WaTANGANYIKA hamjayazoea mambo ya aina hii !! Mnahitajia uamsho ili kusimama kidete na kutorudi nyuma. Ni majuzi tu mliwazomea WaZanzibari na kuwaita magaidi au materoristi na kuisifu serikali hihii mnayoibeza ,WaZanzibari wapo juu ya mstari wa Katiba kudai madai yao kisheria ,mlipoambiwa waliohujumu makanisa sio kutoka uamsho hamkusikia la mkuu leo guu ndio hilo limevunjika ,mnafikiri wenzenu waZanzibari wataungana na nyinyi kivipi ?? Wakati wanapopewa kibano huwa mnashangilia na kuleta hoja za ajabu ajabu ,akina Mwanakijiji mko wapi katika hili mbona hamsemi ??? Ni Serikali ya Muungano huo ndio unaofanya vitendo hivyo au sio.
UPANDE WA PILI WA SHILINGI
Sasa kwa upande mwingine naweza kusema inawezekana kabisa serikali haihusiki na janga hilo , tusifuate ushabiki au jazba ,katika hali ya kisiasa iliyopo leo Tanzania ,jambo lolote linaweza kutokea.
Wapinzani wanajua fika kuna mgogoro kati ya serikali na Madaktari mbali ya taasisi zingine,huu wa madaktari ni mkubwa na unaowavutia wananchi wengi sana. Technically kuitia serikali kwenye kitanzi ni kuwafanyia ushenzi viongozi wa mgomo huo kama alivyofanyiwa Ulimboka na upinzani kuwarushia Serikali kuwa ndio waliotekeleza ili kuwazima madaktari ,tayari serikali itakuwa imeshatiwa doa na pengine kuzidi kwa vurugu.
Serikali nayo inaweza kusema kuna Chama pinzani kimetekeleza uovu huu na uchunguzi unafanywa kubaini ni nani mhusika mkuu , kilichobaki ni huyo jamaa kutoka salama inaweza ikasaidia ,mnakumbuka kesi ya kifo cha Chacha ,dereva alipona ile kesi sijui imeishia wapi kwani ni kati ya serikali na CDM ndio mmoja wao alihusika,lakini hadi leo kimya.
Kisiasa ili kuiangusha serikali au upinzani kupata nguvu ni kutafuta njia yeyote ile ,sasa hii inaweza kuwa njia moja kuipotezea mvuto serikali kutoka kwa wananchi.
Sidhani kama serikali inaweza kuwa mhusika mkuu katika hili na kama imefanya basi walioshauri hawaitakii mema serikali iliyopo madarakani.