Prince Kunta
JF-Expert Member
- Mar 27, 2014
- 22,797
- 28,904
Don't hate the player, Hate the game...Don't be mad
Yanga waleee kuelekea nafasi yao
Yanga waleee kuelekea nafasi yao
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
1. Yanga imekuwa ikishutumiwa....= Inadhaniwa kwamba Yanga ..... = Inawezekana kwamba Yanga ina....Wakuu kama mnavyokumbuka timu ya Kagera Sugar ilifungwa na Yanga ya Dar jumla ya Goli 6 kwa 2. Na kama mnavyokumbuka Yanga imekuwa ikishutumiwa kununua ama timu nzima au baadhi ya wahezaji ili kurahisha mazingira ya ushindi wa kimbunga.
Taarifa zinazosomwa Azam TV zinasema kuwa Wachezaji wawili wa Kagera Sugar, Husein Sharifu 'Casillas Munyama' na Erick Kyaruzi wamesimamishwa na kuondolewa kambini.Wanatuhumiwa kupewa mlungura na Yanga katika kipigo cha 6-2.
TAKUKURU fanyika kazi hii timu inatia aibu Taifa.
c.c Makoye Matale na sembo
Kuna goli analaumiwa kipa kwa uzembe wake pia kuna goli analaumiwa beki au mabeki tofautisha na ujiongeze kiakiriGolikipa wa kwanza alifungwa goli 3, wakabadilisha mwingine naye akapigwa 3.... sasa hapo wote walihongwa? kama ndivyo wangesimamishwa magolikipa wote wawili kwani wote walipigwa 3.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nguvu ya tigo pesaHii ni aibu kwa taifa alafu wakitoka hapo wanajiita wa kimataifa kumbe ni nguvu za tgopesa
Naona watu humu mnalaumu simba kwa kutemwa wachezaji wa kagera,kagera wamechukua hatua kwa watu wao.simba tunahusika vipi? Huyo beki na kipa wake tulijaribu kuhoji hapa tukapigwa matusi ya kutosha.Yanga kashinda mechi nyingi kwanini watu wahoji juu ya kagera na hao wanaotegeana kuokota mpira.
Golikipa wa kwanza alifungwa goli 3, wakabadilisha mwingine naye akapigwa 3.... sasa hapo wote walihongwa? kama ndivyo wangesimamishwa magolikipa wote wawili kwani wote walipigwa 3.
Timu zote zilizofungwa na Yanga magoli mengi (kuanzia 2-0) since 2015/2016 league zichunguzwe na TAKUKURU, maana kuna mazingira ya Rushwa!!!Wakuu kama mnavyokumbuka timu ya Kagera Sugar ilifungwa na Yanga ya Dar jumla ya Goli 6 kwa 2. Na kama mnavyokumbuka Yanga imekuwa ikishutumiwa kununua ama timu nzima au baadhi ya wachezaji ili kurahisha mazingira ya ushindi wa kimbunga.
======================
Uongozi wa Kagera Sugar umewasimamisha wachezaji wake wawili golikipa Hussein Sharif ‘Casillas’ na beki Erick Kyaruzi kwa tuhuma za kuihujumu timu wakati wa mchezo wa liopoteza kwa kufungwa magoli 6-2.
Katibu Mkuu wa klabu hiyo Hamisi Madaki amethibisha kuwasimamisha wachezaji hao kwa muda usiojulikana kwa ajili ya kupisha uchunguzi juu ya tuhuma zinazowakabili.
“Tunaendelea na uchunguzi kwasababu kunaonekana kulikuwa na hujuma katika mechi yetu na Yanga kwahiyo tumeona tuendelee na uchunguzi na tumeona wakae kando wakati tunaendelea na uchunguzi huo.”
“Aina ya magoli tuliyofungwa kila mtu aliyaona na yanatia wasiwasi mkubwa. Suala sio idadi ya magoli suala ni aina ya amagoli mtu aliayofungwa, hata kama ni goli moja lakini kama linatia wasiwasi lazima tuchukue hatua.”
“Makosa ya namna ile hatukuridhika nayo ndiyo maana tunafanya uchunguzi. Hata beki goli alilofungisha unaona dhahiri kwamba halikupashwa kuwa goli ndiyo maana tunafanya uchunguzi.”
“ nikiwa kama Mtendaji mkuu wa klabu, hiyo taarifa sina sisi tumewasimamisha na hata barua tulizowaandikia tumesema tumewasimamisha . Suala la kuwaondoa kabisa hilo siwezi kulisemea, taarifa nilitoa mbele ya wachezaji na benchi la ufundi baada ya kukaa viongozi na benchi la ufundi tulikubaliana kuwasimamisha.”
“Tumewasimamisha kwa muda usiojulikana mpaka tukamilishe uchunguzi, hii si mara ya kwanza watu wanasahau historia, tumeshawahi kusimamisha wachezaji na kuwafukuza kabisa hapo kabla.”
Katika mchezo huo, Hussein Sharif alifungwa magoli matatu kipindi cha kwanza kabla ya kufanyiwa mabadiliko kumpisha David Burhani ambaye pia alifungwa magoli matatu.
Kyaruzi yeye alirudisha pasi fupi kwa golikipa wake ambapo Donald Ngoma aliuwahi mpia huo na kufunga bao.
TAKUKURU fanyika kazi hii timu inatia aibu Taifa.
c.c Makoye Matale na sembo