Ach uongo, serikali haikutaifisha hicho kiwanda. Nakumbuka wakati ule iliamuliwa kiwanda kifungwe na kigeuzwe kuwa storage facility ya mafuta yaliyosafishwa. Hoja za kifisadi zilitolewa wakati ule kuwa Msumbiji na Afrika Kusini kuna refinery kubwa ambazo zitahudumia mpaka huku kwetu, kulikuwa na malumbano makali wazalendo wakipinga na wahujumu ndani ya serikali na washirika wao nje ya serikali wakishabikia Tipper ifungwe isisafishe mafuta. Hadi wakati kinafungwa kiwanda hicho kilikuwa mali ya ubia kati ya Italia na Tanzania.
Uamuzi wa kukifunga haukuwa wa busara bali uligubikwa na ufisadi na sindicate iliyolenga kuifanya Tanzaniaiwe tegemezi wa mafuta yaliyosafishwa nje ya nchi.