Kinana atofautiana na Chongolo mkataba wa bandari

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mzee Kinana ametofautiana msimamo na Katibu Mkuu wa CCM kuhusu mkataba wa bandari.

Kinana anasema wamejitokeza watu wameanza kuhoji, wako wanaohoji kwa nia njema ya kujenga ya uzalendo, hatuwezi kusema kila anayehoji anania mbaya, wako wanaotetea mkataba na wametoa ushauri mzuri, serikali imesema itapokea kila ushauri utakaotolewa, Chama Cha Mapinduzi kimesema serikali isikilize, kwa hiyo serikali inasikiliza ushauri, inasikiliza hoja, haya yote yatafanyiwa kazi, haiwezekani Rais akapuuza haya yote.


Lakini Chongolo yeye anasema Serikali ianze utekelezaji haraka na isisikilize kelele za wajinga wanaopinga mkataba huo.

 
Ana kabachela ka hivi vyuo vya mchongo ( Open university).
Hivi huyu Chongolo ana elimu gani au naye ni zile design za kina Sofia Mjema......!!?
Kithibitisho tosha kua ni mwenye matope kichwan.



Yaan hii CCM ya Samia, Anza na Samia mwenyewe, Njoo Nape, January, Chongolo, Akina Mwana FA.. , Hawa ni wamichongoooo tupuu


Vichwani ni Vitunguu maji !!.
 
Mhe Kinana anahofu ya Mungu na anapenda uadilifu apewe maua yake.
 
Ndugai je?
 
Angalau kwa kusoma alama za nyakati
Kujisahihisha ni Bunge kurudi na kufuta maadhimio yake, mchakato uanze UPYA Kihalali.

Kutuambia kuwa mkataba utarekebisha vifungu tata, ilhali mkataba Hauna chance kurekebishika ni hadaa.

Warudishe pesa za wenyewe kama walihongwa, Mkataba ufutwe, na mchakato uanze UPYA.
 


Hivi kweli CCM haina hazina ya Viongozi mpaka wanakuwa na mtu kama Chogolo
 
Hakuna uwezekano hao wawili wakapingana kimantiki. Upotoshaji ni sifa yenu kuu lakini mwisho wenu kwenye suala hili sio mzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…