TANZIA Kiongozi wa TLS Kagera, Seth Niyikiza akutwa amekufa nyumbani kwake

TANZIA Kiongozi wa TLS Kagera, Seth Niyikiza akutwa amekufa nyumbani kwake

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Mkoa wa Kagera, Seth Niyikiza amefariki dunia akiwa kajifungia ndani mwake.

1740561848953.png
Akithibitisha tukio hilo leo Jumatano Februari 26, 2025 Kamanda wa Polisi mkoani humo, Brasius Chatanda amesema mwili wa wakili huyo ulibainika baada ya mteja wake kwenda nyumbani kwake kufuatilia kwa nini haudhurii kesi yake mahakamani.

"Alilala, hakuonekana mpaka mteja wake amekuja mahakamani hamuoni... ndio akaamua kwenda nyumbani kufika akafanikiwa kusukuma geti, kuingia eneo la ndani akakuta kuna inzi...yaani kuna ‘movement’ ya inzi nyingi kwenye dirisha hali ambayo ilimshtua ikabidi awashirikishe majirani," amesema.

Amesema baada ya majirani kuona hali hiyo wakaamua kuvunja mlango na kumkuta amefariki na mwili umeharibika.

Kwa mujibu wa kaka yake, Laurent Seth mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera mjini Bukoba, wakisubiri kufanyiwa uchunguzi ili kujua chanzo cha kifo chake.
 
Kwani alikuwa team kataa ndoa, mbona picha inaonesha ni mtu mzima aliyewahi kuoa? Anyway, poleni wafiwa
 
Back
Top Bottom