Tetesi: Kiongozi mwandamizi ajitolea kumtetea Mbowe mahakamani asema hata Mkapa alimtetea Profesa Mahalu pale ilipolazimu!

Tetesi: Kiongozi mwandamizi ajitolea kumtetea Mbowe mahakamani asema hata Mkapa alimtetea Profesa Mahalu pale ilipolazimu!

Kiongozi mmoja mstaafu aliyehudumu katika awamu ya kwanza hadi ya nne na ambaye hayati Magufuli alisema Rekodi yake haitavunjwa amesema atamtetea Freeman Mbowe mahakamani endapo Peter Kibatala atatoa baraka zake.

Mstaafu huyo amesema anamjua Freeman na anaijua Chadema lakini pia anazijua fitna za Wanasiasa wenye ngozi nyeusi.

Mzee huyo amedai ilikuwa ngumu sana mzee Mkapa kumtetea Mahalu ila alipomaliza aliwapa wosia mzito.
Mabele marando? Au Jaji Josef Sinde Warioba
 
Mahakama ya Tanzania Haina ubavu wa kumuita raisi aliyeko madarakani kizimbani narudia tena Haina ubavu huo.

Raisi ni muhimili uliojichimbia sana kuliko yote.

Hii mihimili mingine Bunge/Mahakama ni vivuli tu vya Serikali.

Ndio maana Serikali ikisikia neno"katiba Mpya" inashikwa na tumbo la kuendesha!
Katiba mpya ni mwiba kwa Rais
 
Aende tu mbona kuna mabalozi lundo toka mwanzo, ndio uhuru wa mahakama huo, Samia apewe hongera zake.
Apewe ongera KWa lipi, kubambikia watu KESI, ? lini mtakua na akili timam na kuacha sifia ujinga,

Eti anafanya miradi ,anajenga sijui vitu GANI, swali pesa anatoa mfukoni mwake ? Si ni mamikopo ambayo Mimi na wewe,watoto wetu, wajukuu zetu tutailipa

Upambe huu hauna afya KWa nchi na Rais, Rais Mwinyi Zanzibar ameukataa ujinga wa namna hii ,sifia tu, Very shame
 
Mtaa gani acha uongo
Hii ni juzi!
FB_IMG_1645095684327.jpg


Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Huyo Magu ndio kituvo cha huu uovu unaoendelea leo hii.
Acheni kujidhalilisha kwamba vichwa vyenu havina muunganiko na macho.

1. Umesahau namna gani Magu alivyoipangua hii kesi kwa kuwa alipowaambia wampelekee ushahidi wakawa hawana na wamekuja kukiibua baada ya yeye kulala?

2. Kama Magu ndiye ibilisi wako, sasa hayupo, ni Magu huyo aliyekataa kuibariki hii kesi ndiye anayewapa amuri mahakama wafanye wanayofanya?

3. Kama hawa waliopo kwako ni malaika, na wameweza kubadili mambo mengi ya Magu likiwemo la mikataba ya wachina, n.k, kwa nini hili kama wanajua ni ovu, wanaliendeleza kama shutuma zako kwa marehemu ni za kweli?

4. Acheni kujiondoa ufahamu hadi watu wawadharau kwamba hamwezi kufanya mambo kwa ufahamu.

5. Wakati anauawa Mwangosi kwa kupigwa bomu makusudi tena mchana kweupe pale Nyororo, na kisha waandishi wa habari kuanza kufukuzwa kwenye mashamba ya mahindi wakitakiwa wanyang'anywe kamera zao ili picha zile zisitoke, na baadaye wakasema "CHaDEMA wamemuua mwandishi wa habari kwa kumpiga bomu", na baadaye picha zikarushwa chapu chapu zikionyesha anauawa kwa bomu na askari wa polisi wakiwa wamemzunguka wanampiga na rungu kama nyoka, mwangosi anag'ang'ania miguu ya RPC, ambeya hata hivo hakuweza kumwokoa na mtutu wa bomu, utumbo wake ukatawanywa hadharani, na kesi ilivyoendeshwa kkisanii kila mtu akiona, na hukumu iliyotoka , ili kuwa ni enzi ya Magufuli?

6. Wakati Dr. Ulimboka anatekwa na watu wasiojulikana, wakamg'oa meno na kucha bila ganzi kisha kumtumpa Mabwepande, wakidhani kafa, ilikuwa ni siku za Magufuli?

7. Wakati watu wasiojulikana walilpokuwa wanazingira nyumba za viongozi wa CUF zanzibar, wakiwa na magari yanayojulikana, wanawachukua kwa nguvu, na kuwapoteza, ama kuwatupa wakidhani wameshakufa, ilikuwa ni enzi ya Magufuli?

8. Ikiwa Magufuli, ameanza utawala kayakuta haya mambo yakifanyika tena kwa viburi na dharau, ameasisi vipi?
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Lawama kwa waliokufa ambazo si za kweli zinawaletea laana na kuwaweka mbali na Mungu mwenye Kweli na Uweza wote. Kama huna hakika ya jambo, au huna sababu ya kusema, nyamaza. Kumchafua mtu kwa kumsingizia uwongo kunawatengenezea mambo magumu sana safarin mwenu. Wananchi watawadharau kwamba hamna uelewa na ama ni wadanganyifu mnaendeshwa kwa mihemuko na chuki na hivoy vivyo hivyo hamwezi kutenda haki. Ama uelewa wenu hautoshi.
Tafadhari sana lindeni hekima ya Mbowe.
 
[emoji120]Haya bhana!

[emoji871]Mlipewa Sabaya na akachukuwa Mbowe.

[emoji871]Mmepewa mazungumzo, Mbowe amepata kesi ya kujibu.

[emoji871]Mama anajua kucheza na akili zenu.

[emoji871]Halafu muda kidogo huko mbele Sabaya atapata msamaha.
Suala la Sabaya usililinganishe na Mbowe.
Mbowe anagusa maslahi ya watawala wenye hofu.

Sabaya analalamikiwa na watu binafsi . Watu binafsi waliumizwa na Mwovu mkuu na Ibilisi Majinuni Sabaya Mwana wa Lusifer. Watu waliumizwa sana na Sabaya na akajilimbikizia fedha za wizi.

Mbowe ni Kiongozi wa Chama kikubwa. Hakuna mtu aliyewahi kulalamika kuwa amedhulumiwa na Mbowe zaidi ya uovu wa kina Kingai na Mahita. Fuatilieni hata hao watu kama nyuma yao Kuna wema au ni jamii kama Ile ya wale wa Mtwara. Watu wanaojipendekeza Kwa kuumiza wengine ili wapate fedha na Vyeo. Mbowe ni mtoto wa Bilionea aliyemsaidia Nyerere kuleta uhuru huwezi kumlinganisha na Sabaya au Kingai au Siro au Urio. Hao ni watu hata Mali zao zina walakini ni Mali zilizopatikana Kwa Rushwa na ukatili dhidi ya binadamu wenzao.

Hivi Kingai akichunguzwa na Mali alizo nazo nani atatakiwa kwenda jela Kwa Uhuju Uchumi?
Mbowe amedhulumiwa sana Mali zake lakini wapo Watu ndani ya CCM ambao hawana hata rikodi ya walipoanzia Wala kutokea lakini wanapata mpaka uongozi wa Chama. Wote tunamkimbuka Jastini Nyari aliyekua anafanya biashara hatamu ya madini na uovu Mwingine lakini alikua ni Kiongozi mkubwa wa Chama mkoa wa Arusha.
Kuna Mwingine juzi ametuambia ana nyumba 500 na mabasi 60 na ngombe 7000 ,mnajua historia yake akiwa Tanga? Alifanya lini biashara halali mpaka akafikia hapo. ? Je,anafanya siasa za kistarabu Kwa wapinzani wake ? Ameaminika Vipi mpaka anaongiza Chama mkoa na kuwa mjumbe wa Neki.?

Waovu wameshika fedha nyingi hivyo wanaweka mitandao ya kulinda uovu wao.

Bahati iliyopo ni kwamba Mbowe hajapata bado watu wakumpambania kiroho na kiasili.
Hao wanaombambikia kesi za dhulma wangetembelea ndala tofauti na familia zao kubaki zinajuta. Ni bahati kuwa waovu wanafanya hila halafu wananufaika juu ya damu za watu bila kukutana na adhabu hata kusomewa albadiri wakawa vipofu au kubadilika wakawa vichaa.
Waliopo kwenye madaraka mara nyingi ni Wajanja wanatuambia tuwaombee Kwa Imani zetu jambo linalowapa ulinzi mkubwa sana Kiroho. Matokeo yake wanajisahau na kujiona ni miungu.
 
Sasa hao wazee na hao wanasheria wabobezi itakuwaje
 
Aende tu. Ni haki yake. Ila asijulikane kabla ya kupanda kizimbani. Atatishwa sana.
 
hv mnakumbuka enzi za magufuli na kesi ya chadema pale alivyosema mahakamani c kanisani kwenda kuimba kwaya.
 
Back
Top Bottom