Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

Naona CCM kweli mmechokwa....hahaha.
Mpaka mnamtumia Lowassa kama njia ya kuwavuta wasomaji.
 
Wameanza kuangalia wanajipanga vipi ikitokea wanashin dwa uchaguzi. Wasipo jipanga sasa,chama kitakufa na makada wengi watakufa kwa kasi ajabu kwa sababu ya ukata na kukosa mada raka.
 
Dkt. Magufuli amelipa jopo hili majukumu yafuatayo:

1. Kuchunguza na kupendekeza maeneo ambayo Serikali itabana matumizi, ikiwemo manunuzi ya umma, posho za vikao na matumizi ya magari, ili atoe maamuzi kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa;

2. Kuchunguza na kupendekeza maeneo ambayo Serikali itaongeza mapato mara moja bila hatua za kibajeti kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa;

3. Kuchunguza na kupendekeza maboresho makubwa katika mfumo wa utendaji na utumishi na ufanisi katika Serikali;

4. Kupitia kodi na ushuru wenye usumbufu kwa wafanyabiashara wa ngazi zote, wakulima, wafugaji na wavuvi iwapo unaweza kurekebishwa bila kuathiri bajeti ya Serikali inayotekelezwa sasa.

5. Kupitia sheria zote za nchi na kuorodhesha Sheria ambazo zinapaswa kubadilishwa haraka ili kuharakisha mabadiliko ya kweli na ya haraka ambayo ameyaahidi kwa Watanzania;

6. Kupitia na kuorodhesha masuala yote na kero zote zinazosubiri maamuzi ya Serikali ili atoe maamuzi kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa.

7. Kupendekeza miundo na idadi ya Wizara na kutengeneza rasimu za mikataba ya kazi kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu na watendaji wengine wakuu atakaowateua mara baada ya kuapishwa.

8. Kupendekeza njia za haraka za kumaliza kero za watumishi wa umma, hasa walimu, askari, madaktari na wauguzi, ili aanze nao kazi wakiwa na ari na morali ya kusukuma mabadiliko ya kweli.

9. Kutengeneza rasimu ya mpango-kazi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM na ahadi alizozitoa kwenye kampeni, hasa upatikanaji wa ajira kwa haraka na umeme wa uhakika;

10. Kupendekeza muundo wa kitaasisi na utaratibu muafaka wa kutekeleza ahadi ya kutoa shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na mtaa nchini.

Dkt. Magufuli ameazimia kuanza kazi mara moja kwa bidii kubwa na maarifa mapya.


Imetolewa na:-

January Makamba
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa
Mjumbe wa Kamati ya Kampeni

Mabaliko.... lowasa .magufuli.... uwiiiiiiiiii...
 
Hayo ni maandalizi mazuri. Hakuna sababu ya kupoteza muda baada ya uchaguzi. Wananchi wanakiu ya mabadiliko. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Miaka 50 walikua wanaishi wapi? Mnadanganywa kama watoto, mnachekelea...umeshajiuliza hilo jopo lake nani analilipa? Kwa pesa zipi? Wenye ajira siku nyingi kama waalimu mishahara yao ni shida, hawa wengine wanaajiriwa kwa kanuni zipi? Au ndo udikteta wa madaraka yasiyo na mpaka? Rais wake bado yupo, haoni ni kumdharau? Siasubiri amkabidhi ofisi ndo aanzie hapo? Yani Watanzania.. Dah Mungu tu awasaidie.
 
Mkuu lakini Mh.Magufuli hatumii chopa.

Hata wewe mwenyewe hujui kinachoendelea unapelekwa tu kiushabiki...chopa 4 zimepangwa kutumika, na mgombea atatumia itakapomlazimu. Kwahiyo ccm halali, wengine haramu.
 
Acha kusema takataka wewe,matokeo ya urais minimum mda wa kutangaza ni masaa 72.sasa wewe sijui utakua unashangilia matokeo yapi???
Wewe ni mpumbavu na lofa! Mbona huulizi EL anaposema kuwa ushindi utapatikana mapema tarehe 25/10/2015?
 
Ndg Wanajamii,

Jana na leo vyombo vya habari vimejinasibu na habari ya Mgombea wa CCM ndg Magufuli kuteuwa jopo la wataalamu kwa ajili ya mchakato wa kumwezesha kutenda kazi vizuri akiwa ikulu. Kwa taarifa za kweli na rasmi ni propaganda tu, hakuna kitu kama hicho, ni mbinu tu ya wapambe kuona kama gia hiyo inaweza kuwaingia wananchi na kuona kama kweli inalipa kama ile ya tafiti za TWAWEZA kubuma.

Wakati Makamba anatangaza hayo kwa wandishi wa habari, alishindwa kubainisha wabobezi hao wametoka katika taasisi zipi na lead consultant ni nani? Ndio maana mambo muhimu hayajabainishwa katika ushauri wao. Pia mambo mengine kama Mishahara kwa utumishi wa umma uko wazi na kuna sera na tume maalum sasa ya kusimamia mishahara.

Ni vema UKAWA KUCOUNTER ATTACK MARA MOJA Propaganda hii.
 
kwenye tarehe umekosea kidogo, ni asubuhi na mapema ya tarehe 25/10/2015 mheshimiwa edward ngoyai lowassa atakuwa ameshatangazwa mshindi, maana kura atakazozipata kwa muda wa lisaa limoja tu baada ya zoezi kuanza hamna mgombea mwingine atayefikia robo yake. Lowasssssssssssssa
Piga hesabu ya saa vizuri! Uchaguzi unafanyika tarehe 25 kuanzia saa2 hadi 10. Baada ya hapo wanahesabu kura. Mwisho wa siku ni saa6 kamili usiku. Kuanzia saa 6.01 ni tarehe 26/10 ambapo ni siku nyingine na siyo asubuhi na mapema 25/10 kama unavyodai wewe! #Hapakazitu
 
Unafikiri Lowassa akishika nchi vitu vyote vinafutwa? Au yeye anaanza na watumishi wapya kila sehemu!

Nilijua analipwa pension kwa propaganda zake, kama ni mstaafu haina haja kubishana, kwanza huna changamoto za kimaisha kulingana na umri wako pia vyema ungetuacha vijana tufanye ya kwetu labda yatakuwa bora maana yenu nyinyi mlifanya ndio yametufikisha hapa.
 
Yeah: 1%Words 99%Actions. Lowassa.
Kabisa....Mungu akikupa nguvu akakunyima hekima utampiga hadi mamako...ndo ya ccm...wanapiga makofi mama zao bila haya na wanashangilia kwa push ups majukwaani.

Ivi kweli kwa hapa tz ilipo unahitaji kuunda jopo la kuchunguza vitu wakati umetawala for 50 worse years?

Nani anamshauri huyu MTU?

Hilo jopo linalipwa na nani kwa pesa gani?

Hizo milioni 50 zinazogawiwa kama Katanga zinatoka kwenye mfuko gani?

Vifo vya wajawazito na vichanga, albino na wazee...vitawahukumu!

Raisi bado yupo ofisini, kwani hana nyaraka za kumkabidhi zenye taarifa ya mafanikio na changamoto? Haoni ni tusi kwa serikali? Anaharaka ya nini?

Inasikitisha nchi ikiongozwa bila hekima!

Na tunapata tabu kwasababu wenye hekima ni wachache kuliko wasio na hekima ambao wanashangilia huu upuuzi.

Lowasa kapewa hekima, sio nguvu. Mungu amsimamie!

Mungu ikumbuke tz.

Nadhani kilichobaki sasa ni maombi tu!
 
Back
Top Bottom