Kinondoni, Dar: Hamza Mohammed, Polisi Watatu na mlinzi mmoja wauawa katika Majibizano ya Risasi

Kinondoni, Dar: Hamza Mohammed, Polisi Watatu na mlinzi mmoja wauawa katika Majibizano ya Risasi

Guys I am informed there’s a guy shooting randomly near Stanbic Bank, anyone with more news?

Inadaiwa kuna watu wameuawa. Ni Karibu na Makao Makuu ya Stanbic.

========

Mtu mmoja ambaye alionekana kufyatua risasi karibu na Ubalozi wa Ufaransa Jijini Dar es Salaam amedhibitiwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, (IGP) Simon Sirro amethibitisha kuuawa kwa askari wawili kwenye mapambano ya kurushiana risasi yaliyotokea eneo la Daraja la Salenda jirani na Ubalozi wa Ufaransa, Dar es Salaam.

Tukio hilo limetokea leo Jumatano Agosti 25, 2021 baada ya mtu mmoja ambaye hajafahamika kuzua taharuki baada ya kufyatua hewani risasi huku akisikika akisema kuwa anawatafuta polisi.

Akizungumza katika kikao kazi cha maofisa wa polisi, Sirro amesema mtu huyo naye ameuawa kwa kupigwa risasi.

“Mmeziona clip zinaruka sasa hivi akaingia barabara kubwa akawa anatamba na SMG na yeye amepigwa risasi na askari wetu hivyo, askari wetu wamefariki na yeye amefariki” amesema IGP Sirro.

Ameeleza kuwa wanaendelea kufuatilia kufahamu mtu huyo ametokea wapi na baadaye watatoa taarifa kamili.

IGP Sirro amenukuliwa kupitia kipande cha video kilichorushwa kwenye mtandao wa kijamii wa Wasafi Fm.

PIA SOMA:
1. Mashuhuda wasimulia tukio la aliyekuwa akipiga risasi

UPDATE: Waliouawa ni Polisi Watatu na Mlinzi mmoja, wengine sita wajeruhiwa.
Jeshi la Polisi limesema idadi ya Watu waliouwawa na Mtu mwenye Bunduki aliekua akifyetua risasi ovyo karibu na Ubalozi wa Ufaransa Dar es salaam ni Watu wanne huku kati yao Watatu wakiwa ni Polisi na mmoja ni Mlinzi wa Kampuni binafsi ya ulinzi.

"Leo August 25 2021 tumekutwa na tukio baya kabisa, tukio la kihalifu ambalo limepoteza maisha ya Watu wanne na watatu kati yao ni Askari Polisi, limetokea katika makutano ya barabara ya Kenyatta na Kinondoni Askari wetu walikua kazini akatokea Mtu akawashambulia kwa Bastola na alipowashambulia na kuanguka alichukua Bunduki za Askari hao na kuanza kurusha risasi ovyo kuelekea Ubalozi wa Ufaransa"

"Ukiachia Watu wanne waliouwawa leo tuna Watu 6 ambao wamejeruhiwa kwenye tukio hili na wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, taarifa zaidi tutaendelea kupeana kadri muda unavyokwenda, ni mapema sana kubaini kwanini alifanya vile lakini tumeshaanzisha Timu ya upelelezi na muda sio mrefu tutakamilisha"

"Kuhusu baadhi ya video kusema kwamba huyu Mtu ni Mkazi wa Upanga sisi hatuthibitishi mambo kupitia clips za video, tunathibitisha mambo kupitia upelelezi kwahiyo upelelezi ndio utakaoeleza, kuhusu swali la Waandishi kuhusu kuwepo kwa dalili zozote za ugaidi kwenye tukio la leo hatuwezi kusema chochote hii ni mapema lakini uchunguzi ndio utakaosema kama kuna ugaidi au hakuna ugaidi"

"Kwa sasa hatuwezi kusema amekutwa na kitu gani mfukoni, Polisi bado wapo eneo la tukio... ni mapema sana kusema amekutwa na nini kwasababu Wataalamu wapo kazini, kuhusu kama ni Raia kama sio Raia uchunguzi ndio utasema baada ya upelelezi kukamilika tunachojua sasa huyu ni Muhalifu"

UPDATES: Polis wafika Upanga katika nyumba aliyokuwa akiishi Hamza
kutoka Upanga Dar es Salaam kwenye nyumba aliyokua akiishi Hamza, Mwanaume aliyefyatua risasi na kuwauwa Watu wanne leo Jijini Dar es salaam ( Askari Polisi watatu na Mlinzi wa Kampuni binafsi mmoja).

Polisi wameifunga nyumba hiyo na kuondoka na Ndugu wa Hamza kwenda nao Polisi usiku huu ambapo walifika hapa toka saa kumi na moja jioni, endelea kukaa karibu na AyoTV na Youtube ya millardayo kufahamu zaidi.

olisi wameifunga nyumba aliyokua akiishi Mwanaume aliyefyatua risasi leo na kuuwa wanne Dar es salam, baada ya kuifunga nyumba hii iliyopo Upanga Dar es salaam wameondoka pia na Ndugu wa Mtu huyo aitwae Hamza kwenda nao Polisi usiku huu pamoja na Pikipiki aliyokua akiitumia.

Hamza amekua gumzo leo hii Dar es salaam baada ya kuwaua kwa risasi Watu wanne leo na kujeruhi wengine sita, endelea kukaa karibu na Youtube ya millardayo kufahamu zaidi.


View attachment 1907510
View attachment 1907511


View attachment 1907519


Hii ni developing news…

Kuna mtu mmoja, kapigwa risasi na kuanguka katikati ya barabara
View attachment 1907602
View attachment 1907621
View attachment 1907645View attachment 1907646
Huyu anadaiwa kauawa.
Pamoja na yote yaliyotokea hakustahili kufa
 
Wadau wanasema ni mwana CCM.
Lakini nafikiria kwani CCM na tukio kunauhusiano?
Tuepuke kujaji mambo mapema mkuu. Mbona wengine walianza kuhusisha na CDM kwa kadi fake? Nadhani unanipata mkuu.
 
Tuepuke kujaji mambo mapema mkuu. Mbona wengine walianza kuhusisha na CDM kwa kadi fake? Nadhani unanipata mkuu.
Hata mimi nilianzisha uzi kupinga hayo.
Watu tulianza kuhukumu mapema sana.
 
Tuepuke kujaji mambo mapema mkuu. Mbona wengine walianza kuhusisha na CDM kwa kadi fake? Nadhani unanipata mkuu.
Hata mimi nilianzisha uzi kupinga hayo.
Watu tulianza kuhukumu mapema sana.
 
Hata mimi nilianzisha uzi kupinga hayo.
Watu tulianza kuhukumu mapema sana.
Sawa mkuu. Hata sasa baada ya kijulikana kwamba ni mwanachama wa CCM, nadhani haifai kuhusisha chama chake, jambo libaki kwa mhusika mwenyewe. Watu waache ushabiki wa mambo ya kisiasa. Nadhani hili litawafunza watu baada ya mhusika kujulikana ni mwanaCCM tofauti na walivyoanza hadi kufake kadi ya CHADEMA. Ni hayo tu mkuu.
 
Sawa mkuu. Hata sasa baada ya kijulikana kwamba ni mwanachama wa CCM, nadhani haifai kuhusisha chama chake, jambo libaki kwa mhusika mwenyewe. Watu waache ushabiki wa mambo ya kisiasa. Nadhani hili litawafunza watu baada ya mhusika kujulikana ni mwanaCCM tofauti na walivyoanza hadi kufake kadi ya CHADEMA. Ni hayo tu mkuu.
Kweli kabisa mkuu hata mimi nilieleza hivyo.
Pia unaweza soma hapa Wabongo tuache unafiki
 
Popote duniani Ardhi ulipo ubalozi ni nchi nyingine

Ulipo ubalozi wa ufaransa ni nchi ya ufaransa

Askari waliokuwepo waliouawa walikuwa kwenye ardhi ya nchi ya ufaransa eneo la ubalozi wa ufaransa Tanzania

Hamza ni gaidi sababu alirusha risasi na kuua watu waliokuwa kwenye ardhi ya nchi ya ufaransa polisi watatu na mlinzi mwingine wakiwa nchini ufaransa na risasi zikatua nchi ya ufaransa

Ni gaidi sababu kavamia nchi ingine na kuvurumisha marisasi hivyo ni gaidi
 
Hamza hakuwa ubalozini, na hakuuwawa ubalozini. Hamza alikuwa eneo la wazi lililokuwa karibu na ubalozi wa ufaransa, ni barabarani, mtu yoyote anafika na kupita. Hamza alikuwa na visa binafsi dhidi ya Polisi wa Tanzania, alisikika hivyo na aliwalenga polisi.

Tusilazimishe mambo ya kipuuzi hapa JF.
 
Popote duniani Ardhi ulipo ubalozi ni nchi nyingine

Ulipo ubalozi wa ufaransa ni nchi ya ufaransa

Askari waliokuwepo waliouawa walikuwa kwenye ardhi ya nchi ya ufaransa eneo la ubalozi wa ufaransa Tanzania

Hamza ni gaidi sababu alirusha risasi na kuua watu waliokuwa kwenye ardhi ya nchi ya ufaransa polisi watatu na mlinzi mwingine wakiwa nchini ufaransa na risasi zikatua nchi ya ufaransa

Ni gaidi sababu kavamia nchi ingine na kuvurumisha marisasi hivyo ni gaidi
Eneo la ubalozi linaishia kwenye uzio wao.
 
Back
Top Bottom