Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

Acha dharau, ulipo sema makengeza Nikajua Nia yako moyoni ni ipi. Umejaa chuki kwa Mbowe hata ukiulizwa sababu huna. Unaleta misemo eti serikali in mkono mrefu, mbona huo mkono hauonekani kwenye Mambo ya ufisadi au mbona haukuonekana kwenye kesi ya Hamza alipowapiga risasi polisi. Kama mipango miovu kwa Mbowe serikali imefanya mpaka imechoka.

1. Kavunja bilcanass
2. Kuharibu shamba la Mbowe.
3. Kufurushwa nje kampuni yake kwenye Jengo la NHC, ambalo kimsingi lilikuwa la babaake.
4. Kufungiwa kwa gazeti lake.
5. Kuhukumiwa nje ya utaratibu was kisheria, Kama mahakama ya Kuu ilivyosema.
6. Kafungiwa akaunti zake zote za benki.
7. Kuibiwa pesa zake wakati akaunti imefungwa.
8. Kushambuliwa na wasiojulikana na kisha kumsingizia amelewa.
9. Kufunguliwa kesi ya ugaidi .
Hana akili ya kukuelewa
 
na mkicheza anafungwa hivyohivyo kimchongo mwenzenu ateseke nyie na uenyekiti mumnyang'anye
Lissu analeta uanaharakati katika vitu vinavyohitaji hekima.

Yeye hakubaki humuhumu nchini na kuishinikiza serikali imhakikishie usalama wake Ila anadhani anaweza kuishinikiza serikali hiyohiyo imuachie Mbowe bila masharti wakati imeshaamua kucheza faulo!

Busara, Busara, Busara
Siyo kila kitu kinahitaji uanaharakati
 
Sasa wanahangaika nini? Ohh mara chadema hawakuhudhuria mkutano ooh sijui wamenuna?. Nyie si mlisema ni Gaidi??

Onyesheni ugaidi wake sasa sio muombe kuombwa msamaha[emoji28][emoji28][emoji28]
Ndo maana tunataka kesi iendelee mahakamani ili ijulikane mbivu na mbichi.
 
Ya Jiwe muachie Jiwe. Mama hana shida kabisa shida iko kwa CDM, kundi la wahuni
MAMA Ni muhusika na huu umbambikiaji. Lazima mjue HAKUNA MWANADAMU ANAJUTA KWA KUONEWA KWA HIYO KUMUONEA MBOWE USITEGEMEE KUWA ATAJUTA. MSHAMFANYIA MABAYA MENGI TU KWA UONEZI HAJAJUTA MPAKA MKAMPA UGAIDI SASA. Unamtetea mama kwa lipi? Mbona Magufuli alimtoa babu seya mlipombambikia kesi na kumfunga?. Mama anahusika na ndiyo maana alijikanyaga alipojojiwa na bbc
 
Huijui serikali vizuri mzee, Mbowe ni takataka tu, Aliuawa MKURUGENZI WA TAIFA MSTAAFU KISA KUMSHABIKIA MREMA, SEMBUSE HUYO CHIZI WENU MAKENGEZA MBOWE?? Hivi nyie mkisikia SERIKALI ina mkono mrefu huwa mnaelewa nini??
Tuliza makalio creche...
 
Jitihada za kumaliza kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, zinaendelea “nyuma ya pazia,” ambapo taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, amekutana na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana, na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athumani.

Haijaweza kufahamika kama jitihada hizo ni za Mnyika binafsi au zina baraka ya chama hicho, ambacho kwenye mitandao ya kijamii kimetanabaisha kuwa hakitaki suluhu yoyote kuhusiana na kesi hiyo.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba kimsingi Mama Samia Suluhu aliridhia ombi la kuachiwa kwa Mheshimiwa Mbowe na ilitarajiwa aachiwe kwa “nolle prosequi” (tamko la nia ya kutoendelea na mashtaka) ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) lakini “yaliyojiri kabla, wakati na baada ya mkutano wa vyama vya siasa huko Dodoma” yalipelekea mpango huo kukwama.

Licha ya jitihada hizo za Mnyika, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Masoud Othman nae aliwasilisha maombi ya Chadema kwa Mama Samia, na akashauri Mheshimiwa Mbowe aachiwe bila masharti yoyote.

Uamuzi wa Chadema kususia mkutano huo wa vyama vya siasa huko Dodoma ambao ulifunguliwa na Mama Samia, inatajwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kukwama kwa mpango huo wa kumwachia Mheshimiwa Mbowe.

Taarifa hizi zinakinzana na kauli zinazoongewa na viongozi na wafuasi wa chama hicho kuwa “hawako tayari kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe” kwa sababu wanaamini kuwa hana hatia na mashtaka dhidi yake ni ya kutungwa.

Yawezekana tofauti hizo kati ya “kinachoendelea faraghani” na “kinachoongelewa hadharani” zikawa ni mkakati wa Chadema hasa ikizingatiwa kuwa wafuasi wengi wa chama hicho hawaafiki kabisa wazo la kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe. Moja ya sababu zinazochangia “msimamo huo mkali” ni shinikizo la “wanaharakati wa mtandaoni” ambao wanapinga vikali siasa za maridhiano kati ya chama tawala CCM na vyama vya upinzani.

Hata hivyo, suala hilo la kesi ya Mbowe “limevamiwa” pia na kundi moja ndani ya CCM linalompinga Mama Samia, na ambalo linaiona kesi hiyo dhidi ya Mheshimiwa Mbowe kuwa yenye manufaa kwa kundi hilo kwa sababu inatoa taswira mbaya kuhusu Mama Samia.

Nihitimishe kwa kutanabaisha kuwa haitokuwa jambo la kushangaza endapo Mheshimiwa Mnyika atakanusha taarifa hizi kwa sababu “zinaweza kumletea tabu” katika chama z
Hii kamba DO hayupo bongo
 
Hivi kumbe hukuitoa ile mimba ya Sabaya? Miaka 30 mingi utamlea mtoto kama singo mama...
Tatizo lako unafikiri kila mtu alipigwa mimba na sabaya kama ulivyo wewe
 
Hii ndio inafanya wasifute hiyo kesi, we unadhani wao ni wajinga? Hivi unadhani serikali kama ingekuwa na nia mbaya na Mbowe so hata wangemtengenezea ajali?? Hivi huwa mnawaza kwa kutumia nini??
Ajali ni mambo ya kizamani enzi za akina Dube.

Hii ni dunia ya kidigitali bwashee!
 
Yaani ashachafuka,,na nadhani hawatakuja wakurupuke Tena kuwapa viongozi wa Chadema Bogus cases
Tangu hili li case lianze watu Hadi wameanza kumshambulia mno wamesahau na mazuri yote awafute kazi wahuni waliomuingiza mkenge kwenye hii case aisee
 
Huijui serikali vizuri mzee, Mbowe ni takataka tu, Aliuawa MKURUGENZI WA TAIFA MSTAAFU KISA KUMSHABIKIA MREMA, SEMBUSE HUYO CHIZI WENU MAKENGEZA MBOWE?? Hivi nyie mkisikia SERIKALI ina mkono mrefu huwa mnaelewa nini??

Aisee. Dunia inaenda mbio. Hii sio classified information tena? Waliotengeneza assassination ile wote hawapo. Mzee wa Kiraracha naye keshafifia.

Hakuna mkono mrefu. It’s plain cold blooded murder by state tyranny. It’s a no brainer. Serikali inaweza kuua mtu yeyote mahali popote na kusingizia chochote. Hakuna wa kuhoji. Ni kitu cha kujivunia?
 
Back
Top Bottom