Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

Watoto wanakaa chini angali mapori yametuzunguka...
Miaka 54 ya uhuru!
Tunahitaji mabadiliko
 
Tehe! Tehe! Tehe! UCHAGUZI Ukimalizika, Watu Waporejea Ktk. Maisha Yale Yale Ya Kila Siku!! Sipati Picha!!!
 
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana, ameanza ziara ya kampeni katika majimbo 64. Vilevile, viongozi wengine wa CCM, akiwemo Rais na Mwenyekiti wa CCM Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa, nao wataanza safari za kuzunguka nchi nzima kumuongezea kura Dkt. Magufuli na wagombea wetu wa Ubunge na Udiwani.
Huwa nahisi kwamba Magufuli alikuwa ni chaguo la Mkapa ...
 
Mwisho Wa Yote Ni 25 Oct. Tu!! Pale MWAI KIBAKI Wa Tanzania Akiwa Tayari Kuingia White House Kuleta MABADILIKO!!! Hongereni Kwa Kupata Kazi Ya Nape Nnauye!!!
 
kwa kweli kwa upande wa vikosi kazi na organization ccm wako vizuri kuliko UKAWA.nawashauri ukawa ndani ya hizi wiki mbili zilizobaki waingize field vikosi vitatu kimoja kiongozwe na LEMA kingine kiongozwe na mbowe au lissu na cha tatu kiongozwe na mdee. wakichelewa wameliwa. hongereni sana ccm...




Umsahau kuwa Baraza la mawaziri halijavunjwa.
CCM wanafedha nyingi na raslimali za kufanya kila aina ya kampeni kwa kutumia madaraka na kofia za uwaziri.
Wanauwezo wa kuchota fedha popote.
Subiri uone kama Mungu atasikia kilio cha wanyonge na kuwaangusha hao CCM jinsi watu watakavyokumbwa na makashfa kama yale ya EPA. Jiulize ni kwa nini pesa ESCROW ziliingia kwenye mifuko ya watu wa ukanda fulani na mgombea wao ametokea wapi?
CCM hata aje Obama kuwaombea kura hawataingia madarakani.
Awamu hii ni Lowasa.
Awamu ya Tano ni ya Edward.
Kumbuka Sita na Membe walijipanga sana lakini kwa uwezo wa Muumba walisambaratika na kuyeyuka kama bonge la barafu kwenye joto kali.
 
hiyo namba tano haitekelezeki. rejea sheria mliyopitisha ya cyber crime na nyingine nyingi zenye maslahi kwenu. jambo jingine kubwa litakalowabwaga ni kuua katiba ya wananchi.
 
Timu ya magufuli ni hatari. Unapo ambiwa hapa kazi tu kaa mguu sawa wananchi,,kupata maendeleo na john pombe magufuli
 
magufuli ameunda jopo akiwa kama nani?
Na jopo hilo kitafanya uchunguzi kwa mujibu wa sheria gani?
Kwa nini mnamhadaa jk kama vile hakufanya kitu?kwa nini mnapotosha watu?
Ndugu mtanzania tii kiu yako kata ccm
 
Nimesoma taarifa ya January Makamba akieleza Rais mtaafu Benjamin Mkapa ataingia kuongeza nguvu ya katika Campaign za Maghufuri.
Je kuingia kwa Mkapa kutaleta mabadiriko kwa wapiga kura?au CCM imeishiwa pumzi?

Hii ni dalili tosha kuwa CCM imeishiwa pumzi na ipo katikati ya mlima na uwezo wa kubadili gia haupo huku dereva akiwa anapiga push up akidhani atainusuru na zahma inayoikabili.
 
Mlisema wazee hawachezi chandim. Naona kweli maji yako puani na mwaka huu hamchomoki.
 
kwa kweli kwa upande wa vikosi kazi na organization ccm wako vizuri kuliko UKAWA.nawashauri ukawa ndani ya hizi wiki mbili zilizobaki waingize field vikosi vitatu kimoja kiongozwe na LEMA kingine kiongozwe na mbowe au lissu na cha tatu kiongozwe na mdee. wakichelewa wameliwa. hongereni sana ccm...
We unaonekana hata mke wa rafiki yako unamsifia kuliko wako. Ukisikia jambo dogo tu linakupeleka puta sana
 
Back
Top Bottom