Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Fisadi hawezi mkemea mwenzie, mwacheni Kingunge ahangaike kutetea wizi
 
Ndugu Kingunge na wapenzi wa ENL na mashabiki, wana CCM ambao hamkuridhika na mchakato ndani ya CCM acheni kutumia airtime bure tija . Nawashauri kwamba kama kweli mmechukia kaeni kimya ingieni msituni kwa kuwa mnasema au mlisema mna haya yafuatayo
-Mtaji wa wabunge 184
-Mtaji wa wapenda ENL wengi
-Mtaji wa wadhamini 800,000
-Wenyeviti wa CCM 25
-Wakuu wa wilaya
-Wakuu wa mikoa nk
Hakikisheni mnaibana CCM na inapoteza viti vingi vya Ungune, Udiwani na ikiwezekana urais . Tumieni same chanel that you have been using kuifuta CCM . Maana yake ni kwamba saidieni wapinzani kushika Nchi . Hapo tutajua kama kweli mnachukia na mmechukia kukiukwa taratibu na kuvunjwa katiba yenu lakini kama haya hamwezi kuyafanya basi kaeni kimya maana mmesha nyolewa . Nape ni msindhi na tena wa goli la mkono .
 
Huyo mzee agefanya utaratibu mapema ili apite bila kupingwa. Kama kweli imewauma kuenguliwa kwake, mrudishieni hela zake!.
 
Nimeshangaa kidogo. nimesoma kwenye gazeti moja habari za Kingunge Ngombale Mwiru anajaribu kufurukuta kujitetea mbele za watu. Hii inaweza kumletea mwisho mbaya. Nashangaa kwa nini asinyamaze. najua akinyamaza siku akiibukia pazeri hakuna atakayekumbuka upuuzi alioufanya.

Nikafikiri kuwa Siasa maana yake ni kuziba masikio na kufungua mdomo? tangu Kingunge alipojitokeza kwa mara ya kwanza kuwa mpambe wa Mtangaza nia, bila kujali yuko nyuma ya nani watu tulimkosoa sana. Maneno yote yaliyosemwa juu ya mwenendo wake huo bado hajasikia? Ameziba masikio? Anapanua mdomomkusema? Hana mshauri? Eti anatishia kuihama CCM?

Kuna watu wangapi wa kumfuata Kingunge? au anasubiri 'Mzee' akiamua naye afuate? Hivi anayoyasema kama Lowasa angepitishwa kwenye bora tano angeweza kuyasema? Hivi bado haoni sababu za mchakato kuwa kama ulivyokuwa ili kukinusuru chama?

Kama angekuwepo wakati wa Pilato angelifungulia jambazi la Baraba kwa kisingizio kuwa watu wengi wamemtaka? Ninamshangaa kwa kuwalaumu 'wazee'. Akina Mkapa, Karume, Mwinyi. Anasahau kuwa alistahili kuwa mmoja wao. Alistahili kuwa nao akikisaidia Chama alichokianzisha kiendelee kuheshimika kikiwa madarakani au nje ya madaraka (maana lazima siku moja kitatoka madarakani'.

Kingunge hana mshauri? Anamshauri nini? Ngoja niseme mambo mengine yasiyohusiana na mada hiyo hapo juu.

1) Uzee mara nyingi huonekana kwenye makunyanzi ya ngozi, na kutembea na mkongojo. Hauonekani kwenye fikra. Ndiyo maana watu wanaoshika mikongojo huendewa na kutakiwa kutoa mawazo yenye busara.

2) Siku moja Tembo alikuwa anavuka daraja. Kwa jinsi daraja lilivyokuwa na uzito wa tembo likawa (daraja) linatingishika. Baada ya tembo kuvuka akasikia nzi anasema 'kidogo tulivunje daraja'. Kumbe alikuwa mgongoni mwa Tembo wakati 'wakivuka' daraja.

Nakipongeza Chama Cha mapinduzi kwa kulivuka daraja la kwanza. Kumtafuta mgombea. Haikuwa kazi ndogo, pia namuasa mzee kingunge ulitakiwa kuwa kama kina mzee warioba, Dr. salim Ahmed Salim, Butiku, na wengineo amabo hakuwa na kambi.

Vile vile mzee kingunge yakupasa kujua kuwa unapoandaa watu wa kukushangilia ujue na wenzako wataanda watu wa kukuzomea tu na hivyo ndivyo ilivyotokea leo hii watu wote watakupuuza
 
Asema CCM haina uwezo wa kuteua wagombea wa urais zaidi ya mmoja. Yeyote mmoja angechaguliwa na wengine wote wakubali matokeo. Kama ni hivyo anavyofanya kingunge kumshabikia Lowassa basi hata yeye Bilohe anapaswa kulaumu kwani na yeye jina lake lilikatwa.
 
Kingunge anatetea maslahi yake binafsi sio ya taifa.
 
hivi huyu mkulima alishapata nauli ya kurudi kigoma ? maana inasemekana baada ya kukatwa jina alikwama kurudi kwao .
 
Kingunge anatetea maslahi yake binafsi sio ya taifa.

Lakini at least amejitokeza hadharani na kusema kile anachokiamini kwa sauti na bila woga hakutaka kuwa mnafiki, hakutaka kuwa ndumilakuwili machoni ankuchekea moyoni anakung'ong'a
Simfagilii lakini nimependa msimamo wake
 
Kingunge sio mzalendo hata kidogo!!
Huyo mzee kwake yeye maslahi binafsi ni muhimu kwake kuliko maslahi mapana ya Taifa letu.

Hivi nani asiyejua kuwa Kingunge keshautupa kisogo Ujamaa ambao alikuwa akiupaginia 'kinafiki' enzi za Mwalimu Nyerere na kujifanya anavaa 'vi-Cho-en-lai' vyake visivyokuwa na collar ili awaghilibu watanzania kuwa yeye ni die hard supporter wa siasa za kijamaa?

Lakini tumuulize swali moja huyo mzee anayejifanya mjamaa halisi.

Iliwezekanaje ajimilikishe tenda ya kifisadi pale Ubungo Terminal Bus ambako kila siku inakisiwa anawakamua watanzania masikini wanaoingia kituoni hapo, ambapo inakadiriwa kila siku anaingiza zaidi ya shilingi milioni 4 wakati yeye anatoa tozo kwenye kituo hicho shilingi milioni 1 pekee, ambapo anatengeneza super profit kwa kila siku kujiingizia zaidi ya shilingi milioni 3 za kifisadi?!

Huyo mzee kama kweli angekuwa ni mpiganaji halisi wa utekelezaji wa kanuni, ni kwa nini basi wakati wa Bunge la Katiba, wakati Spika wa Bunge hilo Samuel Sitta alipokuwa akizifinyanga finyanga kanuni za Bunge hilo ili kulazimisha akidi ya 2/3 ya wabunge ili kuipitisha katiba yao ya Lumumba, hadi kuruhusu watu waliokuwa wameenda kuhiji Macca na wale waliokuwa wamelazwa hospitali ya Apollo kule India kuruhusiwa kupiga kura kwa 'SMS' ambapo ilikuwa ni ukiukwaji mkubwa mno wa kanuni za Bunge hilo ambazo zinahitaji wapigaji kura ni lazima wawemo kwenye Jengo la Bunge?

Badala yake yeye na huyo anayempigania kufa na kupona mzee wa mamvi waliamua kuwa 'mabubu' wakati kanuni za Bunge zikikiukwa waziwazi.
 
Back
Top Bottom