakika na uzalishaji wa kibiashara umeona wapi mkuu
 
Hilo ndio tatizo; kwa hiyo kama Uchaguzi wa Zanzibar usingefutwa na Shein angeshinda kihalali bado watu mngeendelea kutaka misaada?

Kuna mambo mnataka kuchanganya hapa. Sasa sijui ni kwa bahati mbaya au ni makusudi tu. Tuliosoma somo la Siasa ni kwamba chuki dhidi ya Misaada tulipewa wakati huo. Ilikuwa ni chuki ya kielimu na wazi kabisa. Jiulize ni kwa nini bado tunaamini katika hiyo misaada kupitia tune ya SAP hasa leo kupitia kejeli ya Zanzibar. Nimesema kejeli ya Zanzibar
 
Hapo sasa angalau ubongo umeanza kufanya kazi; kila mmoja anatakiwa kuwa na mawazo ya namna gani tunaweza kujitegemea, siyo kusema hatuwezi. Hivi kesho MCC wakiamua kurudisha misaada yao na mambo ya Zanzibar hayajabadilika si mtageuka kinyume nyume tena?
Kama kauli yako ingerandana na mawazo ya viongozi wa UKAWA unafikiri kungekuwa na mabishano kama hivi. La hasha. Ungepata like hadi ungeomba poo. Kama kauli ya kutoshabikia misaada katika kipindi hiki angeitoa kiongozi wa UKAWA ungeona maoni tofauti na haya yanayoendelea katika mitandao.
Kwa ufupi wa fikra hivi sasa watanzania tumekuwa washabiki wa maneno ya viongozi wa vyama na sio mantiki au uhalisia wa kauli. Hakuna mtu anayependa kuishi kwa kuombaomba. Tusiwe muflisi wa fikra, hili jambo halifurahishi hata kidogo. Kila kiongozi wakati wa kampeni alikuwa anahubiri jinsi ya kuondokana na utegemezi, leo hali imekuwa tofauti kabisa, misimamo imebadilika. Kulikoni? Tulikuwa tunasikia wanasiasa wanajinadi "nchi hii ni tajiri lakini tumekuwa ombaomba." Hili geuko la ghafla linatokana na nini? Hili jambo kwa kipindi hiki limegubikwa na utashi wa kisiasa lakini mwanzoni viongozi wa serikali walikuwa wanalaumiwa sana kwa kutembeza mabakuli kwa wafadhali.
Leo muombwa amekuwa tofauti kwa sababu tofauti ambazo zinazobadilika kila inapofika kipindi cha kutoa msaada sasa fikra za watu zimehama na kuwa tofauti na misimamo yao ya awali. Je shida ni Zanzibar au Sheria ya Mtandao ndizo zinazobadilisha fikra zetu? Hata tukitimiza matakwa yao kwa kipindi kijacho tutasikia mambo mapyaaa, jamaa wanatudhalilisha sana! Hebu tubadilike tuepuke huu udhalilishaji.
 
Ina maana bila MCC hiyo njia isingajengwa?
Unaujua mfuko wa barabara?
Unajua ni kiasi gani cha fedha za kitanzania zilitumika hapo?
Usujtie ujuaji wa kipunda barabara hizo na ile ya Namtumbo/Songea/Mbinga ni fedha za MCC
Source yako ya information ni gazeti la Uhuru hujui lolote ushuzi mtupu
YOU do justice to your name
 
Suluhisho ni rahisi sana, ni kutimiza demokrasia kama inavyopaswa na iwapo utashindwa ni lazima ukubali. Na iwapo tuna lengo kabisa la kutoka hapa tulipo ni lazima tukope ili kukuza kilimo na kujenga viwanda vya kutosha. Kinyume na hapo tutashinda hapa kila siku kulaumiana na wale wengine kupambana kuhakikisha wanasifiwa bila kuleta maendeleo zaidi ya kubaki madarakani.
Demokrasia inakuwepo wakati gani?..kwa hiyo Sefu alivyosema kapata zile kura alizosema ndio demokrasia?
 
Usujtie ujuaji wa kipunda barabara hizo na ile ya Namtumbo/Songea/Mbinga ni fedha za MCC
Source yako ya information ni gazeti la Uhuru hujui lolote ushuzi mtupu
YOU do justice to your name
Hivi unajuwa zaidi ya nusu ya fedha za MCC hurudi US?..Hivi unajuwa kauli ya Raisi kukataa kuongeza mikataba kwa Syimbion ni sababu ya kusitish?...Hivi unajuwa US hupata faida ya hadi mara tano ya kila dola anayotowa?..hivi unajuwa kampuni binafsi za kimarekani zimepata pigo?...Hivi unajuwa US/EU na vibaraka wao wa ukawa kwa pamoja walishindwa uchaguzi?...Hivi unajuwa kwamba Luwasa aliingia mikataba ya siri na serikali za kimagharibi wakiamini angepitishwa na CCM...na hata wamefadhili kampeni zake?
 
Kwa nini unakwepa tatizo halisi ambalo ni ukiukwaji wa democrasia nchini na matumizi mabovu ya sheria ya mtandao kuumiza wananchi kwa maslahi ya watawala?

Kuna mendeleo yakinifu chini ya utawala mbovu usiojali wananchi badala yake unalinda genge la watawala?

Unapiga kelele juu ya wageni na misaada, mbona sioni unaongelea njia mbadala za kufikia kujiendeleza bila kuwaumiza Wafanyakazi wa Tanzania ambao diyo wamebeba zigo la kodi isiyotosha kitu kwa mahitaji muhimu ya binadamu wa Tanzania achilia mbali maendeleo?

Unachokifanya hapa ni unafiki na propaganda ambazo haziwezi kuwa mbadala wa utawala bora unaolalamikiwa. Ninatamani uje uugue hapa uende hospital ukose hata drip ya maji kwa kuwa hazipo ili ushike adabu. Naona kama unaongea ukiwa umevimbiwa. Njoo huku ukutane na vibaka wakuvue hadi huo mkanda unashikilia suruali yako wakuache mtaroni na kuiba laptop yako kwa kuwa hakuna ajira na maisha magumu ndipo utajua kuvimbiwa ni dhambi.

Fika hapa umpeleke mkeo kujigungua akose huduma ndipo ukapofahamu madhara ya unafiki wako.

Kujitegemea kunakujaga kwa makelele ya kinafiki, adhabu ya utawala mbovu au ni mipango inayopangwa na kutekelezwa kitaalamu kwa kupunguza degree ya dependency gradually hadi hapo inapokuwa zero?

Acha upumbavu wako wa kinafiki hapa. Wewe haupo Tanzania unaimba nyimbo kikasuku kwa ujinga huku wanaoumia ni wengine. Ninatamani hata huko uliko mfukuzwe ili uje uone madhara ya ushenzi wa kutetea utawala mbovu na uonevu wa raia. Halafu ndipo uanze kuleta uharo wako kwamba tujitegemee bila maandalizi.



Sijui ni kina nani ambao hawakuwahi kuandika kuhusu utegemezi. Mimi si mmoja wao. Msimamo wangu kuhusu misaada ya kigeni haujaibuka sababu ya MCC kusitishwa kama baadhi ya watu wanataka tuamini. Kama kuandika juu ya hili nimeandika sana na tena wazi kabisa. Sijabadilika msimamo wangu. Na wengine wanalizungumzia hili la MCC leo wakati wengine tulilizungumzia miaka sita nyuma! Hili la MCC limenipa tu sababu ya kuendelea na msimamo huo huo niliokuwa nao. Ushahidi wangu upo hapa:

Niliandika hili - STOP FOREIGN AID TO TANZANIA CAMPAIGN - hili ilikuwa Nov 19, 2008. Nikimjibu Mwalimu Augustino kwenye mada hiyo nilihoji hivi "Mwalimu ni kitu gani ambacho sisi wenyewe tunaweza kukifanya kwa uwezo wetu na fedha zetu wenyewe. Unafikiri misaada ya kigeni??? imetusaidia kuendelea na kiwango cha maendeleo kinaakisi misaada tuliyopokea hadi sasa?"

Niliandika hili -ARE WE ADDICTED TO FOREIGN AID? - hii ilikuwa Feb 17, 2009. Nikaandika hivi mle "Alas! May the truth be told, as a nation we can only function at least semi-effectively as long as there is this constant flow of foreign through the veins and capillaries of Tanzania, without which we will collapse like pieces of cookies in a milk jar! We depend on this drug, we beg for it, we long for it, we sing with high pitched voices, screaming and rukarukaring like kids in a candy store. Whenever we are promised that there is some more coming we smile so wide and our eyes get teary with joy! Our desires are stirred like a man tempted by that midnight temptress in the fortress of passion! "

Katika mada iliyoanzishwa na Mzalendo Halisi Cutting Off Aid - A Condition to lift Africa from Poverty - ya Feb 24, 2009 nilichangia na kuhoji ifuatavyo: "najiulizana sana kwamba endapo misaada ya kigeni itasitishwa:

a. tutaendelea kuwa na NGOs nyingi hivi?
b. Je watanzania wanaweza kujitolea fedha zao kufanya kazi za kujitolea?
c. Itakuwaje kwenye misaada ya visima iliyoanzishwa na fedha za wahisani, tutamudu kuiendeleza?
d. Vipi kuhusu miradi mingine inayosapotiwa na wahisani nayo itakuwaje?"


Nikaandika mada nyingine WAFADHILI MMEIDEKEZA TANZANIA, BADO TUNATAKA NYONYO - hii ilikuwa ni mada ya Feb 26, 2009. Niliandika mle jambo hili "Ninachosema ni kuwa, wakati wa kutukatisha kunyonya umefika. Tayari tuna wasomi wa kutosha, tuna raslimali ya kutosha, tuna watu wa kutosha na tuna sababu za kutosha kujitegemea. Lakini zaidi ya yote tunaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa katika kujiletea maendeleo. Hadi hivi sasa ninachokiona ni importation of development ambapo kile tunachokiita "maendeleo" kwa kweli ni vitu tulivyocopy and paste kutoka ng'ambo! Juzi nilimsikia Waziri Mkuu akitaka watu wanunue vitunguu vya Tanzania!!! Yaani kwa maneno mengine Tanzania inaagiza hadi vitunguu kutoka ng'ambo ambayo wenyewe tunaviona ni 'bora'!" Na watu wananituhumu sijaandika kuhusu "kujitegemea"!

Niliandika tena muda si mrefu baadaye hili RAIS MWENYE MAWAZO YA KUOMBAOMBA - Hii ilikuwa Aprili 9, 2009 Nilikuwa nainukuu hotuba ya Rais na nilitanguliza kusema hivi kabla ya hotuba yenyewe "Sehemu ya hotuba ya Rais Kikwete inayothibitisha kuwa hana mawazo ya kuinua hali ya maisha ya watanzania bila ya kukinga mikono kwa nchi matajiri; asilimia 99 ya mambo anayotaka nchi matajiri zifanye kwa Afrika yanaweza kufanywa na Afrika wenyewe!"

Hiyo ni mifano tu ya nilichokisema na kukiandika humu kuhusu fikra zangu juu ya misaada ya Kigeni; kuna tofauti yoyote na nilichosema leo? Na nimeandika vingi vingine kwa mfano,

Niliandika hivi juu ya MCA ambayo ndio ilikuja mwanzo kabla ya kuwa MCC. Ni katika mada ya SYMBION POWER ACQUIRES DOWANS POWER PLANT

"tatizo liko toka mwanzo tulipokubali kuwa sehemu ya hii MCA. Wengi walifikiria kuwa MCA ina lengo la kutupa sisi uwezo na kujenga uwezo wetu wa ndani la hasha. Masharti ya MCA kama yalivyo masharti ya miradi mingine mingi tu ya Wamarekani ni kuwa fedha za walipa kodi wao ni lazima zinufaishe Marekani. Sasa mimi siwezi kuwalaumu kwa hili. Fikiria dola milioni 700 zinaweza kufanya nini Marekani? Kweli tulifikiria Wamarekani watatoa hizo milioni 700 kwa Tanzania bure tu? Kwa undugu gani?"

Na nikaongeza na kusema,

Hatuwezi kuwalaumu. Kama tungekuwa tunataka kweli iwe ni misaada ya kutunufaisha na sisi watawala wetu wangesema mapema kwenye masharti kuwa kwa kila dola moja inayopelekwa Marekani dola nyingine moja ibakie Tanzania. Lakini hatuna sera ya misaada ya kigeni Tanzania hivyo tunakuwa katika huruma ya wale wanaotoa misaada na hatuwezi kuwalaumu. Kwa wananchi wa kawaida kwa kweli hiyo haiwajalishi maana kama serikali yao imeshindwa kutatua tatizo la nishati na Wamarekani kwa kutumia fedha zao, na makampuni yao wanakuja kusaidia why not?

Sasa leo naambiwa ati sijawahi kuandika juu ya hili; na nina uhakika licha ya kuweka rekodi yangu wazi kuwa sijabadilika kama inavyodaiwa wapo wengine wanaweza wasikiri kuwa "kweli mwanakijiji msimamo wako haujabadilika juu ya misaada ya kigeni". Watajaribu kuuelezea kwa kunilazimisha nizungumzie masuala ya Zanzibar kwa mitazamo yao.

Mwaka 2003 - zingatia kuwa nimesema yale yale tangu 2008! niliandika mada iitwayo
Stop unscrupulous Foreign Aid to Tanzania campaign towards 2015. Niliandika hivi mle:
What would happen if we were to initiate such a campaign to demand that foreign aid ought to be halted until a new policy on solicitation of the same is put in place? Unafikiri CCM na serikali yake watafanya nini kampeni hiyo ikianza?

Je wrwe kama Mtanzania utaathirika vipi na usitwishaji wa misaada hiyo? Je kama kuna misaada kweli inahitajika ni ipi na kwa maeneo gani au kwa muda gani?

Unafikiri tunaweza kupiga hatua ya haraka ya maendeleo bila misaada ya kigeni?


Sasa ni kweli nimebadilika? Ni kweli sijazungumzia kuwa huru kutoka misaada ya kigeni? Ni kweli msimamo wangu wa leo unatokana na matukio ya juzi ya uchaguzi? Au ni msimamo unaotokana na kuthibitika katika kanuni ninazozisimamia. Mtu anayesoma anaweza kuamua mwenyewe bila kuongozwa na hisia za kisiasa au kisasi au kutotaka kuwa mkweli au kuogopa kusema "mwanakijiji yuko sahihi" kwa sababu ataonekana anakubaliana na mtu ambaye hakudandia mabadiliko yale feki!

Naendelea kuamini kusitishwa MCC iwe sababu tu ya kutaka kuondoka na misaada hii ya kitegemezi ya kigeni ambayo imetufanya tuwe watu tusiojiamini, wenye mawazo ya kubembeleza na ambao tuko tayari tufanywe lolote ili mradi dawa hii nzito ya kulevya iingie kwenye damu zetu!

Nitaendelea kupinga misaada ya kigeni ya aina ambayo tunapokea sasa hadi tutakapokuwa tayari kuwa na ushirikiano wa kigeni ambao msingi wake ni heshima, utu, kusaidiana na kuinuana. Na kabisa napinga misaada ya kigeni inayoingizwa kwenye bajeti ya nchi moja kwa moja au ile ambayo inakuja nje ya maeneo yale matatu niliyoyaanisha katika ile mada nyingine. Katika hili inawezekana nimebakia "mimi tu, mimi kuwaletea habari"

MMM
 
Wanaompinga Mwanakijiji wanafanya hivyo kwa sababu za kisiasa tu na si uhalisia.....

Na wengi wanaompinga ni washabiki wapya wa CDM waliokuja na Lowassa.....huo ndio ukweli.
 
What happened in Zanzibar? Kilichotokea Zanzibar ni siasa za Zanzibar period. Irrelevant and inconsequential. Mtanitafuta ugomvi bure tu. Zanzibar walitaka kuiba uchaguzi kwa kulazimisha kushinda wakachomolewa kama walivyotaka kujaribu Bara wakawahiwa. Simple as that.

Kama hayo unayoyasema ni Ukweli wenye kupanga njama za kuiba uchaguzi wangekuwa Lupango sasa hivi, hizo unazozisema ni conspiracy theory!

Eti kwa kuwa Zanzibar walielekea kushindwa, wakifuta uchaguzi unaona sawa kwa kuwa " Waliiba".

Lakini kumbuka hata huko Zanzibar kuna kura za Raisi wa Muungano, Nikuulize swali, Je nazo waliiba ngapi?, Iweje basi waiba uchaguzi wa huko Zanzibar ambao kimsingi ni walewale tu wa nchi nzima waibe za Raisi wa Zanzibar lakini wasiibe na kura za Muungano kwa upande wa Zanzibar?
Vipi uchaguzi wa Raisi wa Muungano na Wabunge kwa huko Zanzibar uwe sahihi kwa muktadha huo?
 
Utajiandaa vipi kujitegemea wakati hata kufikiria kujitegemea hutaki? Utaweza vipi kujiandaa kuacha kunyonya wakati kila nyonyo ikichomolewa unalia "mama kaa chini ninyonye". Well.. ikisitishwa labda tutapata watu wenye akili ya kuona ni vipi tutaweza kujitegemea kwa sababu hatuna 'mjomba' wa kuturushia vijihela...
MM, hili halihusiani na kujitegemea acha kupotosha. Halikufanywa au halikutokea kwa sababu tunataka tujitegemee. Zipo nchi zinajitegemea na bado wanapata misaada. Ni kupotosha kwa makusudi kufikiri kuwa tanzania tulikiuka vigezo vya MCC ili tukose package ya pesa za Changamoto za milenia ili tuanze kujenga mazingira ya matayarisho ya kujitegemea. By the way, wewe uko US, huwez ona madhara kukosa hela hii, ambayo masharti yake siyo magumu!

Sote MM tunakubaliana umuhimu wa kujitegemea, lakini siyo kwa style hiyo unayotaka kutuaminisha!
 
Kama kauli yako ingerandana na mawazo ya viongozi wa UKAWA unafikiri kungekuwa na mabishano kama hivi. La hasha. Ungepata like hadi ungeomba poo. Kama kauli ya kutoshabikia misaada katika kipindi hiki angeitoa kiongozi wa UKAWA ungeona maoni tofauti na haya yanayoendelea katika mitandao.
Kwa ufupi wa fikra hivi sasa watanzania tumekuwa washabiki wa maneno ya viongozi wa vyama na sio mantiki au uhalisia wa kauli. Hakuna mtu anayependa kuishi kwa kuombaomba. Tusiwe muflisi wa fikra, hili jambo halifurahishi hata kidogo. Kila kiongozi wakati wa kampeni alikuwa anahubiri jinsi ya kuondokana na utegemezi, leo hali imekuwa tofauti kabisa, misimamo imebadilika. Kulikoni? Tulikuwa tunasikia wanasiasa wanajinadi "nchi hii ni tajiri lakini tumekuwa ombaomba." Hili geuko la ghafla linatokana na nini? Hili jambo kwa kipindi hiki limegubikwa na utashi wa kisiasa lakini mwanzoni viongozi wa serikali walikuwa wanalaumiwa sana kwa kutembeza mabakuli kwa wafadhali.
Leo muombwa amekuwa tofauti kwa sababu tofauti ambazo zinazobadilika kila inapofika kipindi cha kutoa msaada sasa fikra za watu zimehama na kuwa tofauti na misimamo yao ya awali. Je shida ni Zanzibar au Sheria ya Mtandao ndizo zinazobadilisha fikra zetu? Hata tukitimiza matakwa yao kwa kipindi kijacho tutasikia mambo mapyaaa, jamaa wanatudhalilisha sana! Hebu tubadilike tuepuke huu udhalilishaji.
Mkuu, naamini kila mmoja angependa nchi yetu ijitegemee, lakini bado tunazo changamoto, ni hatua siyo suala la muda mfupi. Jana tumeahidiwa mkopo wa Tsh 100bn> wa masharti nafuu kutoka Japan. Maana yake ni nini, ni kuwa bado tuna changamoto ya rasilimali pesa.

Hivyo kuhusianisha kukosa pesa za MCC kuwa ni kwa sababu tunefanya hivyo kwa nadharia ya maandalizi ya kuanza KUJITEGEMEA, hilo si kweli!
 
Back
Top Bottom