Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Mkoa wa Kagera, Seth Niyikiza amefariki dunia akiwa kajifungia ndani mwake.
Akithibitisha tukio hilo leo Jumatano Februari 26, 2025 Kamanda wa Polisi mkoani humo, Brasius Chatanda amesema mwili wa wakili huyo ulibainika baada ya mteja wake kwenda nyumbani kwake kufuatilia kwa nini haudhurii kesi yake mahakamani.
"Alilala, hakuonekana mpaka mteja wake amekuja mahakamani hamuoni... ndio akaamua kwenda nyumbani kufika akafanikiwa kusukuma geti, kuingia eneo la ndani akakuta kuna inzi...yaani kuna ‘movement’ ya inzi nyingi kwenye dirisha hali ambayo ilimshtua ikabidi awashirikishe majirani," amesema.
Amesema baada ya majirani kuona hali hiyo wakaamua kuvunja mlango na kumkuta amefariki na mwili umeharibika.
Kwa mujibu wa kaka yake, Laurent Seth mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera mjini Bukoba, wakisubiri kufanyiwa uchunguzi ili kujua chanzo cha kifo chake.
"Alilala, hakuonekana mpaka mteja wake amekuja mahakamani hamuoni... ndio akaamua kwenda nyumbani kufika akafanikiwa kusukuma geti, kuingia eneo la ndani akakuta kuna inzi...yaani kuna ‘movement’ ya inzi nyingi kwenye dirisha hali ambayo ilimshtua ikabidi awashirikishe majirani," amesema.
Amesema baada ya majirani kuona hali hiyo wakaamua kuvunja mlango na kumkuta amefariki na mwili umeharibika.
Kwa mujibu wa kaka yake, Laurent Seth mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera mjini Bukoba, wakisubiri kufanyiwa uchunguzi ili kujua chanzo cha kifo chake.