Kinachoendelea Twitter (X) kuhusu maoni ya watu juu ya Waraka wa TEC ni upuuzi mtupu

Kinachoendelea Twitter (X) kuhusu maoni ya watu juu ya Waraka wa TEC ni upuuzi mtupu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Huu waraka naona umewashika pabaya mno na ni wazi hawana pa kutokea! Si waraka mbaya umesheheni ushauri na tadhahari kwa maslahi ya Watanganyika wote bila kujali imani, itikadi wala asili zao.

Ni waraka usio na chembe ya udini wala itikadi za kisiasa.. Umetembea kwenye mstari wa katiba na sheria za nchi. Ni mkataba uliozingatia kwa asilimia 100 uzalendo, ustawi, utu na urithi wa taifa hili na tunu zake kwa vizazi vya sasa na vijavyo.. Lakini nyuma yake kuna mamlaka inajaribu kuukwamisha kwa kutengeneza watu wasiojitambua kuuhuisha na dini na maisha binafsi ya watu.

Wametengezwa watu wanaohojiwa na kutoa maoni yao. Yaani ni vituko na upuuzi mtupu.. Mpaka unaona kabisa hata huyo aliyewatengeneza akili zake hazina akili kama wao.

Inawezekana kabisa kuna kitu kikubwa zaidi kibaya zaidi cha kuogofya zaidi kuhusiana DPW na Bandari zetu za Tanganyika. Maana baada ya waraka kutoka JK kaibukia huko kwa Wasabato na kutoa nasaha zake zilizoacha maswali mengi kuliko majibu

Mama naye ni mwalikwa huko KKKT sijui atasema nini. Lakini unaweza kutabiri. Chama cha mitume na manabii eti nao wametoa waraka wao unaoupinga wa TEC.

Hizo mbinu zote ni namna ya kutaka kuwatenganisha watanganyika na waraka wa TEC na kutaka kuonesha waraka huo ni wa kikundi cha watu wachache wenye malengo yao mabaya.

TEC hawajakurupuka na hawatajibu mapigo kwakuwa wanajua kwa hakika wanachokifanya na waraka husika utaendelea kusomwa kwa wiki sita mfululizo bila kukoma mpaka hata asiye na masikio ya kusikia kama kenge asikie.

Hii panic ya kijinga ya kutafuta watu mitaani waupinge waraka haitafika popote. Wasabato, KKKT, Pentecost BAKWATA na wengine wote unganeni na TEC kwenye hili mwisho hauko mbali

Umoja wetu ndio mtaji wetu
Mungu ibariki Tanganyika
Mungu wabariki Watanganyika

20230821_072314.jpg
 
Mjumbe hauawi. Huyu katumwa na mamlaka yake aseme walichoamua . sasa lawama zinatoka wapi?
Tarehe 25 December 2017, Askofu Zakaria Kakobe akiwa kanisani kwenye ibada ya Christmas, katika kanisa la FGBF Mwenge jijini Dar es Salaam, alinukuliwa akituma salamu kwa Rais wa JMT, Dkt. John P. Magufuli.

"Rais John Pombe Magufuli, nawe unatakiwa kutubu leo. Unaposherekea sikukuu ya Christmas, ili uridhiwe na Mungu unatakiwa nawe utubu".

"Leo ni siku ya watawala wa Tanzania kutubu. Leo tumeanza kuona misingi ya amani ya nchi yetu ikitikiswa. Amani iliyojengwa kwa gharama kubwa na waasisi wetu. Tumeanza kuona nchi hii ni ya chama kimoja na huu ni uovu. Mungu mwenyewe anaheshimu sheria basi kama na sisi tumeweka sheria tunapaswa kuheshimu sheria tulizojiwekea wenyewe. Hii si nchi ya chama kimoja. Kama mnataka kubadilisha si mbadilishe tu mara moja kupitia wabunge wenu wa CCM, si mko wengi?".

"Sheria ni lazima zizingatiwe! Na kwa hili nitapiga kelele mpaka Mlima Kilimanjaro. Huwezi kusema wewe huwezi kusemwa, wewe ni nani? Mungu anasemwa vibaya sembuse wewe?".

"Mungu mwenye nguvu kuliko Magufuli, ana nguvu kuliko majeshi yote ya nchi, lakini anatukanwa na bado hatumii majeshi yake. Hata wewe unaweza ukawa mvumilivu"

Baada ya kauli hii, Askofu Kakobe alipokonywa passport yake, alihojiwa uraia wake na aliandamwa na TRA kwa madai ya kodi.

Huyu alikuwa ni kiongozi wa dini ya Kikistro na alimkosoa Mkristo Magufuri

Huu ulikuwa udini? Wa dini gani?

Askofu wa Catholic Jimbo la Rulenge (Severine Niwemugizi) alimkosoa mkatoliki mwenzake Magufuri juu ya haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano.

Aliishia kupokonywa passport na kuhojiwa uraia wake.

Alikuwa mdini? Akishabikia dini gani?

Nachukizwa sana na yeyote ambaye atataka kutugawa kwa misingi ya kidini.

Kukosoa haiwezi hata mara moja kuwa udini.

Kuwa kiongozi wa dini hakumnyimi haki kiongozi huyo kupata haki zake za kikatiba kutoa maoni juu ya mambo ya nchi yake kama anavyoweza kufanya Mwalimu, daktari, mkulima au mfugaji.

Tukemee wale wote wanaotaka kujificha kwenye udini pale tu wanapokosolewa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.

Mungu Ibariki Tanzania na watu wote.

Uhuru, Umoja na Amani

From your commander of the hand to mouth battalion

A dull, Colorless and Clueless old man now chewing Mugombero the turbo charger

Credit: Fortunatus Buyobe
20230821_075738.jpg
 
Tatizo Taifa letu lina watu wa hovyo sana, wana reasoning capacity ndogo na wengine wapo kwenye utawala. Kuna watu ukiwasikiliza mpaka unajiuliza huyu ana akili kweli na alifikaje hapo alipo au anafanya makusudi.

Wengine ni wanafiki, wabinafsi na wenye kuendekeza masirahi binafsi. Hotuba za Mwalim zilikuwa zipo sahihi sana na aliyaona haya yanayotokea leo. Kuna watu wapo tayari kufanya chochote ilimradi tu umemlipa bila kuangalia athali zitakazotokea siku zijazo, RUSHWA RUSHWA RUSHWA ni adui wa haki siku zote.
 
Tatizo Taifa letu lina watu wa hovyo sana, wana reasoning capacity ndogo na wengine wapo kwenye utawala. Kuna watu ukiwasikiliza mpaka unajiuliza huyu ana akili kweli na alifikaje hapo alipo au anafanya makusudi.

Wengine ni wanafiki, wabinafsi na wenye kuendekeza masirahi binafsi. Hotuba za Mwalim zilikuwa zipo sahihi sana na aliyaona haya yanayotokea leo. Kuna watu wapo tayari kufanya chochote ilimradi tu umemlipa bila kuangalia athali zitakazotokea siku zijazo, RUSHWA RUSHWA RUSHWA ni adui wa haki siku zote.
Hii imetoka kwa Getrude Mollel [emoji23]
20230821_080835.jpg
 
Mwijaku hana akili. Tunatetea wote bandari ibinafisishwe ile siyo kuwatusi viongozi wa dini au viongozi waandaminzi wa serikali wawe wamestaafu au wapo madarakani. Huyu kijana kajichumia laana!
Waraka utasomwa kwa wiki 6 mfululizo tutegemee mengi zaidi
20230821_080250.jpg
Hii Ayo TV ameshurutishwa kuifuta haipo tena
 
Ni maoni ya nani??

Getrude Hata siku ya mwisho mtu wa kwanza kukutupia udongo unamfahamu?

Je maoni ya ccm ni maoni ya watanzania?
Hebu msome vizuri hapa

Hapa Taasisi ambazo zina haki ya kusikilizwa kwenye suala la Bandari ni Bunge na Mahakama, sio taasisi yeyote ya dini wala kikundi chochote hapa nchini.

- Kwenye suala la IGA tayari Mahakama Kuu kanda ya Mbeya ilishatoa hukumu kwamba IGA haina tatizo na kubariki mchakato mzima wa uwekezaji uendelee.

- Tatu, Bunge la JMT limepitisha mkataba wa IGA kwa kuzingatia sheria za bunge na maslahi mapana ya Taifa letu.

- Kama suala la kitaifa la uwekezaji kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu mmeanza kulitia udini, basi niwaambia Mbegu mnayoipanda sio nzuri na kwa hakika, itawatokea puani siku si nyingi.
 
Mshana Jr nchi yetu inaongozwa kwa misingi ya demokrasia hivyo wanao uhuru wa kufanya hicho wanachofanya ila sisi tunaamini serikali itafanyia kazi maoni yote na mkataba kazima utekelezwe.
Ok asante sana kwa hili[emoji1545] lakini kama ni hivyo kwanini waandishi wachaguliwe cha kuandika?
 
Hii imetoka kwa Getrude Mollel [emoji23]View attachment 2723495
Kwa mwenye akili timamu inayofanya kazi kwa uhakika, huwez kupoteza mda kuhusu huyo kijana. Hata wakiuza Nchi hii atajitokeza nakukwambia ni sawa kwa sababu tumeshindwa kujiendesha., ni ujinga tu.

Mnufaika yeyote wa hizi Tawala za Kiafrica hawezi akaona kasoro ya aina yeyote, maana wamezaliwa kwenye mifumo hiyo, wakakulia humo mpaka wamepatiwa vibarua humo humo, unategemea wawe na mawazo gani chanya zaidi ya ujinga ujinga tu.
 
Tarehe 25 December 2017, Askofu Zakaria Kakobe akiwa kanisani kwenye ibada ya Christmas, katika kanisa la FGBF Mwenge jijini Dar es Salaam, alinukuliwa akituma salamu kwa Rais wa JMT, Dkt. John P. Magufuli...

Brother mshana hawa watu usihaingaike nao.... huwezi kubishana na mtu mjinga ukashinda, siku moja hawa hawa watakuja na kilio cha dp world kutupiga. Sio kama hawaelewi wameelewa na ujumbe umefika...

Hao dp world wangekuwa wema wangevunja mkataba na tz maana tayari hawatakiwi hapa!!! siku moja wote tutasema lugha moja
 
Back
Top Bottom