Kwintara Kwinyira amezindua kampeni yake (Social media campaign) ya kupinga UKUKU nchini. UKUKU means Umoja wa Kukubali kila kitu bila Kuhoji. Kuna watu kazi yao ni kuunga mkono kila kitu ili mradi kimesemwa na kiongozi wake.
Tabia hii imeshamiri sana kwa wafuasi wa CCM. They dont reason at all. Ila mradi kiongozi kasema wao ni NDIOO.
Godbless Lema anasema tatizo sio wao, tatizo ni akili zao. UTG wanaita huo ni uzwazwa, lakini Kwinyara anasema ni UKUKU. Kukubali kila kitu bila kuhoji ni UKUKU.
Watu walewale waliosema JK aongezewe muda, kwa kuwa amesaidia sana taifa, ndio haohao wanaokazana sasa JPM aongezewe muda na kusema JK aliharibu nchi. UKUKU.!
Watu walewale wanaoshangilia viongozi wa upinzani wakikamatwa kwa kufanya mikutano ya siasa, ndio haohao wanaoshangilia CCM ikifanya mikutano. UKUKU.!
Watu walewale wanaopitisha mrabaha wa 04% kwa makofi na kusema unatosha, huku wakiwazomea wapinzani waliposema hautoshi, ndio haohao wanaoshangilia kufikishiwa 06%. Mnashangiliaje kupandishwa kwa kitu mlichosema kinatosha? UKUKU.!
Na kwa sasa wapinzani wanasema 06% hazitoshi, wao wanasema inatosha. Akija Rais baada ya JPM akaziongeza tena watashangilia na kumuita mzalendo. UKUKU.!
Watu walewale walioshangilia Ngeleja kurudisha hela TRA ndio haohao wanaoshangilia TRA kuzikataa. UKUKU.!
Walioshangilia JK aliposema pesa za Escrow si za umma, ndio haohao wanaomshangilia JPM kusema pesa zilikua za umma. UKUKU.!
Nchi hii imeharibiwa na hawa KUKU. Kila kitu wanakubali tu bila kuhoji. Kataa UKUKU, kataa kuwa KUKU, kataa viongozi MAKUKU.!
U = Umoja wa
KU = kukubali kila kitu bila
KU = kuhoji.
Tuma kwa watanzania wengi kadri uwezavyo, wajue KUKU wanaoharibu nchi yao. Tusiwaachie kuku nchi yetu. Kataa UKUKU kwa nguvu zote, kataa kuwa KUKU, kataa viongozi MAKUKU.!