G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,795
- 36,704
Na huo ndiyo ukweli wenyewe. Mwana habari Erick Kabendera nje ya Tanzania ni mwana habari mwenye nguvu na mwenye uzani sawa na kina Jamal Khashoggi. Hayo mengine yalitokea yakapita kimya bila madhara makubwa. Wapo waliotekwa, wapo waliopotea, wapo walionusurika kuuawa, wapo waliouawa na wapo walionyang'anywa uwekezaji wao wa jasho na damu kwenye huu utawala wa John Pombe Magufuli. Hayo yote yalipita huku yakiangaliwa kwa mbali kidogo na subira.
Serikali ilikuja kujichanganya sana kumkamata mwana habari Erick Kabendera ambaye ni mwana habari anayehabarisha nje ya mipaka ya Tanzania, mwana habari aliykeuwa anatoa ukweli wote wa yanayoendelea Tanzania huko nje. Walijichanganya sana kumkamata na kumfungulia mashitaka ya uonevu na kubambikia.
Kukamatwa kwa Erick Kabendera kumetibua majeraha yote na sasa Tanzania ilianza kuchunguzwa kwa umakini zaidi na ndipo yanakuja haya.Na kusema kweli tutayavaa na si kwa Marekani pekee bali mlolongo wote wa mataifa ya NATO.
Mwana habari Jamal Khashoggi ambaye aliuawa kikatili ndani ya ofisi za ubalozi kwa kile kinachoelezwa kuwa alikuwa akimvua nguo kwa kumuandika mwana mfalme wa Saudi Arabia, mauaji yake yalileta sintofahamu kubwa duniani na kupelekea utawala wa Saudi Arabia kukosa imani kwa Marekani. Basi huyu Kabendera ni level zile zile za kina marehemu Khashoggi. Naamini kwa wale wanaoenda mahakamani kushuhidia kesi ya Kabendera na kuona wafuatiliaji wageni wa kesi hii tutakuwa pamoja.
Mashitaka dhidi ya Kabendera yataiponza Tanzania zaidi ya hapa!
Bahati mbaya sana na Nigeria nao wamekumbwa na tukio hilo hilo baada ya wao pia kujiingiza ku deal na mwanahabari nguli Omoyele Sowore. Nigeria wana ugaidi wa kila aina, wana matapeli duniani hakuna na yote haya wameyafanya kwa miaka mingi iweje leo? Ukitaka uhasama na dunia iliyostaharabika basi wabughudhi waandishi wanaoonekana ni threat kwako kama wewe ni mtawala.
Serikali ilikuja kujichanganya sana kumkamata mwana habari Erick Kabendera ambaye ni mwana habari anayehabarisha nje ya mipaka ya Tanzania, mwana habari aliykeuwa anatoa ukweli wote wa yanayoendelea Tanzania huko nje. Walijichanganya sana kumkamata na kumfungulia mashitaka ya uonevu na kubambikia.
Kukamatwa kwa Erick Kabendera kumetibua majeraha yote na sasa Tanzania ilianza kuchunguzwa kwa umakini zaidi na ndipo yanakuja haya.Na kusema kweli tutayavaa na si kwa Marekani pekee bali mlolongo wote wa mataifa ya NATO.
Mwana habari Jamal Khashoggi ambaye aliuawa kikatili ndani ya ofisi za ubalozi kwa kile kinachoelezwa kuwa alikuwa akimvua nguo kwa kumuandika mwana mfalme wa Saudi Arabia, mauaji yake yalileta sintofahamu kubwa duniani na kupelekea utawala wa Saudi Arabia kukosa imani kwa Marekani. Basi huyu Kabendera ni level zile zile za kina marehemu Khashoggi. Naamini kwa wale wanaoenda mahakamani kushuhidia kesi ya Kabendera na kuona wafuatiliaji wageni wa kesi hii tutakuwa pamoja.
Mashitaka dhidi ya Kabendera yataiponza Tanzania zaidi ya hapa!
Bahati mbaya sana na Nigeria nao wamekumbwa na tukio hilo hilo baada ya wao pia kujiingiza ku deal na mwanahabari nguli Omoyele Sowore. Nigeria wana ugaidi wa kila aina, wana matapeli duniani hakuna na yote haya wameyafanya kwa miaka mingi iweje leo? Ukitaka uhasama na dunia iliyostaharabika basi wabughudhi waandishi wanaoonekana ni threat kwako kama wewe ni mtawala.