Kinondoni Makaburini: Mazishi ya Mwana JF, Mzalendo Sanctus Mtsimbe

Hahahaha hongera kutuwakilisha mkuu.
 
Jamani tangu nije Dar 1981 wakati wa Nyerere Kinondoni ilikua almost pamejaa. Cha ajabu hata kesho bado Kuna nafasi ya kuhifadhi mwili.
Nini Siri ya makaburi ya Kinondoni kutojaa?
Binafsi sitopenda kuzikiwa Kinondoni.
 
Anasema terminal illness. Kwa tafasiri isiyokuwa rasm ni magonjwa yasiyoyakuambukiza na yaliyo magumu kutibika na kusababisha vifo. Mfano cancer, ugonjwa wa figo,ini, moyo na mengine magumu kama hayo.
Mkuu DAMA2025 , you are absolutely right, ugonjwa wake ni moja ya magonjwa hayo uliyoyataja. Terminal illness ni ugonjwa ambao lazima utakufa, hivyo ukisema unaumwa nini, watu wanakuonea huruma hivyo wanakuangalia kwa jicho la huruma.

Hili la kukabiliwa na changamoto ya kiafya bila kusema, pia tunafanana, mimi pia ninaishi na changamoto fulani ya kiafya ila yangu sio terminal, sijawahi kuitaja ili nisionewe huruma!.
Tunafanana sana na Sanctus Mtsimbe.

P
 
Ivi kumbe ukienda marekani ni kama umekufa (sikujua kama ni kifoni) watu wanavuta vyombo vingine bongo mpaka kifo kitutenganishe kumbe kifo chenyewe ni marekani
 
Ila ngosha mnakosea sana kuoa vibinti vidogo! Naona mwenzio mpaka alikuwa na kitoto cha uzeeni! Utafikri kijukuu chake!
Mkuu Manjagata , kiukweli japo jamaa ni rafiki yangu, na tulifanana kwenye kupenda dogodogo, mimi nilipenda kwa ajili ya matumizi tuu, mwenzangu was searching for a companionship maana by the time tunajuana, wife wake wa sasa Mama JJ was not on the picture na JJ alikuwa hajazaliwa!.

Baada ya msiba ndipo nikagundua huyu jamaa, tumefanana sana, hadi kwenye hili Changamoto za kupata mtoto mchanga ukiwa umri wa kustaafu, unakuwa ni Baba Babu. Dawa ni kujipanga kabla, vinginevyo ni kubebesha watu mizigo yako tumefanana!.
P
 
Kwa vile mumefanana kwa mambo mengi.Usisahau kupima hayo maradhi yake ya terminal .
Muhimu zaidi hata ukiwa hutaonekana na ugonjwa huo nakunasihi umrithi ushujaa wake kwa maradhi yoyote yatakayokupata kwani ushujaa katika maradhi ni zawadi bora kwa wanadamu,
Sisi waislamu tunatakiwe tufe na shahada na pindi ukianza kuchanganyikiwa na maradhi yako basi shahada inakuwa mbali na wewe.
 
Tunashukuru kwa upendo mkuu uliouonyesha kwa ndugu yetu marehemu matsimbe. Nimesikitika Sana, kusikia taarifa hiyo ya msiba wake.
Tunashukuru sana kwa upendo wenu wa dhati mliouonyesha kwa ndugu yetu Matsimbe,Mungu awabariki sana. . Tumesikitika sana kwa msiba huo, mm pia ni msabato mwenzake na tumepoteza mtu wa muhimu sana.
 
Ivi kumbe ukienda marekani ni kama umekufa (sikujua kama ni kifoni) watu wanavuta vyombo vingine bongo mpaka kifo kitutenganishe kumbe kifo chenyewe ni marekani
Lengo la ndoa ni ile huduma, mkiwa mbalimbali na hakuna huduma, ni sawa, hakuna ndoa. Muda wa kikatiba wa existence ya ndoa isiyo na huduma ni miaka miwili, muda huo ukiisha ni hakuna ndoa ila vyeti vipo ni mpaka kifo kiwatenganishe.
P
 
Hapo ngosha ni kujishusha hadhi tu hata kama ulikuwa na heshima zako unakuwa umepunguza marks! Miaka 60 unakuwa na mtoto mchanga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…