Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukweli hapa hatuna mtu serious ni maigizo tupu, kazi anayoweza ni ya kuteua, kutengua na kuhamisha watu pekeeSamia amepwaya, hili halina mjadala, na kabla hata hayo mambo mawili hayajatokea, la bandari na Makonda kuwa Mwenezi wa CCM, tayari palishakuwepo na minon'gono kuwa Samia hatagombea 2025.
Kwa sasa kusema nani atagombea au vipi, hili sioni kama lina uzito sana, ila Mwinyi kupewa hiyo nafasi labda ndio watampa ili kurekebisha namba, kwani atakuwa tayari ameshatumikia kipindi kimoja Znz, ili cha pili aje kumalizia Bara.
Mpole kushinda Samia ..yaani yule akiwa Raisi wapigaji watafurahi sanaSiyo Dr Mpango tena? 😂
Kuna Mtu humu JF aliwahi kusema Mama hana mpango wa kugombea 2025. Sababu kubwa ni kwamba kuna kundi kubwa lenye ushawishi ndani ya CCM, ambalo halijamkubali Mama from day one. Wanasubiri 2025 wajitokeze na kumueleza wazi kuwa ameshamaliza nafasi yake ya pili hivyo akae pembeni. Na aking'ang'ania basi hao Jamaa watatumia plan B".Huu Uzi umeletwa na watu wa propaganda kupima upepo. Inakuwaje Mwinyi ampinge Dada yake? Mwinyi ni Rais mzuri Sana ila siungi mkono njia anayotaka kuitumia. Amalizie Kwanza Zanzibar aje na kwa Muungano Kama afya inaruhusu.
Lingine bandiko hili halimhusu Mwinyi bali Kuna mwanasiasa antaka kumfanyia Shambulizi la kushutukiza Rais Samia. Yaonekana hali sio shwari chamani na serikalini.
Kwa akili yako unafikiri Mwinyi ndio anaamua kumpinga Samia?Huu Uzi umeletwa na watu wa propaganda kupima upepo. Inakuwaje Mwinyi ampinge Dada yake? Mwinyi ni Rais mzuri Sana ila siungi mkono njia anayotaka kuitumia. Amalizie Kwanza Zanzibar aje na kwa Muungano Kama afya inaruhusu.
Lingine bandiko hili halimhusu Mwinyi bali Kuna mwanasiasa antaka kumfanyia Shambulizi la kushutukiza Rais Samia. Yaonekana hali sio shwari chamani na serikalini.
Mpango Umri ni tatizo, huyo atapumzishwa 2025 rasmi.Siyo Dr Mpango tena? 😂
Mfuatilie vizuri ana elements za kidikteta, hana tofouti kubwa na marehemu JPMMpole kushinda Samia ..yaani yule akiwa Raisi wapigaji watafurahi sana
Nikweli waisiharamu ndiyo wanao tuchafulia nchiAje mgalatia sasa
Hao ni nduguMsichokijua ni kuwa kile kiti kina addiction sio rahisi kama mnavyodhani mama samia kampita mbali sana mwinyi kwenye uongozi kwa sasa.
Hawezi kubali hilo kila mtu anapenda kuacha legacy ya kipekee na ndio samia anachotaka kufanya kwa upande wake.
Ushauri kwa team Mwinyi kuna mambo sio ya ya kulazimisha na sio kila mtu ameandikiwa au ana haki ya kuwa rais wa jamhuri jifunzeni kwa kwa mhe. Lowasa na mkubali yapite..
"Halafu we Pascal si ulituambia Mpango ndio Mpango mzima!au amekua sio Mpango!!?"Kwa hiyo ndio huyo humble, patriotic, Truthfully, visionary and intelligent atakaefanikisha next stage sio!!?
Bado mapema mnyukano utamuibua mwingine kabisa wakuu!!
Kwasasa ngoja tuone hizi karata za Mama kumteua kina mwegelo uwt na makonda zitamfikisha wapi!!
Bahati mbaya sana ndani ya CCM kadri jinsi unavoupigania urais ndio unavozidi kuukosa kabisa!!
Tunasubiri haya,
Halafu we Pascal si ulituambia Mpango ndio Mpango mzima!au amekua sio Mpango!!?
Hizo story zote zinategemea wizi wa kura zaidi ili kufikia hilo hitimisho!Mgala ataingia 2030!.
P
Watoto wote ni wa baba mmoja, hamna kinacho badilikaAngalizo kwa Wanabodi na Mode
Hii no C&P kutoka kwa mwana JF fulani.
Kwasababu mwandishi ni member wetu humu na humu hajaileta, naomba ikitokea ameileta humu, then futa hili bandiko langu.
Nime C&P kwasababu mimi ni miongoni mwa watu wa mwanzo mwanzo kuandika humu kuwa mgombea urais wa CCM kwa uchaguzi wa 2025 could be Dr. Hussein Mwinyi, kupitia bandiko hili Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke
Hivyo hoja kama hii inapotolewa na mwajeiefu mwenzetu, mwandamizi kama huyu, hivyo nimejikuta ni muhimu kuisambaza.
Paskali.
Barua ya...
Kwa kiasi kikubwa, siasa za Tanzania zimejikita zaidi kwenye chaguzi, hususan uchaguzi mkuu. Kwamba vyama vya siasa hutumia muda mwingi kujiandaa na chaguzi kiasi kwamba kuna dhana kwamba haviwatumikii wananchi vya kutosha kutokana na hilo.
Lakini lengo kuu la chama chochote cha siasa ni kushika dola. Na katika nchi za kidemokrasia, kushika dola kunawezekana kwa njia moja tu, yaani uchaguzi mkuu. Kwa mantiki hiyo, ni sahihi kwa vyama vya siasa kujipanga vema kwa ajili ya chaguzi.
Na kwa chama tawala, kisipofanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya chaguzi zijazo, nafasi yake kama chama kinachoshika dola inakuwa hatarini.
Ni katika mazingira hayo ndio maana kumekuwa na maongezi mengi kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 japo bado miaka miwili hivi kabla ya uchaguzi huo. Na japo kuna chaguzi za serikali za mitaa mwakani, maongezi mengi ni kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Taarifa za kiintelijensia zinaeleza kwamba kuna jitihada zinafanyika huko Zanzibar kumwezesha Dkt Hussein Mwinyi kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano mwaka 2025.
Si tayari CCM “ina mgombea wake” 2025?
Naam. kwa mujibu wa utaratibu usio rasmi huko CCM, rais aliyepo madarakani anakuwa automatically mgombea pekee wa urais mwaka katika uchaguzi utakaomuingiza awamu ya pili ya urais wake.
Ilikuwa hivyo kwa Mkapa mwaka 2000, Jk 2010 na Magufuli 2020. Na inatarajiwa iwe hivyo kwa Mama Samia 2025.
Hadi wakati makala hii inaandikwa haijafahamika rasmi kwanini kuna mpango huo amba sio tu utapelekea “kuukoroga utaratibu huo usio rasmi wa Rais aliyepo madarakani kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo ili akamilishe ngwe zote mbili” bali pia utakuwa upinzani baina ya wanasiasa wawili kutoka Zanzibar.
Maandalizi yameanza
Taarifa zinaeleza kwamba tangu Zanzibar ijiunge na Tanganyika mwaka 1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hakuna kipindi ambapo upande huo wa Muungano umepokea fedha nyingi kutoka serikali ya Muungano kama kipindi hiki cha utawala wa Mama Samia.
Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa sehemu ya fedha hizo zimekuwa zikitumiwa na wanamkakati wa mpango huo wa kumwezesha Dkt Mwinyi kuwa mgombea mwaka 2025.
Licha ya ukweli kuwa maandalizi ya uchaguzi wowote hule huhitaji fedha za kutosha, yaaminika kuwa uchaguzi wa mwaka 2025 utatawaliwa na matumizi makubwa ya fedha hasa kutokana na ukweli kwamba wanasiasa wengi wamepoteza mvuto machoni mwa wananchi na njia pekee ya “kupendeka” ni kumwaga fedha.
Mama Samia anawarahisishia kazi wapinzani wake ikiwa ni pamoja na mwanasiasa huyo wa Zanzibar
Kuna matukio mawili makubwa ambayo yanatarajiwa “kumsumbua” Mama Samia kati ya sasa na uchaguzi mwaka 2025. La kwanza ni suala la mkataba wa bandari ambalo japo “kwa nje ya CCM” linaonekana kama lilikuwa lina mwafaka miongoni mwa wana-CCM, ukweli ni kwamba sio tu lilizua mgawanyiko wakati wa mjadala bali pia limeacha makovu ambayo yanaweza “kukwanguliwa” pindi kampeni za urais zitaposhika kasi.
La pili ni hili la “Mama Samia kujichoma msumari mwenyewe” kwa kumteua Bashite kuwa katika mwenezi wa chama hicho, huku akifahamu fika kuwa kada huyo anachukiwa na wengi ndani na nje ya chama hicho.
Japo Mama Samia anatarajia kuwa Bashite atamsaidia kukabiliana na “wapinzani wake”, nguvu za kada huyo huko nyuma zilitegemea zaidi staili ya uongozi wa kibabe wa marehemu Magufuli, ambayo ni tofauti na satili ya uongozi wa Mama Samia, unless aamue kubadilika.
Hitimisho
Kuna msemo kuwa kwenye siasa, wiki moja ni sawa na uhai mzima (lifetime). Na kwa hakika, kati ya sasa Novemba 2023 hadi Oktoba 2025 ni takriban miaka miwili, na mengi yanaweza kutokea aidha kuimarisha dhamira ya mwanasiasa yeyote mwenye ndoto za kumpiku Mama Samia au urais wa Mama Samia ukaimarika zaidi kiasi kwamba yeyote mwenye ndoto za kum-challenge atakuwa anapoteza muda wake.
Mwana if fulani.
C&P by Paskali
Alitaka vizuri, alisema Sina mtu yeyote niliyepanga awe Makamu wangu. Ninyi changu CCM mnitafutie.Kwa akili yako unafikiri Mwinyi ndio anaamua kumpinga Samia?
Magufuli mwenyewe hakutaka Samia awe makamu wake ila wenye maamuzi wakalazimisha
JidanganyeAlitaka vizuri, alisema Sina mtu yeyote niliyepanga awe Makamu wangu. Ninyi changu CCM mnitafutie.
Huyo ni tapeli mkubwaMaombi yangu kila siku,siku moja hii nchi iingie katika mikono salama ya Kassim Majaliwa.