Kiongozi wa umma kumiliki vitu vya anasa huku kundi la unaowatawala wakipitia dhiki haijengi taswira nzuri

Jamani Jamani Jamani!
Uchawi siyo Lazima ufuge Nyoka!

Ngoja nikwambie

Kwanza Rais wetu ni Mwanamke!

Kuvaa vizuri ni Sifa kwetu Sisi wananchi wake tuliomchagua!

Saa ya Milioni Mia mbona ni kitu kidogo sana!

Mbona hamuongelei Kamati za Harusi zinachangisha Tsh 150M kwa ajili ya kuozesha tu Binti wakati ndani ya wanafamilia kuna watu wanashindwa kumudu Mlo wa Siku moja?

Tuongee vitu vyenye kujenga bhana tusiongelee ati saa ys 100M!
By the way kwani hiyo saa ni ghali sasa?

Nenda kwenye gallery za saa ujue thamani ya saa

Arnold Shawzneeger hivi majuzi amevaa saa ya almost 1bn.



Sent from my SM-A307FN using JamiiForums mobile app
 
Hiyo Lodge tu ya kawaida hata wilayani watu wanazo acheni uongo uongo!
 
Sasa kama kiongozi huoni aibu ya kuvaa saa mkononi ya Tsh 100+ mkononi katikati ya lindi la umasikini wa watu wako waliokosa fursa ya mlo mmoja tu kwa siku.
Itakuwa mali za huyu kiongozi za uficho achilia mbali za wazi ni za matrilioni ya shilingi.
Ni kiwango cha juu kabisa cha dalili ya mtu asiyejali na wala asie na chembe ya utu.
 
Ukiniambia anatafuta sifa na heshima naweza kukubaliana na wewe, lakini Mbowe ha-hemei siasa ili apate kula, tayari ana pesa nyingi tangu utoto wake ameachiwa utajiri mkubwa. Anatafuta mambo mengine sio chakula kama wewe na wanasiasa wa ccm wanaopiga magoti ili wapate ubunge waweze kula na kujenga nyumba.
 
Acha mkuu yaogelee kwenye umaskini.Kwa maana ni ccm damu damu.
Hivyo kwao ccm ni mzazi wao.

Mabadiriko yapo Kwa waishio mjini ambapo ni wachache,lakini hayo ya vijijini hakuna kitu mkuu.
Acha wale,maana mtaji wao ndo hayo matutusa.
 
Wewe nyumbu akili huna kabisa. Kwa hiyo akiachiwa urithi ndo hapaswi kufanya tena kazi. Baba yake Mbowe alikuwa tajiri ila haina maana warithi wake ndo watulie tu watumie tu kilichochumwa na wazazi. Akili za kingese kama zako ndo zinachangia waafrika tushindwe kurithishana utajiri. Tajiri wa kibongo akishakufa na utajiri wake ndo umekufa. Badili fikra zako wewe nyumbu.
 
Hii ni laana ya CCM. Ujinga wao ndiyo umefanya mpaka watu wa aina hii wapewe urais.
 
Naunga Mkono hoja Ukiwa kiongozi Hata Kama unapesa,, jifiche Kidogo Maana walioko Nyuma Wengi Hata Kula Ni Shida.
Mkuu,

Kwa hiyo wewe tatizo lako si kiongozi kufuja pesa kwa anasa.

Akiweza kufuja pesa kwa anasa kisiri afuje tu.

Tatizo lako ni watu masikini anaowaongoza kuona kiongozi anafuja pesa kwa anasa.

Nimekuelewa vizuri hapo?
 
[QUOTE="So special, post: 49440262, member: 720861]
Tanzania kuna watu wengi sana wanaishi katika dhiki isiyo ya mfano, kama wewe ni mtafutaji wa mtaani au pembezoni mwa mji utakubaliana nami.

Tanzania kuna umasikini napo sema umasikini namaanisha umasikini kweli kama ni mtu wa ofisini tu huwezi kuelewa level ya umasikini waliyo nayo Watanzania wengi inasikitisha sana.[/QUOTE]

Nakuelewa sana mkuu.

Nimefanya kazi ya kuzunguka vijijini kwa miaka 5+.

Aisee tusichukulie poa, watanzania wengi wanaishi maisha yenye ugumu usioelezeka, si umasikini bali ufukara uliopitiliza ambao inafaa upatiwe jina jingine kabisa, naona kama jina la ufukara bado haliwatoshi kabisa! Yaani watu wanaiishi kuzimu wakiwa duniani halafu Kuna matajiri Simba na Yanga wanapewa mamilioni ya fedha yanayotokana na kodi za hao wanaolionja joto la jiwe!

Nikiona viongozi wanavyoleta utani na maisha ya watu halafu nikavuta picha za mambo niliyoyashuhudia huko vijijini huwa naumia sana.

Kuna watu wanalala sehemu ambazo huwezi kuamini kama binadamu anaweza kulala. Kuna familia zikinywa uji usio na sukari (wala chumvi) leo zinapitisha siku mbili, zikinywa na kesho ni anasa. Watu wa namna hii hata ukiwaletea stori za kujenga choo wanaona kama unawapigia makelele tu.

Inaumiza sana kiukweli.

Ndo maana nawaheshimu sana wapinzani, hata wawe na mapungufu milioni+, jitihada zao hata ziwe kiduchu kiasi gani bado zina thamani. Huwezi kuelewa vema kama hujazishuhudia tabu za watu huko ndanindani.
 
Wananchi wote ni sawa, ila wanasiasa wameongezewa kidogo mabaki ya usawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…