BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kiongozi wa upinzani wa Gabon, Guy Nzouba-Ndama, amewekwa chini ya kizuizi cha nyumbani ikiwa ni siku tano baada ya kukamatwa kwenye mpaka wa Congo akiwa na mabegi yenye zaidi ya dola milioni 2. (Tsh. Bilioni 3).
Kukamatwa kwake kulirekodiwa na kufunguliwa kwa masanduku hayo kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii. Nzouba-Ndama mgombea mtarajiwa katika uchaguzi ujao wa Urais ameshtakiwa kwa ukiukaji wa udhibiti wa uagizaji bidhaa na ushirikiano na mamlaka ya kigeni.
Chama chake, The Democrats, kinasema shutuma hizo zimechochewa kisiasa. Mzee huyo mwenye umri wa miaka 76 aliwahi kuwa Spika wa Bunge kwa miaka 19 na mshirika mtiifu wa Rais wa zamani, Omar Bongo, baba mzazi wa Ali Bongo Ondimba aliyemaliza muda wake.
Kukamatwa kwake kulirekodiwa na kufunguliwa kwa masanduku hayo kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii. Nzouba-Ndama mgombea mtarajiwa katika uchaguzi ujao wa Urais ameshtakiwa kwa ukiukaji wa udhibiti wa uagizaji bidhaa na ushirikiano na mamlaka ya kigeni.
Chama chake, The Democrats, kinasema shutuma hizo zimechochewa kisiasa. Mzee huyo mwenye umri wa miaka 76 aliwahi kuwa Spika wa Bunge kwa miaka 19 na mshirika mtiifu wa Rais wa zamani, Omar Bongo, baba mzazi wa Ali Bongo Ondimba aliyemaliza muda wake.