Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Ni Uchambuzi mzuri lakini naomba nipingane na wewe kwenye umalizio wako au niseme ungeongeza point ya Serikali yenyewe kuhusika moja kwa moja kuyafanya hayo.

Huwezi kuitoa serikali kwa kigezo eti ni utoto kufanya hivyo. Tumeshuhudia serikali ikifanya mambo mengi sana ya kitoto kabisa au mengine hata mtoto hawezi kuyafanya, sihitaji kuyasema kwani yanafahamika sana.

Kwa hiyo hatuwezi kuitoa kuhusika, ni moja kati ya makundi ya watuhumiwa uliowataja katika kisa hiki

Mkuu wangu coby,
Ni kweli katika tasnia za ukachero si busara hata kidogo kupuuza uwezekano wa aina yoyote katika jambo kama hili. Hata hivyo, labda tu nifanye usahihisho ili kuweka rekodi sawa. Suala la serikali kufanya jambo kama hilo si tu kwamba ni la kitoto bali ni jambo la hatari kuliko hatari yenyewe. Hivyo basi, pamoja na ukweli kwamba serikali inaweza kufanya jambo la kitoto lakini sizani kama inaweza kufanya jambo la hatari kama hilo ambalo madhara yake kwa taswira ya serikali ni makubwa mno. Ni serikali chache sana, ambazo hususani ni za kidikteta wa wazi ndio wanaweza kufanya jambo kama hilo.

Labda niongeze possibility nyingine katika mambo kama haya. Hata wananchi wa kawaida wanaweza kufanya alichofanyiwa Ulimboka. Just imagine, mtu amepeleka ndugu kipenzi halafu akafa kwa kukosa huduma huku yeye akiamini kwamba pamoja na kwamba madaktari wana madai lakini sio busara kwao kuacha watu wanakufa. Mtu au watu wenye mawazo kama hayo wanaweza kumtendea mbaya Ulimboka kama njia ya kulipiza kisasi.

Na wengine wanaweza kutaka kutoa ujumbe kwa Ulimboka na wenzake waone uchungu wa kuuguliwa....! Wahenga wanasema, ukitaka kujua kifo kachungulie kaburi!
 
...tusikimbilie kutuhumu... kwenye mgomo wao wa mwisho, mi na wenzangu tulikuwa tukiwinda daktari yeyote, "tumnyonye macho" baada ya mshkaji(holder of top secret) wetu kukosa huduma muhimbili kwa siku nzima alikopelekwa kutokana na kuvunjika mguu kwenye ajali...sijui waliomfanyia hayo ulimboka watakuwa kina nani, na kwa sababu zipi....mungu amjalie salama tabibu!...wao (matabibu), ni wana taaluma ambao mgomo wao, haukubaliki na haueleweki hata kidogo na yeyote yule mwenye bahati mbaya ya kuhitaji huduma yao ktk kipindi ambacho wamegoma!

Inasemekana alichukuliwa au kutekwa jana usiku na watu wa.......
 
Nimepata habari toka kwa rafiki yangu aliyeko Muhimbili, kwamba sasa hivi madaktari wa MOI wamempeleka Ulimboka kwenye MRI kwenye hospitali ya MNH lakini waandishi wa habari wanahaha kupata picha bila mafanikio kwa makamera yao, maana Ulimboka kafunikwa na haongei.
 
Ujumbe amenitumia Daktari yupo pale MOI
‘Kaka Zitto,hali ya Dr.Ulimboka yuko unconscious,multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya,yuko icu wanamstabilise kwanza kwasababu hapumui vizuri,the situation here is really bad,I agree with you this is outright outrageous’
Nimechukizwa sana na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dr Ulimboka, Kiongozi wa Madaktari Nchini. Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika Taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko. Nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dokta Ulimboka na kujulishwa kwamba majeruhi huyu wa vitendo vya hovyo kabisa kutokea hapa nchini alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa MagwePande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.
Serikali kama mlinzi wa usalama kwa raia inaWAJIBU kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake. Serikali INAWAJIBIKA kueleza katika nyakati kama hizi ambapo kuna mgogoro kati yake na madaktari imekuwa wapi kuhakikisha usalama wa viongozi wa madaktari ili kuepusha watu wanaoitwa ‘agente provocateure‘ kuweza kuhatarisha hali ya amani ya nchi na hata kupelekea kuweka hali ya vitisho kwa madaktari wetu.
Serikali INAWAJIBIKA kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.
Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya wa CHADEMA kufuatilia suala hili kwa kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote na ukweli mtupu unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake. ‘An injury to one, injuries to all’
Naomba madaktari wamwangalie kwa karibu daktari mwenzao ili aweze kupata nafuu. Ulinzi uimarishwe ili kuhakikisha usalama wake.
 
Habari mbaya kabisa kuisikia kwa maslahi ya wtz ni hii hapa. Naona serikali dhaifu imeamua kuanika udhaifu wake kwa kutangaza vifo vya wanyonge waziwazi. Hatua waliyochukua haitakomesha mgomo wa madr bali ndo itauzidisha na mwisho wa yote ni chachu ya kuwang'oa madarakani
 
ma dr inabidi wasirudi nyuma kwa pigo hilo wakaze uzi zaidi, tumuombee apone mapema aendeleze mapambano
 
Wataweza kuua mwili tu, lakini ROHO iko salama, na mwenye kuamua ukomo wa maisha wa mtu ni MUNGU na wala sio Mwanadamu, kwetu sisi hio ni changamoto tu, wote tutakufa na hata hao wauwaji watakufa, suala ni muda tu. MUNGU ninaemwamini na kumtumikia atamponya tu. Amen
 
serekali wala haihusiki na hilo tukio, hili jambo limesha kuwa la kisiasa na njia moja nzuri ya kuichafua serikali ni kufanya vitendo kama hivi, hii itakuwa ni CHADEMA.
 
Ni makosa km bado anahema. Wangemaliza kazi twende sawa. Jiulize ni watz wangapi wameshafariki kwa migomo hii isiyo kichwa wala miguu.

wewe si mzima bila shaka umerogwa na aliyekuroga ameshafariki.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Khaaa serikali yetu inaufinyu wa mawazo na kwahili wameongeza matatizo na sio kutatua wala kupunguza tatizo. Watanzania tuamuke na tusimame kidete ktk hili!
JINSI YA KUMSINGA (massage) na KUMSUGUA (scrub) MWENZA WAKO KWA KUTUMIA VITU ASILIA.
Binadamu wote lazima tuchoke wakati fulani na kupata maumivu ya viungo vya miili yetu.Basi si kila siku tuwe tunakimbizana kwenye massage spas,siku moja moja unatakiwa umsugue na kumsinga mwenzio nyumba.




















Oga vizuri kabla ya kuanza, shughuli hii inaweza fanywa kitandani au kwenye mkeka. Unaanza kuusugua mwili wote kwanza kwa kutumia unga wa liwa ulichanganywa na maji ya rose pamoja na machicha ya nazi au unga wa manjano uliochanganywa na maji ya rose pamoja na machicha ya nazi. Sugua mwili mpaka uhisi uchafu na nongo zote zimeisha.Baada ya hapo unaoga nakurudi kwa ajili ya kusingwa.Unachukua mafuta ya mzaituni,ya nazi au ya ufuta unampaka mwili mzima na kuanza kumsinga(kummassage) taratibu na kwa upendo alafu unachukua unga wa karafuu na kuunyunyuzia mwilini sana sana sehem za mgongoni na kiunoni(unga huu usiguse sehem za siri,unawasha).Utaendelea kumsinga mpaka utakaporidhika unamuacha akae na ule unga kama dakika 15 hivi,akipitiwa na usingizi muache apumzike akiwa macho*akaoge au ukamuogeshe alafu kitakacho fuata I.T.V hatutaki kujua..........


Kusugua na kusinga mwili inasaidia kuondoa uchafu mwilini,kupunguza maumivu makali mwilini,inakufanya upate pumziko na kuondoa usongo wa mawazo , kutaiwezesha mishipa ya damu kuwa katika hali nzuri na hivyo kurahisisha msukumo wa damu katika mwili wako.Pia huleta furaha kwa wale wawili wapendanao.

MAHITAJI NI KAMA YA FUATAYO



MACHICHA YA NAZI


UNGA WA KARAFUU


UNGA WA LIWA

*MAFUTA YA KARAFUU




*UNGA WA MANJANO

*MAFUTA YA MZAITUNI

MAJI YA MAUA WARIDI

Nyongeza: kwenye swala la mafuta unaweza tumia mafuta ya nazi,ya ufuta au yoyote yale ambayo hayataleta mchubuko wakati wa kusinga. Kusugua na kusinga inaweza chukua dakika 45 mpaka 60 na baada ya hapo pumzika kiasi kisha unaweza kwenda kuoga. Wataalam wanashauri baada ya kuoga utembee kidogo ili kuuweka mwili sawa kabla ya kwenda kulala.

Mafuta ya karafuu unaweza yatumia peke yake*kuchua sehemu zenye maumivu makali*kama kiunoni,shingoni,mgongo na miguu.

KWA ATAKAE HITAJI UNGA WA LIWA,MANJANO NA KARAFUU, MAJI YA ROSE NA AINA MBALIMBALI ZA MAFUTA YA KUSINGA KARIBU SANA DUKANI KWANGU*EmC's CHOICE SINZA MAPAMBANO 0654450200
Evelyne Michael at 4:49 AM
Share

0 comments:
Post a Comment
›
Home
View web version
About Me


Evelyne Michael
I am a Zigua from Tanga,Tanzania.The first born in a family of five children.I am a holder of Bacherol of Law Degree and a Postgraduate Diploma in Human Reso

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
...GOD'S PLAN! Things started this way in many other countries ...
 
Back
Top Bottom