Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

Mkuu samahani sana kwa kukukwaza kwani hata nami ni muungwana, ila kumbuka hili ni jukwaa huru na hapa ni kwenye mjadala huru. Pindi tunapoona upotoshaji mnaufanya kwa makusudi ni lazima tukemee bila kujali utapenda ama la. Samahani kwa kukukwaza ila jirekebishe na huu upotoshaji unaoufanya wa eti ushoga sijui nini.
Mkuu samahani kama ungekuwa unafuatilia uzuri ungeona nani aliyeleta suala la ushoga kwenye majibu yangu. Kwa kweli naafiki huo uungwana wako, sote tupo huru lakini tuchunge ndimi na mikono yetu, maneno mabaya sio mazuri kwa viumbe mwenzio. Pole saana, natumai sijakukwaza.
 
MMM hili povu linalowatoka leo mbona hamukuanza kulitoa miaka 10 nyuma?
Wakati wabunge wa upinzani wakipinga safari za JK kwenda ughaibuni kuomba misaada si nyinyi ndio mlisema hawaitakii mema nchi yetu?
Leo ndio mmeshituka akili baada ya kunyimwa misaada? (Kumbuka tumenyimwa na sio tumeikataa)
Mkiwa mnazungumzia kukatwa kwa misaada ya MCC kuweni wazalendo kwa kutaja pia kwamba sababu za uhuni wa ccm Zanzibar ndio chanzo chake!
 
Mzee Mwanakijiji matamko yanayojitokeza baada ya kunyimwa nayafananisha na sizitaki mbichi hizi, pamoja na maelezo yako swali bado linabakia kwa nini tumenyimwa fedha za MCC je ni kwa sababu sasa Tanzania tunaweza kujitemea bila msaada?

Swali la msingi ni je tuliwaambia hatutaki au tuliambiwa hatutapewa??? ni vizuri kuanza mazoezi ya kujitegemea kiuchumi pamoja na hayo si jambo jepesi na kwenu ninyi msiokaa Tanzania hamtaelewa haya.
 
Hii nchi bwana viongozi wetu wasanii sana, utasign vipi mkataba ambao huwezi kuutekeleza? moja ya masharti ya mkataba wa MCC ni pamoja na kudumisha demokrasia nchini, hayo yote ni mambo ambayo yamo ndani ya huo mkataba ambao mlikubali wenyewe, tujifunze kutekeleza kitu ambacho tuna kisign sio kuja na issue ambazo hazina uhusiano hii ni kuumiza jamii wakati nyie mnaendelea kula mapocho pocho wakati huo mitaani kumekauka.
 
Kwani Seif alipotangaza kura zake, ilizuia vipi tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendelea kutangaza matokeo!?
Tume haikuendelea kutangaza sababu matokeo yalichezewa...na matokeo ya tume ni tofauti na ya Seif.
 
Masharti ya MCC yalikua wazi lakini bado tukaapply? na tuliapply huku tukijua tunaenda kubaka demokrasia... Pathetic!

Well sipendi misaada ila yaliyotokea Zanzibar ni hatari hata zaidi ya hiyo misaada yenyewe!!
 
Sheria iko wazi, hakuna anayemtetea Seif kwa kuvunja sheria, alipaswa kukamatwa na kushitakiwa kwa kujitangaza na sio kufuta uchaguzi wote mpaka wa masheha. Ama kwa maneno mengine unataka kusema Seif alitangaza mpaka matokeo ya masheha? Mkubali mkatae ccm imetuingiza kwenye hasara kubwa na uwezo wa kupata 1trilioni kwa ajili ya maendeleo ccm haina. Nikisema hivi simaanishi naisujudia misaada la hasha, ila kiukweli msaada ule kumbuka sio mkopo, hivyo tungeweka mambo mengi sawa kuliko ccm kupata madaraka huko ZnZ. Unaweza ukaniambia kama ZnZ inaweza kuchangia 1trilioni kwenye bajeti ya nchi hii? Kwani tukitumia akili kuna shida gani ndugu zetu wa ccm, ni kwanini muifanye nchi iwe maskini kwa ajili ya nyinyi kutaka madaraka?
Kukosa msaada sio hasara.
 
Waruhusu bangi NA madawa ya kulevya NA mirungi wala atuitaji kumtegemea mtu
 
Tume haikuendelea kutangaza sababu matokeo yalichezewa...na matokeo ya tume ni tofauti na ya Seif.

Nnaona unazunguka zunguka tu na kujibu kijumla jumla, yangu macho kwa huko tunapo elekea na ahadi ya Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati...

CCM Mmejisahahu mnadili na mabeberu...
 
Kukosa msaada sio hasara.

Wakati mwingine uache utani kwenye mambo makubwa, kama huna hoja si vibaya ukakaa kimya? Tuambie hasara ni nini? Huwa tunatofautiana kwa itikadi na nilikuwa naheshimu michango yako maana hoja nilikuwa naziona hata kama sikubalini nazo. Lakini huku unakoelekea naona unatoka kwenye utu uzima unarudi utotoni.
 
Kukosa msaada sio hasara.

Hasa kwa wanaoshindwa kufunga vifungo vya mashati yao kutokana na shibe wanazozipata chini ya mgongo wa CCM, na mzigo mkubwa tupo 'punda' tutaubeba bila maswali.

Poleni sana makabwela wenzangu...
 
Mzee Mwanakijiji matamko yanayojitokeza baada ya kunyimwa nayafananisha na sizitaki mbichi hizi, pamoja na maelezo yako swali bado linabakia kwa nini tumenyimwa fedha za MCC je ni kwa sababu sasa Tanzania tunaweza kujitemea bila msaada?

Swali la msingi ni je tuliwaambia hatutaki au tuliambiwa hatutapewa??? ni vizuri kuanza mazoezi ya kujitegemea kiuchumi pamoja na hayo si jambo jepesi na kwenu ninyi msiokaa Tanzania hamtaelewa haya.

Huwezi kuamini huyo mzee mwanakijiji nimemuomba arudi nyumbani aje atupatie na sisi huo ujuzi aliochuma huko nje ili kama taifa tufaidike, hata kunijibu hajathubutu na nimemuomba zaidi ya mara tatu. Ila namuona anajibu vijembe tu. Hawa akina mzee mwanakijiji ni wale wachezaji wanaoona makosa ya wenzao wakiwa nje ya uwanja lakini wakiingia ndani inakuwa aibu. Anajaza minadharia hapa jukwaani, ukimwambia njoo nyumbani tutumie hayo mawazo yake anakaa kimya. Si unafiki ni nini huo?
 
WanaCCM tumeshaeleza wazi kuwa hatuna shida na vijimisaada vyenye masharti. Hili hata mstaafu Kikwete alilizungumza na sasa rais Dkt Magufuli anazidi kulikazia.

Ni marais wawili tu walioamini katika kujitegemea nchi hii. Baba wa Taifa na kitukuu chake Magufuli. Wengine wote hapo katikati hawajawahi kujiamini kama wanaweza. Na hili suala sio la CCM, maana CCM ilikuwepo hata wakati wa Kikwete. Hili ni la MAGUFULI.
 
Ni marais wawili tu walioamini katika kujitegemea nchi hii. Baba wa Taifa na kitukuu chake Magufuli. Wengine wote hapo katikati hawajawahi kujiamini kama wanaweza. Na hili suala sio la CCM, maana CCM ilikuwepo hata wakati wa Kikwete. Hili ni la MAGUFULI.

Kujiamini tu kuwa utajitegemea bila mipango inayoonekana hiyo itakuwa kazi bure, suala la Uchumi ni kanuni sio siasa mkuu..

Na mpaka hapa mh raisi amesha feli..... muda utaamua.
 
Huwezi kuamini huyo mzee mwanakijiji nimemuomba arudi nyumbani aje atupatie na sisi huo ujuzi aliochuma huko nje ili kama taifa tufaidike, hata kunijibu hajathubutu na nimemuomba zaidi ya mara tatu. Ila namuona anajibu vijembe tu. Hawa akina mzee mwanakijiji ni wale wachezaji wanaoona makosa ya wenzao wakiwa nje ya uwanja lakini wakiingia ndani inakuwa aibu. Anajaza minadharia hapa jukwaani, ukimwambia njoo nyumbani tutumie hayo mawazo yake anakaa kimya. Si unafiki ni nini huo?

Mkuu hawa jamii ya watanzania waishio nje ya nchi hawajui kabisa tunapitia changamoto zipi katika maisha. Ila wanapenda sana kujiachia nyuma ya computer na nadharia zisizotekelezeka.

Huwezi tu kuanza kusifia kunyimwa misaada bila kueleza tutawafikia vipi wananchi walio wengi waliopo gizani. Nini mbadala wa Trilioni 1 ya MCC???
 
Mkuu hawa jamii ya watanzania waishio nje ya nchi hawajui kabisa tunapitia changamoto zipi katika maisha. Ila wanapenda sana kujiachia nyuma ya computer na nadharia zisizotekelezeka.

Huwezi tu kuanza kusifia kunyimwa misaada bila kueleza tutawafikia vipi wananchi walio wengi waliopo gizani. Nini mbadala wa Trilioni 1 ya MCC???

Ndugu yangu wacha tu, watu wanapiga siasa hapa, ukiwasikiliza hao viongozi ndio utabaki kinywa wazi, wakija hao madiaspora utatamani hata kutapika. Leo uniambie eti hutaki 1trilioni zenye masharti ya kutii demokrasia, halafu ubaki unakimbizana na 2b tshs za mkwepa kodi wa makontena manne!! Hao madiaspora ukiwaambiwa waje watekeleze hayo manadharia yao hapa nchini akija wiki moja kuzika tu, wiki inayofuata karudi kwa wazungu. Ukimuuliza mbona unaondoka haraka hivyo anakuambia huku maisha ni hovyo sana. Sasa si wayabadilishe hayo maisha ya hovyo, wanabaki kupiga vijembe vya kiingereza visivyo na msaada kwa mkulima wa tandahimba.
 
Msiwe na Wasiwasi na hizo fedha za MCC. Rais wetu mpendwa alishasema TANZANIA YA VIWANDA INAKUJA!
 
Pamoja na kwamba ninaunga mkono HOJA yako (either uwe uliianza siku nyingi au le, kwangu mimi hilo sio muhimu) lakini ni vizuri pia tujikite kwenye kisababishi ya kuondolewa hiyo inayoitwa misaada. Nini msimamo wako kwa kile kilicho tokea Zanzabar? Lakini pia tukumbuke hivi, rais mstaafu wa awamu ya 4 alikua muumini mzuri sana wa kuamini katika misaada, ilifikia kipindi watu wakaanza kukumbuka nukuu mbali mbali za maias waliopita kuhusu misaada na kumlinganisha na yeye, ukweli kwake iliishia kua matusi tu; kama kumbukumbu zangu zitakua zipo sawa, ni kama na yeye alianza kutuandaa kisaikolojia kua tuanze kujitegemea, na kama kumbukumbu zangu zitaendelea kua sawa basi nakumbuka kuongezwa kodi ya Mafuta ya jamii ya Petrol ili tujitegemee (hi ni miongoni mwa sababu zinazo sababisha Tanzania bei ya mafuta kuendelea kua juu ili hali sokoni yameshuka). Kinacho nihuzunisha ni hiki, JK, Magufuli pamoja na wewe mwenyewe MMM ni kutwambia tujitegemee bila kujali kisababishi. JK alituandaa hivyo mara baada ya Wazungu kutishia kuto kutoa pesa kwasababu ya mambo ya Escrow, Kafulila alitaahadharisha hili JAMBO bungeni wakati mambo ya Escrow yanachangiwa, aliyekua waziri wa fedha bi Saada Mkuya na profesa Muhongo wakabisha, KIKO wapi leo? Haya jambo la Zanzibar ndio hilo, hakuna mwana ccm yeyote anayetaka kuligusua akiliunganisha na hilo la kukatiwa misaada kwamba ndio kisababishi, wote tunaimba wimbo wa kujitegemea. Nakumbuka Mbowe akiwa Denmark alitoa hotuba iliyo shiba sana na akaizungumiza hiyo hiyo misaada, aliponda sana, wengine walimlaumu sana na kuonekana haitakii mema Tanzania. Leo wale wale waliokua wakimponda Mbowe ndio hao hao wanaosema tujitegemee! Tusubiri KODI mbali mbali kuongezwa ili kufidia PENGO. Yetu macho,
 
Sijui ni kina nani ambao hawakuwahi kuandika kuhusu utegemezi. Mimi si mmoja wao. Msimamo wangu kuhusu misaada ya kigeni haujaibuka sababu ya MCC kusitishwa kama baadhi ya watu wanataka tuamini. Kama kuandika juu ya hili nimeandika sana na tena wazi kabisa. Sijabadilika msimamo wangu. Na wengine wanalizungumzia hili la MCC leo wakati wengine tulilizungumzia miaka sita nyuma! Hili la MCC limenipa tu sababu ya kuendelea na msimamo huo huo niliokuwa nao. Ushahidi wangu upo hapa:

Niliandika hili - STOP FOREIGN AID TO TANZANIA CAMPAIGN - hili ilikuwa Nov 19, 2008. Nikimjibu Mwalimu Augustino kwenye mada hiyo nilihoji hivi "Mwalimu ni kitu gani ambacho sisi wenyewe tunaweza kukifanya kwa uwezo wetu na fedha zetu wenyewe. Unafikiri misaada ya kigeni??? imetusaidia kuendelea na kiwango cha maendeleo kinaakisi misaada tuliyopokea hadi sasa?"

Niliandika hili -ARE WE ADDICTED TO FOREIGN AID? - hii ilikuwa Feb 17, 2009. Nikaandika hivi mle "Alas! May the truth be told, as a nation we can only function at least semi-effectively as long as there is this constant flow of foreign through the veins and capillaries of Tanzania, without which we will collapse like pieces of cookies in a milk jar! We depend on this drug, we beg for it, we long for it, we sing with high pitched voices, screaming and rukarukaring like kids in a candy store. Whenever we are promised that there is some more coming we smile so wide and our eyes get teary with joy! Our desires are stirred like a man tempted by that midnight temptress in the fortress of passion! "

Katika mada iliyoanzishwa na Mzalendo Halisi Cutting Off Aid - A Condition to lift Africa from Poverty - ya Feb 24, 2009 nilichangia na kuhoji ifuatavyo: "najiulizana sana kwamba endapo misaada ya kigeni itasitishwa:

a. tutaendelea kuwa na NGOs nyingi hivi?
b. Je watanzania wanaweza kujitolea fedha zao kufanya kazi za kujitolea?
c. Itakuwaje kwenye misaada ya visima iliyoanzishwa na fedha za wahisani, tutamudu kuiendeleza?
d. Vipi kuhusu miradi mingine inayosapotiwa na wahisani nayo itakuwaje?"


Nikaandika mada nyingine WAFADHILI MMEIDEKEZA TANZANIA, BADO TUNATAKA NYONYO - hii ilikuwa ni mada ya Feb 26, 2009. Niliandika mle jambo hili "Ninachosema ni kuwa, wakati wa kutukatisha kunyonya umefika. Tayari tuna wasomi wa kutosha, tuna raslimali ya kutosha, tuna watu wa kutosha na tuna sababu za kutosha kujitegemea. Lakini zaidi ya yote tunaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa katika kujiletea maendeleo. Hadi hivi sasa ninachokiona ni importation of development ambapo kile tunachokiita "maendeleo" kwa kweli ni vitu tulivyocopy and paste kutoka ng'ambo! Juzi nilimsikia Waziri Mkuu akitaka watu wanunue vitunguu vya Tanzania!!! Yaani kwa maneno mengine Tanzania inaagiza hadi vitunguu kutoka ng'ambo ambayo wenyewe tunaviona ni 'bora'!" Na watu wananituhumu sijaandika kuhusu "kujitegemea"!

Niliandika tena muda si mrefu baadaye hili RAIS MWENYE MAWAZO YA KUOMBAOMBA - Hii ilikuwa Aprili 9, 2009 Nilikuwa nainukuu hotuba ya Rais na nilitanguliza kusema hivi kabla ya hotuba yenyewe "Sehemu ya hotuba ya Rais Kikwete inayothibitisha kuwa hana mawazo ya kuinua hali ya maisha ya watanzania bila ya kukinga mikono kwa nchi matajiri; asilimia 99 ya mambo anayotaka nchi matajiri zifanye kwa Afrika yanaweza kufanywa na Afrika wenyewe!"

Hiyo ni mifano tu ya nilichokisema na kukiandika humu kuhusu fikra zangu juu ya misaada ya Kigeni; kuna tofauti yoyote na nilichosema leo? Na nimeandika vingi vingine kwa mfano,

Niliandika hivi juu ya MCA ambayo ndio ilikuja mwanzo kabla ya kuwa MCC. Ni katika mada ya SYMBION POWER ACQUIRES DOWANS POWER PLANT

"tatizo liko toka mwanzo tulipokubali kuwa sehemu ya hii MCA. Wengi walifikiria kuwa MCA ina lengo la kutupa sisi uwezo na kujenga uwezo wetu wa ndani la hasha. Masharti ya MCA kama yalivyo masharti ya miradi mingine mingi tu ya Wamarekani ni kuwa fedha za walipa kodi wao ni lazima zinufaishe Marekani. Sasa mimi siwezi kuwalaumu kwa hili. Fikiria dola milioni 700 zinaweza kufanya nini Marekani? Kweli tulifikiria Wamarekani watatoa hizo milioni 700 kwa Tanzania bure tu? Kwa undugu gani?"

Na nikaongeza na kusema,

Hatuwezi kuwalaumu. Kama tungekuwa tunataka kweli iwe ni misaada ya kutunufaisha na sisi watawala wetu wangesema mapema kwenye masharti kuwa kwa kila dola moja inayopelekwa Marekani dola nyingine moja ibakie Tanzania. Lakini hatuna sera ya misaada ya kigeni Tanzania hivyo tunakuwa katika huruma ya wale wanaotoa misaada na hatuwezi kuwalaumu. Kwa wananchi wa kawaida kwa kweli hiyo haiwajalishi maana kama serikali yao imeshindwa kutatua tatizo la nishati na Wamarekani kwa kutumia fedha zao, na makampuni yao wanakuja kusaidia why not?

Sasa leo naambiwa ati sijawahi kuandika juu ya hili; na nina uhakika licha ya kuweka rekodi yangu wazi kuwa sijabadilika kama inavyodaiwa wapo wengine wanaweza wasikiri kuwa "kweli mwanakijiji msimamo wako haujabadilika juu ya misaada ya kigeni". Watajaribu kuuelezea kwa kunilazimisha nizungumzie masuala ya Zanzibar kwa mitazamo yao.

Mwaka 2003 - zingatia kuwa nimesema yale yale tangu 2008! niliandika mada iitwayo
Stop unscrupulous Foreign Aid to Tanzania campaign towards 2015. Niliandika hivi mle:
What would happen if we were to initiate such a campaign to demand that foreign aid ought to be halted until a new policy on solicitation of the same is put in place? Unafikiri CCM na serikali yake watafanya nini kampeni hiyo ikianza?

Je wrwe kama Mtanzania utaathirika vipi na usitwishaji wa misaada hiyo? Je kama kuna misaada kweli inahitajika ni ipi na kwa maeneo gani au kwa muda gani?

Unafikiri tunaweza kupiga hatua ya haraka ya maendeleo bila misaada ya kigeni?


Sasa ni kweli nimebadilika? Ni kweli sijazungumzia kuwa huru kutoka misaada ya kigeni? Ni kweli msimamo wangu wa leo unatokana na matukio ya juzi ya uchaguzi? Au ni msimamo unaotokana na kuthibitika katika kanuni ninazozisimamia. Mtu anayesoma anaweza kuamua mwenyewe bila kuongozwa na hisia za kisiasa au kisasi au kutotaka kuwa mkweli au kuogopa kusema "mwanakijiji yuko sahihi" kwa sababu ataonekana anakubaliana na mtu ambaye hakudandia mabadiliko yale feki!

Naendelea kuamini kusitishwa MCC iwe sababu tu ya kutaka kuondoka na misaada hii ya kitegemezi ya kigeni ambayo imetufanya tuwe watu tusiojiamini, wenye mawazo ya kubembeleza na ambao tuko tayari tufanywe lolote ili mradi dawa hii nzito ya kulevya iingie kwenye damu zetu!

Nitaendelea kupinga misaada ya kigeni ya aina ambayo tunapokea sasa hadi tutakapokuwa tayari kuwa na ushirikiano wa kigeni ambao msingi wake ni heshima, utu, kusaidiana na kuinuana. Na kabisa napinga misaada ya kigeni inayoingizwa kwenye bajeti ya nchi moja kwa moja au ile ambayo inakuja nje ya maeneo yale matatu niliyoyaanisha katika ile mada nyingine. Katika hili inawezekana nimebakia "mimi tu, mimi kuwaletea habari"

MMM
juzi japan nao wametugea bilions kama 116 hivi hizi safii eeh....
 
Back
Top Bottom