SI KWELI Kiongozi Mkuu wa North Korea asilimu kuwa Muislam

SI KWELI Kiongozi Mkuu wa North Korea asilimu kuwa Muislam

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Tizama hi video kwa makini kabla ya ku-comment.

Kiongozi wa Korea kasikazini amelegeza mashariti kwa dini moja tu uko nchini kwake baada ya kushuhudia great miracle en Wisdom katika kitabu cha Qur"an tukufu, wakati anaingia madarakani 2011 Uislamu kama dini zingine zilikua marufuku nchini mwake, mwaka 2015 waislamu kwa kujificha ficha walifika 3000 tu kwasasa waislamu ni 30,000.

Adhana ya kila swala kwa kutumia vipaza sauti misikitini imeruhusiwa katika hiyo nchi kali ya kicommunist kuna hofu kubwa kwamba Uislamu ndani ya miaka 10 watagawana hiyo nchi na wa Buddha.


kimu.png
 
Tunachokijua
Kim Jong Un ni kiongozi wa Korea Kaskazini tangu 2011, alipochukua nafasi ya baba yake, Kim Jong Il. Utawala wake unazingatia itikadi ya Juche, falsafa inayosisitiza kujitegemea, ingawa kwa hali halisi inatumiwa kudumisha mfumo wa udikteta wa chama kimoja. Serikali yake inadhibiti karibu kila sekta ya maisha ya wananchi, ikiwemo dini, na kuifanya Korea Kaskazini kuwa moja ya mataifa yanayokiuka sana uhuru wa kuabudu.

Tangu Desemba 2, 2024 kumeibuka Taarifa inayodai kiongozi huyo Kim Jong Un ameamua kubadii dini na kuwa Muislam. Taarifa hii iliyoletwa na MwanaJamiiCheck inamuonesha Kim akiwa ameshika Msahafu huku kukiwa na ujumbe unaoarifu kiongozi huyo kusilimu. Uchunguzi wa JamiiCheck umebaini taarifa hiyo kutokea Mtandao wa YouTube (hapa na hapa), Mtandao wa TikTok (Tazama hapa), kwenye tovuti za watu binafsi (Tazama hapa). Aidha, JamiiCheck imebaini kuwa madai kama haya yameshawahi kujitokeza mwaka mmoja uliopita (Mwaka 2023) (Tazama hapa na hapa).

1733642513679-png.3171923

Baadhi ya Post za TikTok zinazoelezea Kim Jong Un kusilimu

Upi uhalisia wa Madai hayo?
Ufuatiliaji wa kimtandao uliofanywa na JamiiCheck umebaini kuwa madai ya Kim Jong Un kubadili dini na kuwa Muislamu yameenea hasa kupitia YouTube, katika akaunti za watu binafsi. (Tazama hapa na hapa)

Hata hivyo, hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa sauti au video unaothibitisha madai haya. Zaidi ya hayo, ufuatiliaji wetu katika vyanzo vya kimataifa umeonyesha kuwa hakuna ripoti rasmi au chanzo kinachoaminika kilichoripoti madai hayo.

Kwa kuzingatia historia ya Korea Kaskazini na msimamo wa serikali yake dhidi ya dini, madai haya yanaonekana kuwa ya kubuniwa. Viongozi wa taifa hilo mara nyingi hujihusisha na itikadi ya Juche, ambayo inapinga kufuata dini yoyote rasmi. Ikiwa madai haya yangekuwa ya kweli, ni dhahiri kwamba yangekuwa habari kubwa katika vyombo vya habari vya kimataifa, lakini hilo halijatokea.

Nafasi ya Uislamu na Ukristo Korea Kaskazini
Ukristo unachukuliwa kama tishio kubwa zaidi kwa serikali ya Korea Kaskazini, hasa kutokana na historia yake ya kuhusishwa na mataifa ya Magharibi. Wakristo wanaoshiriki ibada za siri hukabiliwa na mateso makali, kukamatwa, na mara nyingine kupelekwa katika kambi za kazi. (Tazama hapa na hapa)

Ingawa kuna taarifa chache kuhusu Waislamu nchini Korea Kaskazini, dini yoyote isiyoidhinishwa na serikali, ikiwemo Uislamu, inadhibitiwa vikali. Serikali huona imani za kidini kama tishio kwa itikadi rasmi na utii wa wananchi kwa kiongozi wa taifa. (Tazama hapa)
Kim jong.png


Wakuu katika pitapita kwenye mitandao ya kijamii nimekutana na hii taarifa inayodai kuwa Kiongozi Mkuu wa North Korea, Kim Jong Un amesilimu na kuwa Muislam. Ni jambo zuri sana kwake, na naamini hii itapelekea wakorea wengi kuhamia dini hiyo.

SubhanAllah, MashaAllah, Alhamdolillah
 
Masikini mnahangaika sana kueneza dini yenu kwa mabavu na propaganda ila kwa bahati mbaya dunia ya leo vinazaliwa vizazi ambavyo vinajua kuhoji na vinatumia akili kuliko hisia, ndio maana mnaona watu wengi siku hizi wanaanza kuachana na hizi dini na huko tunakoelea dini zinazidi kufubaa kwahiyo hata ikitokea uislam ukaenea dunia nzima, hautakuwa ule wa itikadi kali kama sasa hivi wengi watakuwa waislam kwa majina tu ila hawata practice uislam ipasavyo hivyo hautakuwa na impact yoyote
 
Masikini mnahangaika sana kueneza dini yenu kwa mabavu na propaganda ila kwa bahati mbaya dunia ya leo vinazaliwa vizazi ambavyo vinajua kuhoji na vinatumia akili kuliko hisia, ndio maana mnaona watu wengi siku hizi wanaanza kuachana na hizi dini na huko tunakoelea dini zinazidi kufubaa kwahiyo hata ikitokea uislam ukaenea dunia nzima, hautakuwa ule wa itikadi kali kama sasa hivi wengi watakuwa waislam kwa majina tu ila hawata practice uislam hivyo hautakuwa na impact yoyote
Jadda, umepotea sana madam.
 
Masikini mnahangaika sana kueneza dini yenu kwa mabavu na propaganda ila kwa bahati mbaya dunia ya leo vinazaliwa vizazi ambavyo vinajua kuhoji na vinatumia akili kuliko hisia, ndio maana mnaona watu wengi siku hizi wanaanza kuachana na hizi dini na huko tunakoelea dini zinazidi kufubaa kwahiyo hata ikitokea uislam ukaenea dunia nzima, hautakuwa ule wa itikadi kali kama sasa hivi wengi watakuwa waislam kwa majina tu ila hawata practice uislam hivyo hautakuwa na impact yoyote
Mkuu mbona hujanijibu vizuri, ila muislamu ni muislamu hata akiwa mlevi wa pombe, wengi huacha ila sio dini ya Uislamu yenyewe inazidi kushika mizizi kwa nchi zile ambazo zili beza uislamu mwanzoni
 
Sheikh wangu umehamia lini kwenye ukuristo? Mi mwenzetu tunakujua leo hii unataka wapa sifa hao makafir?
Mkuu mkuristo alio "huru" manaake ni Muislimu ni wale wa ahal li-kitabu sio hawa walio chakachua toureti na Injili kwa kuingiza maneno yao na kufuata binaadamu wenzao mkristo alio huru hawezi kuabudu masanamu.
 
Kwani dunia ni nchi moja? Ukuristo kama mfumo hauwezi kiongaza dunia kwasbb hawana muongozo wa maisha.
Tunapoongelea kuongoza dunia tunaongelea kuwa na uwezo wa kifedha,kimamlaka,kivita, kiuchumi na kadhalika,,,nchi zinazoongoza ni nchi za kikristo,asa huo uislamu unaongozaje dunia,jibu kwa hoja ya kueleweka???
 
Tunapoongelea kuongoza dunia tunaongelea kuwa na uwezo wa kifedha,kimamlaka,kivita, kiuchumi na kadhalika,,,nchi zinazoongoza ni nchi za kikristo,asa huo uislamu unaongozaje dunia,jibu kwa hoja ya kueleweka???
Mkuu nchi za kikuristo ni zipi hizo? au unamanisha za kishogaa?
 
Back
Top Bottom