Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mnafahamu sheria na katiba inasemaje? Hapo angewashtaki mngesema anavunja katiba na dikteta. Uwezo mdogo
Watafungwa vidagaa mapapa watalindwa kwa gharama yoyote.Nchi itatikisika.
Anamaanisha atawalinda kwenye maovu yao yote ya ufisadi walipokuwa madarakani. Kama utakumbuka Salma Kikwete na Ridhwan ni shareholders wa UDA ambayo imekwapuliwa kinyemela kutoka halmashauri ya jiji la Dar na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali katika ripoti yake ya mwaka aliandika kuhusu ufisadi huu. Jamaa kaamua ile ripoti iendelee kupigwa na vumbi pale Ikulu ili kuendelea kuwakingia kifua wakwapuzi wa shirika la UDA, na huyu ndiye aliyejinadi kwamba kajitoa kafara ili kupambana na ufisadi nchini.
kama ana kashfa nzito kwa nini sasa hawampeleki mahakamani? ina maana hizi mahakama tulizonazo haziwezi kusikiliza tuhuma zake mpaka iunde mahakama maalum ya mafisadi? na hao majaji watakuwa ndio hao hao wa mahakama za sasa au na wao wataagizwa toka nje ya nchi ili kuleta utofauti?Lowasa ana kashfa nzito sana ya ufisadi wa Richmond...mahakama ya mafisadi itaanza nae
Mkuu namba ilishasomwa, imebaki kuiandika na kuikariri tu.Hivi mlivoambiwa CCM ni ile ile inamaana hamkuelewa?
Ndo hivo sasa.... mmeipenda wenyewe, chaguo lenu wenyewe.....
Kilichobaki ni kuisoma namba tu
Lowasa ana kashfa nzito sana ya ufisadi wa Richmond...mahakama ya mafisadi itaanza nae
Amen!!!. Pia Yesu atakuja kuvunja falme zote hizi za ulimwneguni na kusimamisha falme yake moja milele!Mwenge kutenda haki ni Mungu peke yake. Hawa W engine ni wasanii tu ndiyo maana mhubiri anasema ni ubatili mtupu chini ya jua
Mahakama haiwezi kuwepo kisha izikwepe kesi hizi watu waikubali . 1- zile bilion 252 zilipotea Wizara ya Ujenzi Kwa kuwalipa makandarasi hewa , 2- Ununuzi kivuko chakavu cha mwaka 1978 Kwa bilion 8 cash , 3- Mabehewa Feki ya mwakyembe na gharama halisi za Ukarabati wa reli ya tren ya mwakyembe na ile reli ya kati na ufisadi bandarini pia Ujenzi uwanja wa ndege. 4- Chenji ya Rada na Chenji Bunge la katiba -5- pesa za NIDA na mali na Mabilion ya marehemu Gadafi yaliyofichwa na Membe -6- NSSF ufisadi kwenye miladi yote likiwemo daraja la Kigamboni -7- TTCL , ATC waliozifirisi mpaka kufikia zilipo sasa, -8- Madili ya sukari yanayofanyika sasa pia hiyo pesa inayotumika kumpatia Lipumba avuruge CUF nayo ni ufisadi , haiwezekani kwenda kumpatia Lipumba pesa afanye pumba wakati kuna wagonjwa kibao wanateseka pasipo kupata Dawa wala msaada . Yapo Madili mengi sana lakini hiyo Mahakama bila hizo kesi haitakuwa na maana tena."Sioni umhimu wa mahakama ya mafisadi Tanzania, kwakuwa naona hadi sasa hakuna nia ya dhati ya kutenda haki katika mahakama hiyo ya mafisadi, hii imetokana na Mh Rais John Pombe Magufuli kunikosesha imani kupitia hotuba yake jana"
Rais anaposema atawalinda marais wastaafu anamanisha nini? Hii ina maana hata kama watathibitika kuwa marais hao ni mafisadi Rais atazuia mahakama kuwapa hukumu au atatengua hukumu. Na hii inaonesha kwamba nia ya katiba mpya ni F,wazo la kupunguza majukumu na kinga ya rais ndo baaasi
Wewe upo Somalia nini ? au upo Uvunguni Kwa Lugumi ? Umekariri propaganda za Membe na Timu yake akina January hadi Leo ? Kwa Taarifa yako Richmond ni ya Kikwete Dili zima Nenda Tanesco watakupa data zote jinsi ilivyokwenda hadi Rais Obama kuja kumwekea baraka pale Ubungo .Lowasa ana kashfa nzito sana ya ufisadi wa Richmond...mahakama ya mafisadi itaanza nae