Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Magamba mwaka huu mtagawana fito Kingunge ameanza ngoja Lowasa mwenyewe afunguke ccm ipasuka vipande-vipande Pasco umemsikia Kingunge?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu NTOBI ni afadhari wanaojua huu UFA na makada tu pamoja na baadhi ya wasomi. lkn kama wapiga kura wa vijijini wanhekuwa wanajua haya, basi ilikuwa CCM kwisha. Bado wana bahati hii.
 
Ndio madhara ya kuchakachua maoni ya wananchi.. Nafikiri amepata fundisho.
 
Mtu ukipewa pesa lazima uitolee maelezo ya matumizi. Ndilo analofanya Ngombale. Ana justify pesa ya Lowassa.
 

Ndo uhuni wenyewe huo sasa unaopelekea watu kuenguliwa kiajabu ajabu tu.

Mtu kama Amina Salum Ali anapita anaenda hadi tatu bora halafu watu makini kama Mark Mwandosya na Agustino Mahiga wanaenguliwa bila hata kujua ni kwa sababu zipi.

Kwa nini hayo majina yote 38 yasipigiwe kura na kuchukua watano waliopata kura nyingi na kuendelea na utaratibu huo hadi kumpata mtu mmoja?

CCM ni wahuni hadi wanafanyiana uhuni wao kwa wao na wakiunda serikali wanauendeleza uhuni wao kwa wananchi.
 
Maneno ya wakosaji! Mbona wao wamefanya sana fitna kwa wengine? Tunasubiri Oktoba 25 tupige kura.
 
Kingunge anasahau kamati iliyomchinja lowassa ndio iliyomchinja malecela akiwa makamu mwenyekiti wa chama taifa na yeye kingunge hakupaza sauti kumlilia!

Kinachoonekana sasa ni mbinu mbadala ya kundi LA mafisadi wanaomzunguka lowasa kutaka wasisahaulike kwenye utawala mpya

Pia kasahau kutuambia yeye na mwalimu walitumia busara gani kumfunika lowassa!
 
kwa kifupi sana


wakati wa kikao cha maadili kujadili report za watia nia kusomwa membe na lowasa wote walikatwa majina ...report zao zilikuwa mbaya sana..tena mbaya mno...ila ya lowasa ilikuwa mbaya zaidi kuliko.....mtu aliyeongoza kwa kuw ana alama za juu kwenye maadili ni Makongoro,magufuli, makamba, migiro na huyo amina... kamati ikaazimia kuchuku majina hayo kwa sababu walizozijua wao...baada ya mda mweneyekiti akaonekana kutoridhika na hiyo tano bora..akamwita mstaafu wa awamu ya tatu na ya pili na pia kina malecela...akalamimika kuwa tano bora yote imejaa watu ambao wao wazee wastaafu waliwataka..yeye kama mwenyekiti hana mtu...iweje tano bora awe na mtu mmoja tena mwanamke..mvutano kidogo ukatokea...mwenyekiti akapewa uhuru wa kuamua anachotaka...ndipo akasema namuondoa mmoja na kuweka mwingine...akaliondoa jina la Makongoro na kuweka la membe..wazee wastaafu wakashangaa sana ...ili amani ya yerusalemu iendelee kudumu wakakubaliana na mawazo ya mwenyekiti japo kwa shingo upande...
wakarudi chumba cha mkutano wakawaeleza wajumbe wa maadili juu ya mabadiliko hayo ...minong'ono ikatokea mle ndani..gafla mwenyekiti akafunga kikao.... na kutoka na hiyo tano bora iliyochachuliwa kwa kuondolewa makongoro na kumwingiza membe...hii ni kwa kifupi sana hivyo ndivyo ilivyokuwa...badae huko mbele nikipata mda ntaeleza kwa nini lowasa alikatwa tena kwa kutumia ''collecting ink''...
 
Maneno ya wakosaji! Mbona wao wamefanya sana fitna kwa wengine? Tunasubiri Oktoba 25 tupige kura.

Hata huko kupiga kura ni kutimiza wajibu wa kujisumbua tu maana tayari Magufuli ndo rais anayesubiri kuapishwa.

Usitegemee kabisa Jaji Lubuva amtangaze mgombea tofauti na Magufuli kuwa ndo mshindi wa urais.

Hiyo tume ya uchaguzi ni tawi la CCM.

Si wenyewe mmeona mwaka huu yule Jaji mkuu wa zamani Agustino Ramadhani alitangaza nia kupitia CCM?

Yule mwaka 2010 si ndo alikuwa makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi chini ya mwenyekiti Lewis Makame..?

Hiyo tume ya uchaguzi ni makada wa CCM tu na jukumu lao kubwa ni kulinda maslahi ya chama kwanza.
 
Mzee amelalamikia taratibu kutofuatwa ........ hajalalamikia Lowasa pekee kukatwa .....
Mkuu mbona waliochukua form walikuwa wengi wakiwemo Mh.Membe,Mwigulu,Nyerere nk. Mbona muda wote alikuwa anahudhulia mikutano ya Lowasa na kumpigia debe na kujaribu kumtetea kwa hoja za kulazimisha tu!! Tusijidanganye hapa atetei cha kanuni wala nini sijui, kakasirika baada ya mteule wake kukatwa hana jingine analotetea hapa ni unafiki tu, Baba wa taifa angefufuka leo hii angemshangaa mjamaa mwenzake damu damu, sio Kingunge tunayemjua sisi kabadirika kabisa!
 
Mfumo wa ccm ni mbovu na Dr wao kila akifanya dili akishtukiwa huwa anakimbia nje na kwanza anatunga tukio kama la juzi ili kupoteza watanzania kisha anakimbia haibu.sasa yuko swiss.

swissme

lipi hilo,lile la majambazi wa ukonga stakishari?.dah!!....
 

Hata kama hatetei kanuni lakini bado anachokisema ni cha msingi.

Mchakato wa CCM hata mimi nisiyewapenda niliuona ni wa kijanja kijanja.
 
kumbe Kinjekitile ni mtoto wa kingunge?halafu kumbe anauza madawa ya kulevya ndo akili zake hazipo kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Kosa kubwa alilofanya Kingunge ni Kuonyesha kwa wazi ni mtu gani alitaka awe kiongozi!Hakutendea haki wanachama wengine waliojitokeza....Kama Mwinyi,Mkapa na Kikwete wangejitokeza hadharani na kutangaza wagombea ambao wanawapenda Chama kingegawanyika kabisa...kutokana na hilo Kingunge anakosa sifa ya kuzungumzia mchakato wa uchaguzi kwa kuwa watu wanafikiri anatoa haya maelezo kwa sababu mgombea wake alienguliwa...amepoteza sifa ya kuwa mshauri katika kwa chama kwa sababu yuko biased...Hii ndo siasa pale karata zinapochangwa vibaya!
 
Kingunge ni mtu wa jk,anacho kifanya hapo ni kumhadaa lowasa na kumpoza ili atulie hio ni fitna yetu ccm na kingunge ndo mpikaji mkubwa, ccm ni zaidi ya chama.
 
Hiki kizee ni kinafiki sana. Mbona hakikulalamika rafu iliyofanywa kwenye bunge la katiba ambamo yeye alikuwa mganga wa kienyeji?
 
Lowasa angeingia top 5 ndiye angepita...!!! na asingeweza chochote kuongoza hii nchi zaidi ya malumbano, kumkata juu kwa juu ilikuwa ni sahihi, na kumpiga teke membe ilikuwa sahihi ili kuequalize wote waliokuwa na magroup (na hizo ni hekima za mkapa) ...wagombea wenye uwezo wa kuongoza hii nchi walikuwa wawili tu ndani ya CCM ambao hawaangalii uso wa mtu kwenye utendaji kazi...MAGHUFULI na MWAKYEMBE.
 
haya sio mambo ya kudharau, kwa kuwa hakuna mwingine wa kutoa haya.! Kwa kweli anajiamini..! Ndio tunataka watu wenye msimamo kama wa huyu mzee..!
#Bg Up

Ni kweli mawazo ya kingunge ni sahihi kichama kwa sasa kuliko binadamu yeyote aliyewahi kuumbwa chini ya jua. Yeye ni miongoni mwa watu watatu walio-design na kuandika katiba ya CCM, anaielewa katiba sawa na mimi ninavyoielewa Biblia.
 

Bado sijaelewa kuhusu yule Jaji Augustino Ramadhani ambaye tuliaminishwa kwamba hana kashfa je ni ithibati gani zilizotumika kumdhalilisha kiasi hiki? Na wale waliomshawishi kuchukuwa fomu wanajionaje?

Jaji hadhi yake imeshuka sana na hiki ni kiburi na uroho wa madaraka alionao kutoitambuwa hadhi ya Jaji. Hili ndio jinga kuliko wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…