Kinachonipa hofu mechi ya Yanga, ni wachezaji kutokuwa pamoja kambini hivi karibuni wakitumikia timu zao za Taifa kufukuza Fainali za Kombe la Dunia

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza, hii ndio hofu yangu kwa mechi ya leo kwani baadhi ya wachezaji wetu wa humu ndani na wale wa kimataifa, walikuwa wanatumikia timu zao za Taifa katika kusaka nafasi ya kushiriki kombe la Dunia mwaka 2026.

Sasa sijui wamekaa kambini kwa siku ngapi ingawa bado nina imani na kikosi chetu kwa ujumla.

Mungu ibariki Yanga.
 
Uzuri waliokuwa na timu za Taifa ndio wenye faida kwa sababu wana mechi fitness kuliko waliotangulia.

Mpira wa kisasa ni mfumo tu na approach ya kocha ndio vinaleta matokeo.

Ondoa shaka Yanga inabeba point 3 muhimu, au kupoteza kwetu ni sare tu.
 
Visingizio vya nini wakati tunasubiri muwapige Tano
 
Uzuri waliokuwa na timu za Taifa ndio wenye faida kwa sababu wana mechi fitness kuliko waliotangulia.

Mpira wa kisasa ni mfumo tu na approach ya kocha ndio vinaleta matokeo.

Ondoa shaka Yanga inabeba point 3 muhimu, au kupoteza kwetu ni sare tu.
Umemaliza ,siku nyingine naomba uwafundishe watu humu mpira unakuaje
 
Tuko pamoja kwenye hili mkuu
 
Kimpira hkn tatizo
 
Wasi wasi ndo akili...fanya fasta kapande ndege ukasimamishe mafuriko ya magoli uko nenda kaforce gemu isicheze lasivyo utavaa kinyago kesho usubuhi
 
si Yanga Tu, hata hiyo Timu ina hali kama hiyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…